Friday 19 December 2008

JOSE MOURINHO: 'Ni furaha kukutanishwa na Timu Bora!!'

-Aikandya ARSENAL!!!

Jose Mourinho, aliekuwa Meneja wa Chelsea na kwa sasa yuko Italia akiiongoza Inter Milan timu ambayo haijachukua Ubingwa wa Ulaya tangu 1965, ametamka ana furaha timu yake kukutana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United kwenye Raundi ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE kwa sababu ndio timu bora.
Mourinho alisema: 'Nimeridhika! Nilitaka timu bora nimeipata! Pengine baada ya siku mbili watakuwa Mabingwa wa Dunia! Wana Mchezaji Bora Ulaya, Ronaldo, Meneja Bora, Ferguson na Kiwanja Bora, Old Trafford!'
Mbali ya Liverpool, watakaopambana na Real Madrid, Timu zote 3 nyingine za England zitapambana na Klabu za Italia kuwania Ubingwa huo wa Klabu za Ulaya.
Chelsea na Juventus, Arsenal na AS Roma, Manchester United na Inter Milan.
Nae Jose Mourinho, kama alivyokuwa Chelsea, hakuacha kukandya!
Alisema: 'Mechi zote 3 kwa Timu za Italia ni fifte fifte lakini AS Roma wanaurahisi kidogo kwa sababu Arsenal sio Chelsea au Manchester United!'


RATIBA:

Jumanne, 24 Februari 2009

Arsenal v AS Roma

Atletico Madrid v FC Porto

Inter Milan v Man U

Lyon v Barcelona

Jumatano, 25 Februari 2009

Chelsea v Juventus

Real Madrid v Liverpool

Sporting v Bayern Munich

Villarreal v Panathinaikos

Jumanne, 10 Machi 2009

Bayern Munich v Sporting

Juventus v Chelsea

Liverpool v Real Madrid

Panathinaikos v Villarreal

Jumatano, 11 Machi 2009

Barcelona v Lyon

FC Porto v Atletico Madrid

Man U v Inter Milan

Roma v Arsenal
DRO YA RAUNDI YA MTOANO YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE YAFANYWA!!

Mabingwa Watetezi wa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya Manchester United wamepangiwa kukutana na Timu inayoongozwa na aliekuwa Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, ambae kwa sasa yuko Italia akiwa na Inter Milan.
Mechi ya kwanza kati ya Inter Milan na Manchester United itachezwa nyumbani kwa Inter Milan kati ya Februari 24 au 25, 2009 na mechi ya marudiano ni kati ya Machi 10 au 11, 2009 uwanjani Old Trafford.
Timu nyingine za Uingereza zilizo kwenye raundi hii ni Chelsea watakaocheza na Juventus, Liverpool atakumbana na Real Madrid na Arsenal atapambana na Roma.
Washindi wa Raundi hii wataingia Robo Fainali.

RATIBA KAMILI NI: [Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]
-Mechi za kwanza ni 24 na 25 Februari na marudiano ni 10 na 11 Machi 2009.

Chelsea v Juventus

Villareal v Panathinaikos

Sporting Lisbon v Bayern Munich

Atletico Madrid v FC Porto

Lyon v Barcelona

Real Madrid v Liverpool

Arsenal v Roma

Inter Milan v Manchester United

DRO YA UEFA CUP:

Sambamba na Dro ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE, vilevile ilifanyika Dro ya Kombe la UEFA ambayo ilijumuisha jumla ya Timu 32 zikiwemo Timu 8 zilizokuwa Washindi wa tatu kwenye Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Washindi wa mechi hizo zitakazochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini wataingia RAUNDI YA Timu 16 za mwisho ambayo pia Dro yake ilifanywa.
Uingereza inawakilishwa na Timu za Aston Villa, Tottenham na Manchester City.
Kwenye RAUNDI YA TIMU 32, Aston Villa anacheza na CSKA Moscow, Tottenham v Shakhtar Donetsk na Manchester City v FC Copenhagen.
Lakini kwenye RAUNDI YA TIMU 16, Aston Villa na Tottenham huenda wakapambana endapo watashinda mechi zao za RAUNDI YA TIMU 32.

