Sunday 7 December 2008


West Brom 1 Portsmouth 1

West Brom imefanikiwa kupata pointi moja baada ya kutoka suluhu leo na Portsmouth lakini bado ndio timu ya mwisho kwenye msimamo wa LIGI KUU ikiwa nafasi ya 20 na pointi 12 kwa mechi 16.
Nafasi ya 19 inashikwa na Blackburn ikiwa nayo imecheza mechi 16 na ina pointi 13.
Sunderland ni ya 18 kwa mechi 16 na pointi 15.
West Bromwich ilikuwa wa kwanza kupata bao wakati Nahodha wao Jonathan Greening alipofunga dakika ya 39 lakini Peter Crouch wa Portsmouth alisawazisha dakika ya 58 kwa shuti kali la mita kama 20 hivi.
Kimsimamo, Portsmouth wako nafasi ya 7 wamecheza mechi 16 na wana pointi 23.
Everton 2 Aston Villa 3
Ni mechi iliyoanza kwa bao la kwanza kupatikana sekunde 34 tu tangu mechi ianze!
Steve Sidwell, akipokea pasi kutoka kwa James Milner, alifumua mkwaju na kuipatia Aston Villa bao la kuongoza.
Dakika ya 30, wenyeji Everton wakasawazisha kupitia Beki wao John Lescott kufuatia fikikiki ya Arteta.
Kipindi cha pili dakika ya 54 Beki wa kutumainiwa wa Everton Phil Jagielka akiwa mtu wa mwisho kwenye safu ya ulinzi aligeuka na kurudisha mpira nyuma kwa Kipa wake Tim Howard bila ya kutazama kumbe alikuwa akitoa pasi murua kwa adui Winga Ashley Young ambae akaipa kilaini Aston Villa bao la pili.
Zikiwa dakika 90 zimekwisha na mechi iko kwenye dakika 3 za nyongeza, John Lescott tena akaisawazishia Everton baada ya krosi ya Jagielka kumkuta Cahill aliempasia mfungaji Lescott aliefunga goli zuri sana dakika ikiwa ya 92.
Dakika ya 93, Ashley Young akaipa bao la ushindi Aston Villa baada ya defensi ya Everton kujikoroga yenyewe.

No comments:

Powered By Blogger