Sunday 1 March 2009

Manchester United washinda Carling Cup!!

Dakika 120 hazikutoa hata bao na ikaja tombola ya penalti ndipo Mabingwa wa England, Ulaya na Dunia, Manchester United, wakafunga penalti 4 huku wapinzani wao wakifunga moja tu na kukosa 2.
Wafungaji wa Man U walikuwa Giggs, Tevez, Ronaldo na Anderson.
Wapigaji wa Tottenham walikuwa Jamie O'Hara ambae penalti yake iliokolewa na Kipa wa Man U Ben Foster, Vedran Corluka alifunga na David Bentley akatoa nje.
Tottenham ndio walikuwa Mabingwa Watetezi wa Kombe hili.
Tangu msimu huu uanze Agosti mwaka jana Man U washatwaa Ngao Ya Hisani na Kombe la Klabu Bingwa Duniani. Na bado wapo kwenye vinyang'anyiro vya Kombe la FA na Klabu Bingwa Ulaya huku wakiwa wanaongoza LIGI KUU England.

Vikosi vilikuwa:
Man U: Foster, O'Shea [Vidic dak 76], Evans, Ferdinand, Evra, Ronaldo, Scholes, Gibson [Giggs 91], Nani, Tevez, Welbeck [Anderson 56]
Tottenham: Gomes, Corluka, Dawson, King, Assou-Ekotto, Lennon [Bentley 102], Jenas [Bale 98], Zokora, Modric, Bent, Pavlyuchenko [O'Hara 65]
Refa: Chris Foy

No comments:

Powered By Blogger