RATIBA KAMILI NI:

MECHI ZA RAUNDI YA TIMU 32 (Mechi ya kwanza 18-19 Feb na mechi ya marudiano 26 Feb 2009):

Paris Saint-Germain v Wolfsburg

FC Copenhagen v MANCHESTER CITY

NEC Nijmegen v Hamburg

Sampdoria v Metalist Kharkiv

Braga v Standard Liege

ASTON VILLA v CSKA Moscow

Lech Poznan v Udinese

Olympiakos v Saint-Etienne

Fiorentina v Ajax

Aalborg v Deportivo La Coruna

Werder Bremen v AC Milan

Bordeaux v Galatasaray Dynamo Kiev v Valencia

Zenit St. Petersburg v Stuttgart

Marseille v FC Twente

Shakhtar Donetsk v TOTTENHAM

MECHI ZA RAUNDI YA TIMU 16 (Mechi ya kwanza 12 Mar na marudiano 18-19 Mar 2009):

Werder Bremen AU AC Milan v Olympiakos AU Saint-Etienne

ASTON VILLA AU CSKA Moscow v Shakhtar Donetsk AU TOTTENHAM

Lech Poznan AU Udinese v Zenit St Petersburg AU Stuttgart

Paris Saint-Germain AU Wolfsburg v Braga AU Standard Liege

Dynamo Kiev AU Valencia v Sampdoria AU Metalist Kharkiv

Copenhagen AU MANCHESTER CITY v Aalborg AU Deportivo

Marseille AU FC Twente v Fiorentina AU Ajax

NEC Nijmegen AU Hamburg v Bordeaux AU Galatasaray

Thursday 18 December 2008

KOMBE LA DUNIA LA KLABU: MAN U watinga Fainali!!!!

Mabingwa wa Ulaya Manchester United leo wamewachakaza wenyeji wa mashindano Gamba Osaka ya Japan ambao pia ni Mabingwa wa Asia kwa mabao 5-3 na hivyo kuingia Fainali ya Kombe la Dunia ya Klabu na sasa watavaana na Liga de Quito ya Ecuador siku ya Jumapili tarehe 21.
Timu zilikuwa:

Gamba Osaka: Fujigaya, Kaji, Nakazawa, Yamaguchi, Endo, Michihiro Yasuda, Myojin, Hashimoto, Bando (Terada 85), Lucas, Yamazaki.
Akiba hawakucheza: Matsuyo, Shimohira, Futagawa, Kurata, Takei, Roneliton.
Kadi: Yamaguchi.
Magoli: Yamazaki 74, Endo 85 pen, Hashimoto 90.
Man Utd: Van der Sar, Neville, Ferdinand, Vidic (Evans 69), Evra, Nani, Anderson, Scholes (Fletcher 67), Ronaldo, Giggs, Tevez (Rooney 73).
Akiba hawakucheza: Kuszczak, Rafael Da Silva, O'Shea, Carrick, Gibson, Park, Welbeck, Amos.
Kadi: Rooney.
Magoli: Vidic 28, Ronaldo 45, Rooney 75, Fletcher 78, Rooney 79.
Watazamaji: 67,618
Refa: Benito Archundia Tellez (Mexico).

Wednesday 17 December 2008

Allardyce atua Blackburn Rovers!

Sam Allardyce ametangazwa kuwa Meneja mpya wa Blackburn Rovers kuchukua nafasi ya Paul Ince aliefukuzwa.
Allardyce alikuwa Meneja wa Bolton na baadae Newcastle.
Liga de Quito yatinga FAINALI!

Klabu ya Liga de Quito ya Ecuador ambao ndio Mabingwa wa Marekani Kusini wametinga Fainali ya KLABU BINGWA DUNIANI baada ya kuipiga Pachuca bao 2-0 na watakutana na mshindi kati ya Gamba Osaka na Manchester United wanaocheza kesho.
Mabao ya Claudio Bieler dakika ya 4 na Luis Alberto Bolanos dakika ya 25 ndio yaliwaua Pachuca.
Sasa Liga de Quito wako FAINALI itakayochezwa JUMAPILI tarehe 21 DESEMBA 2008 mjini Yokohama, Japan.

Tuesday 16 December 2008

MAN U haikati rufaa kupinga adhabu ya EVRA!!!

