Thursday 11 December 2008

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: DRO YA RAUNDI YA MTOANO KUFANYIKA DESEMBA 19: Vigogo Man U, Chelsea, Arsenal na Liverpool kukutana na nani?

Wakati tayari Timu 16 zilizoingia Raundi ya Mtoano ambayo huchezwa kwa mtindo wa mechi za nyumbani na ugenini ili kupata Timu 8 zitakazoingia Robo Fainali zimeshapatikana, Dro ya kuamua nani anacheza na nani itafanyika tarehe 19 Desemba 2009.
Timu 16 zilizoingia kwenye Dro hiyo ni:
WALIOSHINDA KILA KUNDI: Roma, Panathinaikos, Barcelona, Liverpool, Man U, Bayern Munich, FC Porto, Juventus.
WASHINDI WA PILI: Chelsea, Inter Milan, Sporting, Atletico Madrid, Villareal, Lyon, Arsenal, Real Madrid.
KANUNI ZINAZOTAWALA DRO:
-Timu toka Nchi moja haziwezi kukutana.
-Mshindi wa Kundi na Mshindi wa Pili wa Kundi hilohilo hawawezi kukutana.
-Washindi wa Makundi hawawezi kukutanishwa.
-Washindi wa Pili wa Makundi hawawezi kukutanishwa.
-Washindi wa Pili wa kila Kundi watacheza mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano nyumbani kwao.

Kufuatana na Kanuni hizi, Timu za England, Man U, Chelsea, Arsenal na Liverpool, haziwezi kukutana zenyewe.

Hivyo basi, tumechambua ni Timu zipi ambazo Vigogo hao wa England wanaweza kupambanishwa nao:

MANCHESTER UNITED: Inter Milan, Sporting Lisbon, Atletico Madrid, Lyon, Real Madrid.

ARSENAL: Bayern Munich, Juventus, AS Roma, Panathinaikos, Barcelona.

CHELSEA: Panathinaikos, Barcelona, Bayern Munich, FC Porto, Juventus.

LIVERPOOL: Inter Milan, Sporting Lisbon, Villareal, Lyon, Real Madrid.

No comments:

Powered By Blogger