Saturday 13 December 2008

MCHEZAJI BORA DUNIANI KUJULIKANI JANUARI 12: Listi yapunguzwa hadi Wagombea Watano!!!

Winga wa Manchester United, Cristiano Ronaldo na Straika wa Liverpool, Fernando Torres, wamo katika listi ya mwisho ya Wachezaji watano wanaogombea Tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia inayotolewa na FIFA.
Uteuzi huo wa Wachezaji hao watano umefanywa na Makocha na Manahodha wa Timu za Taifa za Nchi kutoka duniani kote.
Wachezaji wengine watatu ni Kaka wa AC Milan, nyota wa Barcelona Lionel Messi na Xavi wa Barcelona.
Ronaldo, ambae alipata Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ulaya [Ballon D'Or] siku ya Jumapili, alimaliza nafasi ya 3 kwenye Tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia wa FIFA mwaka uliopita nyuma ya Messi na Mshindi Kaka.
Mshindi atakabidhiwa Tuzo yake huko Zurich, Uswisi kwenye Jumba la Opera la Zurich Januari 12, 2009.
Kwa upande wa wanawake mshindi atakuwa kati ya Nadine Angerer, Cristiane, Marta, Birgit Prinz au Kelly Smith.
Kwa kina mama, Marta wa Brazil [pichani] ndie Mshindi mwaka uliopita na anapewa nafasi kubwa kushinda tena.
Mabingwa wa Afrika Al Ahly yatolewa nje KLABU BINGWA DUNIANI!
Wabandikwa 4-2 na Pachuca!!!

Leo Jumamosi tarehe 13 Desemba 2008, Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri, waliingia dimbani National Stadium, Tokyo, Japan kucheza na Pachuca ya Mexico ambao ni Mabingwa wa CONCACAF [Nchi za Marekani ya Kati, Kaskazini na Carribean].
Al Ahly walikuwa wakiongoza mabao 2-0 huku la kwanza Pachuca wakijifunga wenyewe kupitia Fausto Pinto na la pili akafunga Mshambuliaji wa Al Ahly kutoka Angola Amado Flavio.
Pachuca wakasawazisha kupitia Luis Montez na Christian Gimenez dakika ya 47 na 73.
Mpaka dakika 90 kumalizika mabao yalibaki 2-2 na dakika 30 za nyongeza zikachezwa.
Pachuca wakatoka kifua mbele kwa mabao ya Damian Alavarez dakika ya 98 na Gimenez akaongeza la 4 dakika ya 110.
Pachuca sasa watapambana na Liga de Quito ya Ecuador, Mabingwa wa Nchi za Marekani ya Kusini kwenye Nusu Fainali ya kwanza itakayochezwa Jumatano tarehe 17 Desemba 2008 .
Kesho ni mechi kati ya Mabingwa wa Asia, Gamba Osaka ya Japan na Adelaide United ya Australia ambao ni Washindi wa pili wa Klabu Bingwa Asia.
Mshindi wa mechi hii atapambana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United siku ya Alhamisi Desemba 18 katika Nusu ya pili.
Ronaldo ajiunga na Corinthians

Aliekuwa nyota wa Brazil Ronaldo de Lima ambae aliumia vibaya goti lililomlazimu kuiacha klabu ya Italia AC Milan mwezi Juni ametangazwa kujiunga na klabu ya Sao Paulo, Brazil iitwayo Corinthians.
Ronaldo aliumia goti hilo mwezi Februari na mkataba wake na AC Milan uliisha Juni.


Kipa Van der Sar aongeza mkataba

Golikipa wa Mabingwa Manchester United, Edwin van der Sar [38], ameongeza mwaka mmoja katika mkataba wake na sasa atabaki klabuni hapo hadi mwaka 2010.
Van der Sar alijiunga Man U Juni 2005 akitokea klabu ya Fulham. Awali alichezea klabu za Ajax na Juventus.


Barcelona v Real Madrid leo Nou Camp!

Timu inayosuasua kwenye Ligi ya Spain, La Liga, na ambayo siku ya Jumannne ilimtimua Meneja wake Bernd Schuster na kumchukua Juande Ramos ambae nae alietimuliwa Tottenham, Real Madrid, leo inaingia myumbani kwa mahasimu wao na vinara wa ligi, Barcelona, uwanjani Nou Camp.
Mpaka sasa Real Madrid wako nafasi ya 5 wakiwa pointi 9 nyuma ya viongozi wa La Liga Barcelona.
Juande Ramos amepewa mkataba wa miezi 6 tu kuwa Meneja wa Real Madrid na kumfanya awe Meneja wa 8 wa klabu hiyo katika miaka 6 iliyopita.