Manchester United imeamua kutokata rufaa kupinga adhabu ya kufungiwa mechi 4 na faini ya Pauni 15,000 ya Mchezaji wao Patrice Evra aliyopewa na FA baada ya kupatikana na hatia ya kupigana na Mfanyakazi mkata nyasi wa Uwanja wa Chelsea, Stamford Bridge, aitwae Sam Bethell, ugomvi uliotokea mara baada ya mechi kati ya Chelsea na Man U msimu uliopita.
Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson alistushwa na kukasirishwa na adhabu hiyo aliyoiita 'ni uamuzi mbovu ambao sijawahi kuuona!'.
Katika taarifa yake, Klabu ya Manchester United imesisitiza kwamba adhabu hiyo haikustahili, ina kasoro nyingi na kuikatia rufaa ni kupoteza muda hasa wakati klabu inaingia awamu ya pili ya LIGI KUU.
Vilevile, Man U wamesema kumfungia Mchezaji mechi 4 ambae hajawahi kupewa Kadi Nyekundu hata moja wakati wale wanaocheza rafu mbaya sana na wale wanaolipiza kwa kuwarushia Watazamaji vitu walivyorushiwa kufungiwa mechi 3 tu, ni ukiukwaji mkubwa wa haki.
Evra, ambae kwa sasa yuko Japan pamoja na kikosi kamili cha Man U kitakachoshiriki Mashindano ya Klabu Bingwa Duniani, atazikosa mechi za LIGI KUU za Man U watakapocheza na Stoke na Middlesbrough, Kombe la FA dhidi ya Southampton hapo tarehe 3 Januari 2009 na pambano la kwanza la Nusu Fainali ya Kombe la Carling dhidi ya Derby litakalochezwa siku nne baadae.
Mechi yake ya kwanza anayoweza kurudi uwanjani itakuwa ni pambano la kukata na shoka la LIGI KUU litakalofanyika Old Trafford dhidi ya klabu iliyomtia matatizoni, Chelsea, hapo tarehe 11 Januari 2009.
LIGI KUU ENGLAND: Kipindi kigumu kinaingia!!!

Inasemekana, hakika inaaminika hasa kwa wafuatiliaji wazuri wa historia ya LIGI KUU ENGLAND, mechi zinazochezwa mwezi Desemba hasa wakati wa kipindi cha Sikukuu ya Krismas ambako kunakuwa mechi za 'kubanana' na zinazoendelea mfululizo hadi Januari, ndizo zinazotoa mwelekeo wa nani anaweza kuwa Bingwa.
Wakati tunaelekea kipindi hicho, msimamo wa ligi mpaka sasa kwa Timu 5 za juu ni kama ifuatavyo:

-Liverpool mechi 17 pointi 38

-Chelsea mechi 17 pointi 37

-Man U mechi 16 pointi 32

-Aston Villa mechi 17 pointi 31

-Arsenal mechi 17 pointi 30

Mabingwa Watetezi Manchester United wamecheza mechi moja pungufu kwa sababu walienda kucheza mechi ya UEFA SUPER CUP na mechi yao dhidi ya Fulham ikaahirishwa.
Mechi hii sasa imepangwa kuchezwa tarehe 17 Februari 2009.

Ratiba ya mechi za 'VIGOGO' hao wa LIGI KUU katika kipindi hiki ambacho kawaida hutoa fununu wa nani anaunusa ubingwa ni kama ifuatavyo:

[Timu inayotajwa kwanza iko nyumbani]

MANCHESTER UNITED:

-Stoke v Man U [26 Desemba]
-Man U v Middlesbrough [29 Desemba]
-Man U v Chelsea [11 Januari]
-Man U v Wigan [14 Januari] [Hiki ni kiporo.
Mechi hii ilitakiwa ichezwe Desemba 21 lakini Man U watakuwa Japan kwenye Kombe la Dunia la Klabu]

CHELSEA

-Everton v Chelsea [22 Desemba]
-Chelsea v West Brom [26 Desemba]
-Fulham v Chelsea [28 Desemba]
-Man U v Chelsea [11 Januari]

ARSENAL

-Arsenal v Liverpool [21 Desemba]
-Aston Villa v Arsenal [26 Desemba]
-Arsenal v Portsmouth [28 Desemba]
-Arsenal v Bolton [10 Januari]

LIVERPOOL

-Arsenal v Liverpool [21 Desemba]
-Liverpool v Bolton [26 Desemba]
-Newcastle v Liverpool [28 Desemba]
-Stoke v Liverpool [10 Januari]

Hebu tusubiri tuone nani atavuka hivi vigingi na kuibuka kidedea.
PAUL INCE ATIMULIWA BLACKBURN!!

