Monday 8 December 2008

STRAIKA EDUARDO KARIBUNI KUSHUKA DIMBANI!!

Mshambuliaji wa Arsenal Eduardo ambae aliumizwa vibaya mwezi Februari mwaka huu huko Birmingham wakati Arsenal wakicheza mechi ya LIGI KUU na Birmingham City yupo karibu kuonekana tena uwanjani.
Eduardo [25] alivunjwa enka na Mchezaji wa Birmingham City Martin Taylor [tizama picha] na tangu wakati huo alikuwa akijiuguza lakini kwa sasa yupo mazoezini na hucheza hata mechi kamili za mazoezi.
Meneja Arsene Wenger wa Arsenal amethibitisha: 'Ndio yupo mazoezini na atacheza hivi karibuni.'
Eduardo ni mzawa wa Brazil ingawa anaichezea Croatia.

Wenger amtetea Mchezaji wake Eboue aliekasirishwa kubadilishwa kwenye mechi.

Kwenye mechi ya Jumamosi iliyopita ya LIGI KUU ambayo Arsenal wakiwa kwao Emirates Stadium waliifunga Wigan bao 1-0 kwa bao la Adebayor, Eboue alianza mechi hii akiwa benchi la akiba kama resevu.
Eboue alipata nafasi ya kuingizwa kucheza dakika ya 32 baada ya Samir Nasri kuumia.
Lakini, hiyo itakuwa ni mechi ambayo hatopenda kuikumbuka kwani mara baada ya kuingizwa akawa akicheza kosa baada ya kosa mojawapo likiwa kumnyang'anya mpira mwenzake Kolo Toure na kumpasia adui!
Washabiki wa Arsenal wakaanza kumzomea!
Alipozidi kuzodolewa na kuendelea kufanya makosa huku timu yake Arsenal ikiwa imebanwa sana na Wigan ambao walionekana wanaweza kurudisha, Meneja Arsene Wenger akalazimika kumbadilisha na kumwingiza Mlinzi Mikael Silvestre.
Wakati Eboue akitoka uwanjani, Washabiki wa Arsenal walimshangilia kwa kejeli kubwa na yeye akakasirika na akasusa kwenda benchi la akiba na badala yake akaingia moja kwa kwa moja vyumba vya kubadilishia jezi Wachezaji.
'Ulikuwa uamuzi mgumu lakini alishapoteza morali na imani yake' Wenger alisema. 'Alikuwa hawezi tena kumiliki mpira na ilikuwa hatari kwetu! Mashabiki wetu wamenisikitisha sana! Atarudi tu ni mchezaji mzuri na mashabiki haohao watamshangilia!'

DWIGHT YORKE ALIA KUONDOKA ROY KEANE SUNDERLAND!!!

Dwight Yorke[37] amekaririwa akinung'unika kuhusu kung'oka kwa aliekuwa Mchezaji mwenzake huko Manchester United, Roy Keane, kama Meneja wake wa Sunderland: 'Nilishtuka, nilishangaa na nimesikitishwa!'
Yorke aliongeza: 'Yeye ndie alienileta Sunderland! Namshkuru sana! Naamini sana angeendelea hapa lazima timu ingefanya vizuri tu!'
Roy Keane alimleta Dwight Yorke kuichezea Sunderland mwaka 2006 wakati timu ikiwa Daraja la Chini ya LIGI KUU na wote wakaipandisha LIGI KUU msimu huo huo.

No comments:

Powered By Blogger