Mechi ya leo itachezwa saa 6 usiku saa za bongo.

Thursday 11 December 2008

Baada ya Miaka 40 Tuzo ya 'BALLON d'OR' yarudi OLD TRAFFORD!!!

Kabla ya kuanza mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE iliyochezwa Jumatano kati ya Manchester United na Aalborg uwanjani Old Trafford, Cristiano Ronaldo alietunukiwa 'Ballon d'Or' [KOMBE LA DHAHABU] kudhihirisha yeye ndie MCHEZAJI BORA ULAYA mwaka huu, alitambulishwa rasmi na kukabidhiwa tena Kombe hilo uwanjani hapo huku akiwa amesindikizwa na Wachezaji wa zamani wa Manchester United Dennis Law, alieshinda tuzo hiyo mwaka 1964 na Sir Bobby Charlton alieipata 1966.
Mchezaji wa mwisho wa Manchester United kushinda Tuzo hiyo ni George Best alietunukiwa mwaka 1968.
George Best ni marehemu.

LIGI KUU UINGEREZA: Kitimtim cha Wikiendi

Jumamosi, 13 Decemba 2008

[saa 8 dak 45]
Middlesbrough v Arsenal

[saa 12 jioni]
Aston Villa v Bolton

Liverpool v Hull

Man City v Everton

Stoke v Fulham

Sunderland v West Brom

Wigan v Blackburn

[saa 2 na nusu]
Tottenham v Man U

Jumapili, 14 Decemba 2008
[saa 10 na nusu jioni]
Portsmouth v Newcastle

[saa 1 usiku]
Chelsea v West Ham
FIFA CLUB WORLD CUP JAPAN 2008 yaanza!!!

Mabingwa wa Afrika Al Ahly kucheza Jumamosi, Man United dimbani wiki ijayo!!!!!

Leo mashindano ya kugombea 'KOMBE LA KLABU BINGWA YA DUNIA' yajulikanayo kama 'FIFA CLUB WORLD CUP JAPAN 2008' yameanza rasmi huko Tokyo, Japan kwa mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa kati ya Adelaide United, Washindi wa Pili wa Klabu Bingwa Asia wanaotoka Australia, na Waitakere United ya New Zealand, ambayo inawakilisha Timu kutoka Nchi za Oceania.
Katika mechi hiyo ya ufunguzi, Adelaide United ilibwaga Waitakere United kwa mabao 2-1 wafungaji wakiwa ni Daniel Mullen na Travis Dodd kwa Adelaide kwenye dakika ya 38 na 83.
Paul Seaman aliifungia Waitakere dakika ya 34.
Sasa Adelaide United wanasonga mbele na watakutana na Gamba Osaka ya Japan ambao ndio Mabingwa wa Bara la Asia mchezo ambao utachezwa Toyota Stadium, mjini Tokyo, Japan siku ya Jumapili tarehe 14 Desemba 2008.
Kesho ni mapumziko na siku ya Jumamosi tarehe 13 Desemba 2008, Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri, inashuka dimbani National Stadium, Tokyo, Japan kucheza na Pachuca ya Mexico ambao ni Mabingwa wa CONCACAF [Nchi za Marekani ya Kati, Kaskazini na Carribean].
Mshindi wa mechi hii atapambana na Liga de Quito ya Ecuador, Mabingwa wa Nchi za Marekani ya Kusini kwenye Nusu Fainali ya kwanza.
Mabingwa wa Ulaya, Manchester United, wao wameingizwa moja kwa moja Nusu Fainali ya pili na watapambana na mshindi wa mechi kati Adelaide United na Gamba Osaka hapo Alhamisi tarehe 18 Desemba 2008 mjini Yokohama, Japan.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: DRO YA RAUNDI YA MTOANO KUFANYIKA DESEMBA 19: Vigogo Man U, Chelsea, Arsenal na Liverpool kukutana na nani?

Wakati tayari Timu 16 zilizoingia Raundi ya Mtoano ambayo huchezwa kwa mtindo wa mechi za nyumbani na ugenini ili kupata Timu 8 zitakazoingia Robo Fainali zimeshapatikana, Dro ya kuamua nani anacheza na nani itafanyika tarehe 19 Desemba 2009.
Timu 16 zilizoingia kwenye Dro hiyo ni:
WALIOSHINDA KILA KUNDI: Roma, Panathinaikos, Barcelona, Liverpool, Man U, Bayern Munich, FC Porto, Juventus.
WASHINDI WA PILI: Chelsea, Inter Milan, Sporting, Atletico Madrid, Villareal, Lyon, Arsenal, Real Madrid.
KANUNI ZINAZOTAWALA DRO:
-Timu toka Nchi moja haziwezi kukutana.
-Mshindi wa Kundi na Mshindi wa Pili wa Kundi hilohilo hawawezi kukutana.
-Washindi wa Makundi hawawezi kukutanishwa.
-Washindi wa Pili wa Makundi hawawezi kukutanishwa.
-Washindi wa Pili wa kila Kundi watacheza mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano nyumbani kwao.

