Saturday 13 December 2008

Ronaldo ajiunga na Corinthians

Aliekuwa nyota wa Brazil Ronaldo de Lima ambae aliumia vibaya goti lililomlazimu kuiacha klabu ya Italia AC Milan mwezi Juni ametangazwa kujiunga na klabu ya Sao Paulo, Brazil iitwayo Corinthians.
Ronaldo aliumia goti hilo mwezi Februari na mkataba wake na AC Milan uliisha Juni.


Kipa Van der Sar aongeza mkataba

Golikipa wa Mabingwa Manchester United, Edwin van der Sar [38], ameongeza mwaka mmoja katika mkataba wake na sasa atabaki klabuni hapo hadi mwaka 2010.
Van der Sar alijiunga Man U Juni 2005 akitokea klabu ya Fulham. Awali alichezea klabu za Ajax na Juventus.


Barcelona v Real Madrid leo Nou Camp!

Timu inayosuasua kwenye Ligi ya Spain, La Liga, na ambayo siku ya Jumannne ilimtimua Meneja wake Bernd Schuster na kumchukua Juande Ramos ambae nae alietimuliwa Tottenham, Real Madrid, leo inaingia myumbani kwa mahasimu wao na vinara wa ligi, Barcelona, uwanjani Nou Camp.
Mpaka sasa Real Madrid wako nafasi ya 5 wakiwa pointi 9 nyuma ya viongozi wa La Liga Barcelona.
Juande Ramos amepewa mkataba wa miezi 6 tu kuwa Meneja wa Real Madrid na kumfanya awe Meneja wa 8 wa klabu hiyo katika miaka 6 iliyopita.

Mechi ya leo itachezwa saa 6 usiku saa za bongo.

No comments:

Powered By Blogger