Klabu ya Blackburn Rovers imemfukuza kazi Meneja wake Paul Ince kufuatia matokeo mabaya kwenye LIGI KUU.
Ince alijiunga Blackburn mwezi Juni akitoka MK Dons na kuiongoza timu hiyo kwenye mechi 17 za LIGI KUU lakini wameshinda mechi 3 tu kati ya hizo na ushindi wao wa mwisho ulitokea Septemba 27 walipoifunga Newcastle.
Kwa sasa Blackburn ipo nafasi ya 19 kwenye msimamo wa ligi yaani timu ya pili toka mwisho.
Mwenyekiti wa Blacburn John Williams akitangaza uamuzi huo wa kumtimua alisema: 'Ushindi wa mechi 3 katika 17 kwa timu iliyomaliza ligi nafasi ya 7 msimu uliopita na kutufanya sasa tuwe wa 19 kati ya timu 20 haukubaliki!'
Paul Ince ameweka historia ya kuwa Meneja wa kwanza mweusi kuongoza klabu iliyo LIGI KUU.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Benitez alazwa hospitali jana, augua ugonjwa uleule uliomlaza Scolari juzi!!!
Klabu ya Liverpool imethibisha Meneja wao Rafa Benitez alikimbizwa hospitali Jumatatu usiku na inabidi afanyiwe operesheni ndogo baadae wiki hii kwa kuwa anasumbuliwa na vijiwe kwenye figo.
Taarifa hizi zimekuja masaa 24 tu tangu Meneja wa Chelsea Luis Felipe Scolari alazwe hospitali kwa usiku mmoja kwa tatizo la aina hiyohiyo.
Katika msimamo wa LIGI KUU, Liverpool ndio inaongoza ikifuatiwa na Chelsea walio pointi moja nyuma.
Rooney, Ronaldo wanusurika adhabu

Nyota wa Manchester United, Wayne Rooney na Cristiano Ronaldo, wamenusurika kubandikwa adhabu na UEFA na FA baada ya kutuhumiwa kutenda makosa katika mechi na makosa hayo kutoonwa na Marefa wa mechi hizo.
Rooney alituhumiwa kumkanyaga Mlinzi wa Aalborg ya Denmark Kasper Risgard kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE kati ya Man U na Aaalborg iliyochezwa Old Trafford Jumatano iliyopita.
Baada ya UEFA kupitia mkanda wa video wameamua hakuna hatua zozote zinastahili kuchukuliwa.
Baada ya mechi hiyo, Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, aliwapandishia Waandishi wa Habari kwa kulivalia njuga tukio ambalo halikustahili chochote.
Nae Ronaldo alituhumiwa kumpiga teke Mlinzi wa Tottenham Michael Dawson kwenye mechi ya Tottenham na Manchester United siku ya Jumamosi.
FA ilimtaka Refa wa pambano hilo Mike Dean kulitazama tena tukio hilo kwenye video na kuamua kama angeliliona angechukua hatua gani lakini Dean alithibitisha hata kama angeliona asingempa Ronaldo Kadi Nyekundu.

Monday 15 December 2008

Mabingwa Man U watua Tokyo, Japan kucheza KOMBE LA KLABU BINGWA DUNIANI

Kikosi cha Wachezaji 23 wa Mabingwa wa Ulaya Manchester United kikiongozwa na Meneja wao Sir Alex Ferguson leo asubuhi kimetua Uwanja wa Ndege wa Narita mjini Tokyo [pichani] ili kupambana kwenye Nusu Fainali ya FIFA CLUB WORLD CUP na Gamba Osaka ya Japan ambao ndio Mabingwa wa Asia.
Jana Gamba Osaka iliifunga Adelaide United ya Australia bao 1-0 na kuingia Nusu Fainali.
Mechi hii itachezwa siku ya Alhamisi tarehe 18 Desemba 2008 saa 7 na nusu mchana kwa saa za bongo.
Kikosi cha Man U kilichopo Japan ni:
MAKIPA: Van der Sar, Kuszczak, Amos; WALINZI: Neville, Evra, Ferdinand, Vidic, O'Shea, Evans, Rafael; VIUNGO: Ronaldo, Anderson, Giggs, Park, Carrick, Nani, Scholes, Fletcher, Gibson; WASHAMBULIAJI: Berbatov, Rooney, Tevez, Welbeck.
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Harry Redknapp: 'Bingwa ni Man U au Chelsea!'
Meneja wa Tottenham Harry Redknapp amesema Bingwa wa England msimu huu atakuwa Chelsea au Watetezi Man U na hadhani kama Liverpool ana ubavu wa kuhimili mikikimikiki ya muda mrefu.
Redknapp, ambae Timu yake Tottenham ililazimisha sare ya 0-0 ilipocheza na Mabingwa Man U juzi, alisema: 'Mmoja kati ya Chelsea au Man U atashinda. Arsenal wamepoteza pointi nyingi na siwaoni kama wanaweza kurudi kwenye kinyang'anyiro! Nao Liverpool wanawategemea sana Steve Gerrard na Fernando Torres! Sijui kiktokea kitu kwa hao wawili watafanya nini na hivyo wana mapungufu ukilinganisha na vikosi vya Chelsea na Man U!'
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
LIGI KUU ENGLAND: MECHI ZA WIKIENDI [saa ni za bongo]
JUMAMOSI, 20 Desemba 2008
[saa 12 jioni]