Kufuatana na Kanuni hizi, Timu za England, Man U, Chelsea, Arsenal na Liverpool, haziwezi kukutana zenyewe.

Hivyo basi, tumechambua ni Timu zipi ambazo Vigogo hao wa England wanaweza kupambanishwa nao:

MANCHESTER UNITED: Inter Milan, Sporting Lisbon, Atletico Madrid, Lyon, Real Madrid.

ARSENAL: Bayern Munich, Juventus, AS Roma, Panathinaikos, Barcelona.

CHELSEA: Panathinaikos, Barcelona, Bayern Munich, FC Porto, Juventus.

LIVERPOOL: Inter Milan, Sporting Lisbon, Villareal, Lyon, Real Madrid.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Arsenal apigwa, Man U sare!!!

Timu zote 16 zitakazocheza Raundi ya Mtoano zilikuwa zishajulikana na mechi za Jumatano zilikuwa ni kuamua msimamo wa kila Kundi.

Baada ya mechi hizo hali ni kama ifuatavywo:

KUNDI E
Celtic 2 v Villarreal 0,
Man U 2 v AaB 2,

Msimamo:
1 Man U 10 pts
2 Villareal 9 pts
3 Aab Aalborg 6 pts
4 Celtic 5 pts

KUNDI F
Steaua Bucharest 0 v Fiorentina 1,
Lyon 2 v Bayern Munich 3,
Msimamo:

1 Bayern Munich 14 pts
2 Lyon 11 pts
3 Fiorentina 6 pts
4 Steau Bucharest 1 pts

KUNDI G
Dynamo Kiev 1 v Fenerbahce 0,
FC Porto 2 v Arsenal 0,

Msimamo:
1 FC Porto 12 pts
2 Arsenal 11 pts
3 Dynamo Kiev 8 pts
4 Fenerbahce 2 pts

KUNDI H
Juventus 0 v BATE 0
Real Madrid 3 v Zenit St Petersburg 0

Msimamo:
1 Juventus 12 pts
2 Real Madrid 12 pts
3 Zenit St Petersburg 5 pts
4 BATE Borisov 3 pts

MECHI ZA JUMANNE:
WALIOSHINDA KILA KUNDI: Roma, Panathinaikos, Barcelona, Liverpool.
WASHINDI WA PILI: Chelsea, Inter Milan, Sporting, Atletico Madrid.
MECHI ZA JUMATANO:
WALIOSHINDA KILA KUNDI: Man U, Bayern Munich, FC Porto, Juventus
WASHINDI WA PILI: Villareal, Lyon, Arsenal, Real Madrid

Wednesday 10 December 2008

UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
TIMU 16 ZINAZOINGIA RAUNDI YA MTOANO ZAPATIKANA!!

Mechi za jana za UEFA CHAMPIONS LEAGUE zimetoa Timu 3 zilizobaki ili kufanya idadi ya timu kuwa 16 zitakazocheza Raundi inayofuata ya Mtoano.
Dro ya kuamua timu ipi inakutana na ipi kwa mechi za nyumbani na ugenini ili kupata timu 8 zitakazoingia Robo Fainali itafanyika tarehe 19 Desemba 2008.
Mechi za Raundi hii ya Mtoano zitachezwa tarehe 24 na 25 Februari 2009 na marudiano ni tarehe 10 na 11 Machi 2009.
Katika Timu hizo 16 zilizofuzu 4 zinatoka England, nazo ni Manchester United, Chelsea, Liverpool na Arsenal na 4 nyingine zinatoka Spain ambazo ni Real Madrid, Barcelona, Villareal na Atletico Madrid.
Timu zilizobaki ni AS Roma, Inter Milan, Panathinaikos, Sporting Lisbon, Lyon, Bayern Munich, FC Porto na Juventus.
Katika hiyo Dro ya Raundi ya Mtoano Timu kutoka nchi moja na zile zilizokuwa Kundi moja haziruhusiwi kukutana.
Pia Timu iliyoongoza Kundi itapambanishwa na Timu iliyokuwa ya pili toka Kundi jingine.
Timu amabazo jana zilipata nafasi ya tatu katika msimamo wa Makundi na ambazo sasa zitaingizwa UEFA CUP ni: Bordeaux, Werder Bremen, Shakhtar Donetsk na Marseille.

