Wednesday 10 December 2008

UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
TIMU 16 ZINAZOINGIA RAUNDI YA MTOANO ZAPATIKANA!!

Mechi za jana za UEFA CHAMPIONS LEAGUE zimetoa Timu 3 zilizobaki ili kufanya idadi ya timu kuwa 16 zitakazocheza Raundi inayofuata ya Mtoano.
Dro ya kuamua timu ipi inakutana na ipi kwa mechi za nyumbani na ugenini ili kupata timu 8 zitakazoingia Robo Fainali itafanyika tarehe 19 Desemba 2008.
Mechi za Raundi hii ya Mtoano zitachezwa tarehe 24 na 25 Februari 2009 na marudiano ni tarehe 10 na 11 Machi 2009.
Katika Timu hizo 16 zilizofuzu 4 zinatoka England, nazo ni Manchester United, Chelsea, Liverpool na Arsenal na 4 nyingine zinatoka Spain ambazo ni Real Madrid, Barcelona, Villareal na Atletico Madrid.
Timu zilizobaki ni AS Roma, Inter Milan, Panathinaikos, Sporting Lisbon, Lyon, Bayern Munich, FC Porto na Juventus.
Katika hiyo Dro ya Raundi ya Mtoano Timu kutoka nchi moja na zile zilizokuwa Kundi moja haziruhusiwi kukutana.
Pia Timu iliyoongoza Kundi itapambanishwa na Timu iliyokuwa ya pili toka Kundi jingine.
Timu amabazo jana zilipata nafasi ya tatu katika msimamo wa Makundi na ambazo sasa zitaingizwa UEFA CUP ni: Bordeaux, Werder Bremen, Shakhtar Donetsk na Marseille.

MATOKEO MECHI ZA Jumanne, 9 Decemba 2008

KUNDI A
Chelsea 2 v CFR 1,
Roma 2 v Bordeaux 0,
Msimamo:
1 Roma 12 pts
2 Chelsea 11 pts
3 Bordeaux 7 pts
4 CFR Cluj 4 pts

KUNDI B
Werder Bremen 2 v Inter Milan 1,
Panathinaikos 1 v Anorthosis Famagusta 0,
Msimamo:
1 Panathinaikos 10 pts
2 Inter Milan 8 pts
3 Werder Bremen 7 pts
4 Anorthosis 6 pts

KUNDI C
Barcelona 2 v Shakhtar Donetsk 3,
Basle 0 v Sporting 1,
Msimamo:
1 Barcelona 13 pts
2 Sporting Lisbon 12 pts
3 Shakhtar Donetsk 9 pts
4 Basle 1 pt

KUNDI D
Marseille 0 v Atletico Madrid 0,
PSV 1 v Liverpool 3,
Msimamo:
1 Liverpool 14 pts
2 Atletico Madrid 12 pts
3 Marseille 4 pts
4 PSV 3 pts

MECHI ZA LEO: Jumatano, 10 Decemba 2008

Ingawa Timu zote 16 zitakazocheza Raundi ya Mtoano zimepatikana, umuhimu wa mechi za leo ni kuamua nani ataongoza kwenye Kundi na nani atacheza UEFA.

KUNDI E
Celtic v Villarreal,
Man U v AaB,

KUNDI F
Steaua Bucuresti v Fiorentina
Lyon v Bayern Munich

KUNDI G
Dynamo Kiev v Fenerbahce,
FC Porto vArsenal,

KUNDI H
Juventus v BATE
Real Madrid v Zenit St Petersburg

No comments:

Powered By Blogger