Tuesday 27 January 2009

West Brom 0 Man United 5!!!
Kipa Van Der Sar avunja rekodi ya kutofungwa goli kwa zaidi ya dakika 1,025!!

Mabingwa Manchester United wakicheza ugenini Uwanja wa Hawthorns waliwashindilia wenyeji wao West Bromwich Albion mabao 5-0 na kuwafanya wazidi kuongoza LIGI KUU England sasa wakiwa pointi 3 mbele ya Liverpool.
Kwa kutofungwa hata goli moja kwenye mechi hii, Man U wameweka rekodi mpya ya LIGI KUU kwa kucheza mechi 11 bila ya nyavu zao kutikisika rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na Chelsea tangu msimu wa 2004/5.
Na ilipofika dakika ya 84 ya mchezo Kipa wa Man U Edwin van der Sar alivunja rekodi ya Kipa wa Chelsea ya kucheza dakika 1,025 bila kufungwa hata goli moja kwenye LIGI KUU England, dakika ya 84 ya mechi hii ilikuwa van der Sar anaingia dakika yake ya 1,026 bila kufungwa!!!
Sasa anashikilia rekodi kwa kucheza dakika 1,032 bila kufungwa goli kwenye LIGI KUU!!
Mechi hii ilichelewa kuanza kwa dakika 30 kwa sababu Watazamaji wengi walichelewa uwanjani kutokana na msongamano mkubwa wa magari kwenye barabara zote zilizokuwa zinaelekea hapo Hawthorns.
Iliwachukua dakika 22 kwa Man U kuanza kufunga kwa goli la Berbatov.
Na kazi ya Man U ilirahisishwa pale Nahodha wa West Brom Paul Robinson alipopewa Kadi Ny ekundu baada ya kumchezea Ji-Sung Park rafu mbaya.
Katika dakika ya 43 Kipa Scott Carson aliutema mpira kufuatia frikiki ya Ryan Giggs na Tevez akauwahi na kuushindilia wavuni. Vidic akapachika la 3 dakika ya 60 na Ronaldo akafunga mawili dakika ya 65 na 73.
West Brom: Carson, Hoefkens, Pele, Donk, Robinson, Zuiverloon (Morrison 64), Borja Valero, Koren, Brunt, Simpson (Bednar 64), Fortune (Cech 46).
Akiba hawakucheza: Kiely, Kim, Dorrans, Filipe Teixeira.
Kadi Nyekundu: Robinson (40).
Kadi Njano: Koren, Bednar, Carson, Donk, Morrison.
Man Utd: Van der Sar, Neville (Eckersley 71), Ferdinand (Brown 70), Vidic, O'Shea, Park, Carrick, Giggs, Ronaldo, Berbatov (Tosic 77), Tevez.
Akiba hawakucheza: Kuszczak, Scholes, Fletcher, Gibson.
Kadi Njano: Park, Carrick.
Magoli: Berbatov 22, Tevez 44, Vidic 60, Ronaldo 65, 73.
Watazamaji: 26,105
Refa: Rob Styles

MATOKEO MECHI NYINGI ZA LEO ZALIGI KUU ENGLAND:
Portsmouth 0-1 Aston Villa

Sunderland 1-0 Fulham

Tottenham 3-1 Stoke

MECHI ZA Jumatano, 28 Januari 2009

[saa 4 dak 45 usiku]
Chelsea v Middlesbrough
Man City v Newcastle
Wigan v Liverpool

[saa 5 usiku]
Blackburn v Bolton
Everton v Arsenal
West Ham v Hull

Meneja wa Newcastle apigwa faini na FA kwa kumwita Refa Katuni 'Mickey Mouse!!!'

Joe Kinnear, Meneja wa Newcastle, amepigwa faini ya Pauni 500 baada ya kumwita Refa Martin Atkinson Katuni 'Mickey Mouse' aliechezesha mechi Newcastle waliyofungwa 2-1 na Fulham Novemba 9 mwaka jana.
Kinnear alikasirishwa na Refa huyo kwa kukataa kuwapa frikiki na badala yake akaruhusu mpira uendelee na hapo hapo akawapa Fulham penalti waliyofunga bao la pili na la ushindi.
Kinnear hakuadhibiwa katika kesi yake ya pili iliokuwa ikimkabili ya kumkashifu Mwamuzi katika mechi waliyocheza na Stoke City baada ya kuonekana hana hatia.
Sasa Kinnear bado ana kesi moja hapo FA pamoja na Meneja wa Hull City Phil Brown ambayo wote wawili walitolewa nje na kuamriwa kukaa kwa Watazamaji na Refa baada ya kuonekana wanazozana vikali pembeni ya uwanja huku mechi inaendelea wakati timu zao Newcastle na Hull City zilipokutana Januari 14.

Staa wa Chelsea John Mikel Obi abambwa na Polisi akiendesha gari huku akiwa njwiiiiii!!!

Mikel Obi alikamatwa na Polisi alfajiri ya Jumamosi iliyokwisha akiendesha gari mjini London huku akiwa amelewa chakari.
Mchezaji huyo atafikishwa Mahakamani tarehe 3 Aprili kujibu shtaka hilo.


Brazil yamwita tena Ronaldinho kundini!!!!

Kocha wa Brazil, Dunga, amemwita tena Ronaldinho kwenye Timu ya Taifa ya Brazil itakayocheza mechi ya kirafiki na Italia mwezi ujao mjini London Uwanja wa Emirates Februari 10.
Ronaldinho hajaitwa Timu ya Brazil tangu mwaka jana na alicheza mechi yake ya mwisho mwezi Septemba Brazil walipotoka 0-0 na Bolivia kwenye mechi ya Mtoano wa Kombe la Dunia.

Mechi zilizofuata za Brazil dhidi ya Venezuela na Colombia za Kombe la Dunia, Ronaldinho aliachwa pamoja na mechi ya kirafiki na Portugal iliyochezwa Novemba mwaka jana.
Brazil na Italia walicheza mara ya mwisho mwaka 1997 na kutoka sare 3-3 huko Ufaransa.

Kabla ya hapo walikutana kwenye Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1994 mechi iliyoisha 0-0 na Brazil wakashinda kwa penalti na kuwa Mabingwa wa Dunia.
Kikosi kamili [klabu wanazochezea kwenye mabano]:
Makipa: Doni (AS Roma), Julio Cesar (Inter Milan)
Walinzi: Daniel Alves (Barcelona), Adriano Correia (Sevilla), Maicon (Inter Milan), Marcelo (Real Madrid), Lucio (Bayern Munich), Luis¿o (Benfica), Juan (AS Roma), Thiago Silva (AC Milan)
Viungo: Anderson (Manchester United), Gilberto Silva (Panathinaikos), Felipe Melo (Fiorentina), Josue (VfL Wolfsburg), Elano (Manchester City), Julio Baptista (AS Roma), Kaka (AC Milan), Ronaldinho (AC Milan)
Washambuliaji: Alexandre Pato (AC Milan), Adriano (Inter Milan), Lus Fabiano (Sevilla), Robinho

No comments:

Powered By Blogger