MATOKEO MECHI ZA Jumanne, 9 Decemba 2008

KUNDI A
Chelsea 2 v CFR 1,
Roma 2 v Bordeaux 0,
Msimamo:
1 Roma 12 pts
2 Chelsea 11 pts
3 Bordeaux 7 pts
4 CFR Cluj 4 pts

KUNDI B
Werder Bremen 2 v Inter Milan 1,
Panathinaikos 1 v Anorthosis Famagusta 0,
Msimamo:
1 Panathinaikos 10 pts
2 Inter Milan 8 pts
3 Werder Bremen 7 pts
4 Anorthosis 6 pts

KUNDI C
Barcelona 2 v Shakhtar Donetsk 3,
Basle 0 v Sporting 1,
Msimamo:
1 Barcelona 13 pts
2 Sporting Lisbon 12 pts
3 Shakhtar Donetsk 9 pts
4 Basle 1 pt

KUNDI D
Marseille 0 v Atletico Madrid 0,
PSV 1 v Liverpool 3,
Msimamo:
1 Liverpool 14 pts
2 Atletico Madrid 12 pts
3 Marseille 4 pts
4 PSV 3 pts

MECHI ZA LEO: Jumatano, 10 Decemba 2008

Ingawa Timu zote 16 zitakazocheza Raundi ya Mtoano zimepatikana, umuhimu wa mechi za leo ni kuamua nani ataongoza kwenye Kundi na nani atacheza UEFA.

KUNDI E
Celtic v Villarreal,
Man U v AaB,

KUNDI F
Steaua Bucuresti v Fiorentina
Lyon v Bayern Munich

KUNDI G
Dynamo Kiev v Fenerbahce,
FC Porto vArsenal,

KUNDI H
Juventus v BATE
Real Madrid v Zenit St Petersburg

Monday 8 December 2008

STRAIKA EDUARDO KARIBUNI KUSHUKA DIMBANI!!

Mshambuliaji wa Arsenal Eduardo ambae aliumizwa vibaya mwezi Februari mwaka huu huko Birmingham wakati Arsenal wakicheza mechi ya LIGI KUU na Birmingham City yupo karibu kuonekana tena uwanjani.
Eduardo [25] alivunjwa enka na Mchezaji wa Birmingham City Martin Taylor [tizama picha] na tangu wakati huo alikuwa akijiuguza lakini kwa sasa yupo mazoezini na hucheza hata mechi kamili za mazoezi.
Meneja Arsene Wenger wa Arsenal amethibitisha: 'Ndio yupo mazoezini na atacheza hivi karibuni.'
Eduardo ni mzawa wa Brazil ingawa anaichezea Croatia.

Wenger amtetea Mchezaji wake Eboue aliekasirishwa kubadilishwa kwenye mechi.

Kwenye mechi ya Jumamosi iliyopita ya LIGI KUU ambayo Arsenal wakiwa kwao Emirates Stadium waliifunga Wigan bao 1-0 kwa bao la Adebayor, Eboue alianza mechi hii akiwa benchi la akiba kama resevu.
Eboue alipata nafasi ya kuingizwa kucheza dakika ya 32 baada ya Samir Nasri kuumia.
Lakini, hiyo itakuwa ni mechi ambayo hatopenda kuikumbuka kwani mara baada ya kuingizwa akawa akicheza kosa baada ya kosa mojawapo likiwa kumnyang'anya mpira mwenzake Kolo Toure na kumpasia adui!
Washabiki wa Arsenal wakaanza kumzomea!
Alipozidi kuzodolewa na kuendelea kufanya makosa huku timu yake Arsenal ikiwa imebanwa sana na Wigan ambao walionekana wanaweza kurudisha, Meneja Arsene Wenger akalazimika kumbadilisha na kumwingiza Mlinzi Mikael Silvestre.
Wakati Eboue akitoka uwanjani, Washabiki wa Arsenal walimshangilia kwa kejeli kubwa na yeye akakasirika na akasusa kwenda benchi la akiba na badala yake akaingia moja kwa kwa moja vyumba vya kubadilishia jezi Wachezaji.
'Ulikuwa uamuzi mgumu lakini alishapoteza morali na imani yake' Wenger alisema. 'Alikuwa hawezi tena kumiliki mpira na ilikuwa hatari kwetu! Mashabiki wetu wamenisikitisha sana! Atarudi tu ni mchezaji mzuri na mashabiki haohao watamshangilia!'

DWIGHT YORKE ALIA KUONDOKA ROY KEANE SUNDERLAND!!!

