Saturday 13 December 2008

MCHEZAJI BORA DUNIANI KUJULIKANI JANUARI 12: Listi yapunguzwa hadi Wagombea Watano!!!

Winga wa Manchester United, Cristiano Ronaldo na Straika wa Liverpool, Fernando Torres, wamo katika listi ya mwisho ya Wachezaji watano wanaogombea Tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia inayotolewa na FIFA.
Uteuzi huo wa Wachezaji hao watano umefanywa na Makocha na Manahodha wa Timu za Taifa za Nchi kutoka duniani kote.
Wachezaji wengine watatu ni Kaka wa AC Milan, nyota wa Barcelona Lionel Messi na Xavi wa Barcelona.
Ronaldo, ambae alipata Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ulaya [Ballon D'Or] siku ya Jumapili, alimaliza nafasi ya 3 kwenye Tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia wa FIFA mwaka uliopita nyuma ya Messi na Mshindi Kaka.
Mshindi atakabidhiwa Tuzo yake huko Zurich, Uswisi kwenye Jumba la Opera la Zurich Januari 12, 2009.
Kwa upande wa wanawake mshindi atakuwa kati ya Nadine Angerer, Cristiane, Marta, Birgit Prinz au Kelly Smith.
Kwa kina mama, Marta wa Brazil [pichani] ndie Mshindi mwaka uliopita na anapewa nafasi kubwa kushinda tena.

No comments:

Powered By Blogger