Dwight Yorke[37] amekaririwa akinung'unika kuhusu kung'oka kwa aliekuwa Mchezaji mwenzake huko Manchester United, Roy Keane, kama Meneja wake wa Sunderland: 'Nilishtuka, nilishangaa na nimesikitishwa!'
Yorke aliongeza: 'Yeye ndie alienileta Sunderland! Namshkuru sana! Naamini sana angeendelea hapa lazima timu ingefanya vizuri tu!'
Roy Keane alimleta Dwight Yorke kuichezea Sunderland mwaka 2006 wakati timu ikiwa Daraja la Chini ya LIGI KUU na wote wakaipandisha LIGI KUU msimu huo huo.
LEO LIGI KUU: West Ham v Tottenham

West Ham wakiwa nyumbani uwanjani Upton Park leo wanawakaribisha wenzao wa jijini London Tottenham kwenye mechi pekee ya LIGI KUU itakayochezwa saa 5 usiku saa za kibongo.
Timu zote mbili zikiwa zimecheza idadi sawa ya mechi 15 kila mmoja, West Ham yuko juu ya Tottenham kwa pointi 3. West Ham yuko nafasi ya 15 akiwa na pointi 18 na Tottenham yuko wa 17 akiwa na pointi 17.
Meneja wa West Ham Gianfranco Zola amesisitiza umuhimu wa mechi hii wakati yule wa Tottenham Harry Redknapp amekiri Upton Park ni mahali pagumu sana kupata ushindi.
VIKOSI VITATATOKANA NA:
West Ham: Green, Neill, Collins, Upson, Ilunga, Faubert, Boa Morte, Parker, Mullins, Behrami, Bellamy, Cole, Noble, Lastuvka, Tristan, Davenport, Collison, Di Michele, Bowyer.
Tottenham: Gomes, Cesar, Alnwick, Bale, Gunter, Dawson, Assou-Ekotto, Woodgate, King, Corluka, Zokora, Bentley, Huddlestone, Jenas, O'Hara, Bostock, Lennon, Jenas, Boateng, Bent, Campbell, Pavlyuchenko, Modric.
REFA: CHRIS FOY
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Mechi za mwisho za MAKUNDI!!!

Jumanne tarehe 9 Desemba 2008 na Jumatano mechi za mwisho za Makundi ya kugombea Klabu Bingwa Ulaya 2008/9, yaani UEFA CHAMPIONS LEAGUE, zitamalizika.
Awamu hii iligawiwa kwenye Makundi manane yenye timu 4 kila moja huku mbili za juu zikisonga mbele kuingia Raundi inayofuata ya Mtoano itakayokuwa na jumla ya timu 16.
Timu zitakazokuwa nafasi ya 3 toka kila Kundi zitaingizwa kwenye Kapu la Dro yenye Timu 32 kugombea Kombe la UEFA.
Mpaka sasa Timu 13 kati ya 16 tayari zimeshafuzu kuingia Raundi hiyo ya Mtoano.
Timu hizo 13 ni pamoja na Mabingwa Watetezi wa Kombe hili Manchester United, Liverpool, Inter Milan, Atletico Madrid, Villareal , Barcelona, Sporting Lisbon, Lyon, Bayern Munich, Arsenal, FC Porto, Juventus na Real Madrid.
Timu 3 zilizobaki zitakazokamilisha idadi ya Timu 16 moja itatoka Kundi B, ambako tayari Inter Milan kashafuzu, hivyo nafasi hiyo moja itaamuliwa kwenye mechi ya mwisho ya Jumanne kati ya Panathinaikos na Anorthosis Famagusta na mshindi ndie ataendelea.
Nafasi mbili za mwisho kukamilisha jumla ya Timu 16 ni za Timu za Kundi A ambamo kukiwa kumesalia mechi moja kwa kila Timu, AS Roma, anaongoza Kundi hili akiwa na pointi 9, Chelsea, ni wa pili akiwa na pointi 8 na Bordeaux wa tatu akiwa na pointi 7 huku CFR Cluj wa mwisho akiwa na pointi 4.Katika mechi za mwisho, AS Roma anamkaribisha Bordeaux na Chelsea atakuwa nyumbani Stamford Bridge kupambana na CFR Cluj. Timu mbili za juu toka Kundi hili zitaendelea.
Vilevile, mechi hizi za mwisho kwa baadhi ya Makundi zitaamua nani atashika nafasi ya uongozi na nani wa pili kitu ambacho ni muhimu sana kwenye upigaji kura timu zipi zinakutana kwenye Raundi hiyo ya Mtoano yenye jumla ya timu 16 zitakazopangwa kucheza nyumbani na ugenini kuanzia tarehe 24 na 25 Februari 2009.
Umuhimu huo unakuja kutokana na Timu iliyoshika uongozi kupangiwa kukutana na mshindi wa pili toka kundi jingine na kwamba timu zilizokuwa Kundi moja kwenye awamu ya Makundi na zile zinazotoka Nchi moja haziwezi kupangwa kukutana kwenye Raundi hiyo ya Mtoano.
Hivyo, kwenye Raundi ijayo, Man U, Arsenal, Liverpool na Chelsea haziwezi kukutana kwani zote zinatoka England.
Dro ya kuamua nani wanakutana kwenye Mtoano itafanyika tarehe 19 Desemba 2008.
KUNDI A
Kundi hili ndilo lenye kasheshe kubwa.
Mahesabu yake ni kwamba ni CFR Cluj pekee ndio imeshatolewa nje na ina uhakika wa kumaliza nafasi ya mwisho. Chelsea wanawakaribisha CFR Cluj hapo Jumanne.
Chelsea wanahitaji ushindi ili wasonge mbele ingawa wanaweza kusonga mbele hata wakifungwa endapo tu Bordeaux hawatowafunga AS Roma timu inayoongoza Kundi hili kwenye mechi itakayochezwa Rome, Italia.
Nao AS Roma wanaweza kusonga mbele hata kama wakifungwa ikiwa Chelsea atafungwa.
Bordeau hana ujanja. Lazima amfunge AS Roma ili asonge mbele.
KUNDI B
Inter Milan, ambao washafuzu, watashika uongozi Kundi hili wakiifunga Werder Bremen walio nafasi ya mwisho na ambao wanahitaji ushindi angalau wamalize wa tatu na kucheza Kombe la UEFA. Na hata huo ushindi unaweza usitosheleze kwa Werder Bremen kwani ikiwa Anorthosis Famagusta ya Cyprus ikiifunga Panathinaikos ya Ugiriki hukohuko Ugiriki basi Anorthosis Famagusta watasonga mbele na Panathinaikos watacheza UEFA.
Lakini droo kwa Panathinaikos ni vilevile nzuri kuwafanya wasonge mbele ingawa ushindi unaweza kuwapa nafasi ya kuongoza Kundi.
KUNDI C
Kila kitu kimekamilika toka Kundi hili huku Barcelona wako wa kwanza na Sporting Lisbon wako wa pili na ndio timu zinazosonga mbele.
Timu toka Ukraine Shakhtar Donetsk iko ya 3 na itacheza UEFA.
FC Basel ya Uswisi wako mkiani na nje ya mashindano na wanacheza mechi ya mwisho na Sporting Lisbon kukamilisha ratiba tu.
KUNDI D
Atletico Madrid na Liverpool wameshafuzu lakini nani ndie wa kwanza ndio kitaamuliwa kwenye mechi zao za Jumanne. Timu zote hizi zina pointi 11 lakini Atletico Madrid wanaongoza kwa tofauti ya magoli.
Atletico Madrid atacheza ugenini na Olympique de Marseille ambao wanahitaji ushindi ili wacheze UEFA.
Liverpool watakuwa wageni wa PSV Eindhoven ambao nao wanahitaji ushindi wa nguvu ili kuwapiku Marseille kucheza UEFA.
KUNDI E
Mabingwa Watetezi wa Kombe hili Manchester United wanaoongoza ingawa wako pointi sawa na Villareal, wote wakiwa wameshapita, wanawakaribisha Aaalborg ya Demark ambao nao washaingia UEFA CUP.
Man U wanajua wazi wakishinda mechi hii basi watashika uongozi Kundi hili labda Villareal aifunge Celtic magoli mawili zaidi ya yale Man U watawafunga Aalborg.
Celtic ya Scotland, timu iliyotupwa nje, itaikaribisha Villareal.
KUNDI F
Lyon wanawakaribisha Bayern Munich katika mechi itakayoamua nani anachukua hatamu za Kundi hili kwani timu zote zimeshafuzu.
Ushindi kwa Lyon au suluhu ya bila magoli itawapa uongozi Lyon.
Ili wacheze UEFA, wenyeji Steau Bucharest lazima wawafunge Fiorentina na matokeo mengine yeyote Fiorentina ataonja UEFA.
KUNDI G
Arsenal wanasafiri hadi Ureno kupambana na FC Porto na ingawa timu zote zimefuzu ni pambano ambalo litaamua nani ataongoza Kundi hili huku Arsenal anahitaji suluhu tu ili aongoze.
Nao Fenerbahce watasafiri hadi nyumbani kwa Dynamo Kiev na inabidi washinde ili wacheze UEFA.
KUNDI H
Juventus wanaongoza Kundi hili na wakicheza nyumbani wanahitaji sare tu katika mechi na timu iliyotupwa nje ya FC Bate.
Real Madrid, nao washafuzu ingawa wakishinda na Juventus akifungwa basi wao watashika hatamu.
Real anacheza na timu ya FC Zenit St Petersburg ambao sasa watacheza UEFA baada ya kukosa nafasi kusonga mbele na hii ni nafasi nzuri kwao kutetea Taji lao la UEFA kwani wao ndio Mabingwa wa UEFA CUP msimu uliopita.
RATIBA KAMILI NI:
Jumanne, 9 Decemba 2008
KUNDI A
Chelsea v CFR
Roma v Bordeaux,
KUNDI B
Werder Bremen v Inter Milan,
Panathinaikos v Anorthosis Famagusta,
KUNDI C
Barcelona v Shakhtar Donetsk,
Basle v Sporting,
KUNDI D
Marseille v Atletico Madrid,
PSV vLiverpool,
Jumatano, 10 Decemba 2008
KUNDI E
Celtic v Villarreal,
Man U v AaB,
KUNDI F
Steaua Bucuresti v Fiorentina
Lyon v Bayern Munich
KUNDI G
Dynamo Kiev v Fenerbahce,
FC Porto vArsenal,
KUNDI H
Juventus v BATE
Real Madrid v Zenit St Petersburg

Sunday 7 December 2008

RONALDO AKABIDHIWA TUZO YA 'Ballon d'Or'

Leo, mjini Paris, Ufaransa, nyota wa Mabingwa wa Uingereza na Ulaya, Manchester United, Cristiano Ronaldo, amekabidhiwa Tuzo inayotukuka ya Ballon d'Or, yaani 'MPIRA WA DHAHABU' inayoashiria yeye kwa sasa ndie MCHEZAJI BORA ULAYA.
Ronaldo, ambae vilevile ndie anaetegemewa sana kushinda Tuzo ya MCHEZAJI BORA WA DUNIA inayotolewa na FIFA, ameshashinda Tuzo ya MCHEZAJI BORA WA DUNIA YA FIFPRO ambayo hutolewa na Wachezaji wa Kulipwa.
Akipokea Tuzo hiyo, huku Mama yake Mzazi aitwae Maria na Meneja wa Klabu yake Sir Alex Ferguson wakiwepo [tizama picha] kwenye ghafla iliyorushwa moja kwa moja kwenye televisheni, Ronaldo alitoa shukrani zake za dhati.
Sir Alex Ferguson alitoa nasaha zake kwenye ghafla hiyo kwa kusema: 'Cristiano, tunasikia fahari sana, wewe ni mfano bora kwa vijana wote duniani wanaokuja Manchester kutoka nje! Sasa endelea mazoezi ili ushinde, endeleza kipaji chako! Hongera! Endelea hivihivi!'
Nao Mameneja wa Chelsea, Felipe Scolari na wa Arsenal, Arsene Wenger, nao walipewa ruhusa ya kuongea kwa njia ya video.
Luis Felipe Scolari aliewahi kuwa Kocha wa Ronaldo kwenye Timu ya Taifa ya Ureno alisema: 'Hii ni tuzo yako ya kwanza kwa yote uliyofanya lakini sio ya mwisho. Hii itakuwa moja ya nyingi utakazopata kwenye historia yako.'
Arsene Wenger alisema wakati Ronaldo amesimama bega kwa bega na Ferguson kwenye ghafla hiyo: 'Una kipaji kikubwa sana! Nawapongeza nyote wawili kwani hii ni kazi ya pamoja.'

West Brom 1 Portsmouth 1

West Brom imefanikiwa kupata pointi moja baada ya kutoka suluhu leo na Portsmouth lakini bado ndio timu ya mwisho kwenye msimamo wa LIGI KUU ikiwa nafasi ya 20 na pointi 12 kwa mechi 16.
Nafasi ya 19 inashikwa na Blackburn ikiwa nayo imecheza mechi 16 na ina pointi 13.
Sunderland ni ya 18 kwa mechi 16 na pointi 15.
West Bromwich ilikuwa wa kwanza kupata bao wakati Nahodha wao Jonathan Greening alipofunga dakika ya 39 lakini Peter Crouch wa Portsmouth alisawazisha dakika ya 58 kwa shuti kali la mita kama 20 hivi.
Kimsimamo, Portsmouth wako nafasi ya 7 wamecheza mechi 16 na wana pointi 23.
Everton 2 Aston Villa 3
Ni mechi iliyoanza kwa bao la kwanza kupatikana sekunde 34 tu tangu mechi ianze!
Steve Sidwell, akipokea pasi kutoka kwa James Milner, alifumua mkwaju na kuipatia Aston Villa bao la kuongoza.
Dakika ya 30, wenyeji Everton wakasawazisha kupitia Beki wao John Lescott kufuatia fikikiki ya Arteta.
Kipindi cha pili dakika ya 54 Beki wa kutumainiwa wa Everton Phil Jagielka akiwa mtu wa mwisho kwenye safu ya ulinzi aligeuka na kurudisha mpira nyuma kwa Kipa wake Tim Howard bila ya kutazama kumbe alikuwa akitoa pasi murua kwa adui Winga Ashley Young ambae akaipa kilaini Aston Villa bao la pili.
Zikiwa dakika 90 zimekwisha na mechi iko kwenye dakika 3 za nyongeza, John Lescott tena akaisawazishia Everton baada ya krosi ya Jagielka kumkuta Cahill aliempasia mfungaji Lescott aliefunga goli zuri sana dakika ikiwa ya 92.
Dakika ya 93, Ashley Young akaipa bao la ushindi Aston Villa baada ya defensi ya Everton kujikoroga yenyewe.
Mabingwa Man U washinda kwa mbinde: Beki Vidic apachika bao la ushindi dakika za majeruhi!!!

Goli lililofungwa na Nemanja Vidic, Beki pacha na Rio Ferdinand, kwenye dakika ya 90 ya mchezo, liliwapa ushindi wa bao 1-0 Mabingwa Man U wakiwa nyumbani Old Trafford wakicheza na Sunderland timu ambayo haina Meneja baada ya Roy Keane kuitema na ambayo kwa sasa iko nafasi za mwisho kabisa kwenye msimamo wa LIGI KUU.
Nae Meneja wa Man U, Sir Alex Ferguson, alishuhudia mechi hii akiwa amekaa jukwaani [pichani akiwa amekaa nyuma ya Mkurugenzi na Mchezaji wa zamani wa Man U Sir Bobby Charlton] kwa Watizamaji ikiwa ni kutumikia adhabu ya kufungiwa mechi 2 na hivyo kutoruhusiwa kukaa benchi la timu yake baada ya kufarakana na Refa Mike Dean wakati Man U ilipocheza na Stoke.
Hii ilikuwa mechi yake ya pili ya kifungo.
Wimbi baada ya wimbi la mashambulizi kwa dakika zote za mchezo hazikuzaa goli kwani Wachezaji karibu wote wa Sunderland walijikita mbele ya penalti boksi yao kujihami.
Wenyewe Wazungu wanaita 'Timu imepaki basi mbele ya mlango wao'.
Katika mechi nzima Man U walipiga jumla ya mashuti 23 golini na Sunderland hawakupiga hata moja.

Man U walipata kona 10 na Sunderland walipata 1 tu na ambayo ndiyo ilisababisha kifo chao.
Kona hiyo pekee waliyopata Sunderland dakika ya 89 ilizuiwa na ukuta wa Man U na huku Wachezaji wengi wa Sunderland wakiwa wamepanda golini kwa Man U ili kuongeza mashambulizi, Man U walifanya shambulizi la haraka na Kiungo Michael Carrick akiwa nje ya boksi alipiga shuti lilombabatiza Collin Edwards, kumpita Kipa, na kugonga posti chini na kurudi ndani na mpira kumkuta Beki Nemanja Vidic aliushindilia wavuni.
Man U walimiliki mpira kwa asilimia 78 na Sunderland asilimia 28 tu!

Wataalam wa LIGI KUU wameielezea mechi hii kuwa ni ya upande mmoja sana kiasi ambacho haijawahi kutokea ingawa cha kushangaza ni kukosekana lundo la magoli.
Katika mechi hii Mabingwa Man U walipata pigo pale Mchezaji wao Bora wa Ulaya Ronaldo alipoumia na ikabidi atoke nje ya uwanja kwenye dakika ya 68.
Ingawa Man U hawakupata ushindi wa kishindo lakini kupata pointi 3 kwao ni jambo bora kwani linawafanya bado wawe karibu sana na vinara wa ligi Liverpool na Chelsea.
Msimamo mpaka sasa ni:
Liverpool: mechi 16 pointi 37
Chelsea: mechi 16 pointi 36
Man U: mechi 15 pointi 31
Arsenal: mechi 16 pointi 29
MECHI ZA LEO:
Jumapili, 7 Decemba 2008
[saa 12 jioni] West Brom v Portsmouth
[saa 1 usiku]Everton v Aston Villa
Powered By Blogger