Blackburn v Stoke

Bolton v Portsmouth

Fulham v Middlesbrough

Hull v Sunderland

[saa 2 na nusu usiku]

West Ham v Aston Villa

JUMAPILI, 21 Desemba 2008

[saa 10 na nusu jioni]

West Brom v Man City

[saa 12 jioni]

Newcastle v Tottenham

[saa 1 usiku]

Arsenal v Liverpool

JUMATATU, 22 Desemba 2008
[saa 5 usiku]

Everton v Chelsea

Sunday 14 December 2008

LIGI KUU ENGLAND: Nao Chelsea wakwama!!!

Chelsea leo wameshindwa kuchukua mwanya wa Liverpool kutoka suluhu ya bao 2-2 na Hull City hapo jana na wao kushinda leo ili wachukue uongozi wa ligi baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na West Ham wakiwa nyumbani kwao Stamford Bridge.
West Ham, wakiongozwa na Meneja wao Gianfranco Zola ambae alikuwa Mchezaji nyota hapo Chelsea, walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Craig Bellamy aliefunga dakika ya 33.
Nicholas Anelka aliisawazishia Chelsea dakika ya 51.
Matokeo hayo yanawafanya Liverpool waendelea kuongoza ligi wakiwa na pointi 38 kwa mechi 17, Chelsea wanafuata pointi 37 kwa mechi 17, kisha Mabingwa Man U pointi 32 mechi 16, Aston Villa pointi 31 mechi 17 na Arsenal ni wa 5 wakiwa na pointi 30 kwa mechi 17.

Portsmouth 0 Newcastle 3

Katika mechi ya awali ya LIGI KUU leo, Newcastle, ikiwa ugenini, iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Portsmouth huo ukiwa wa ushindi wao wa kwanza wa mechi za ugenini msimu huu ambao umewafanya kuchupa hadi nafasi ya 14 kutoka nafasi ya 18.
Hadi mapumziko mechi ilikuwa 0-0 na kipindi cha pili mabao ya Nahodha wao Michael Owens dakika ya 52, Obafemi Martins dakika ya 77 na la Guthrie dakika ya 89 yaliwapa ushindi.
GAMBA OSAKA yatinga Nusu Fainali, kuikwaa MAN U Alhamisi!

Leo, Mabingwa wa Asia, Gamba Osaka ya Japan, imeipachika Adelaide United ya Australia, timu iliyoshika nafasi ya pili katika Ubingwa wa Asia. bao 1-0 na kuingia Nusu Fainali watakakopambana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United siku ya Alhamisi tarehe 18 Desemba 2008.
Katika mechi iliyochezwa Toyota Stadium mjini Tokyo, Japan, Mchezaji wa Gamba Osaka Yasuhito Endo alipachika bao la ushindi dakika ya 23.
Timu hizi, Gamba Osaka na Adelaide United, zilikutana wiki kadhaa nyuma kwenye Fainali ya Klabu Bingwa Asia na Gamba Osaka waliibuka kidedea baada ya kuichabanga Adelaide United katika mechi zote mbili jumla ya Mabao 5-0 ikiwa 3-0 mechi iliyochezwa Japan na 2-0 mechi iliyochezwa Australia.
LIGI KUU ENGLAND: Liverpool, Arsenal na Man U wabanwa mbavu! Chelsea leo!

Vigogo Man U, Liverpool na Arsenal jana walitoka suluhu katika mechi zao za LIGI KUU na sasa nafasi iko wazi kwa Chelsea kuchukua uongozi wa ligi hiyo toka mikononi mwa Liverpool endapo watawafunga West Ham kwenye mechi yao ya leo itakayochezwa Stamford Bridge saa 1 usiku saa za bongo.
Liverpool, akiwa kwake Anfield, alijikuta yuko nyuma kwa bao 2-0 walipocheza na Hull ndani ya dakika 22 za kwanza kwa mabao yaliyofungwa na McShane dakika ya 12 na Beki wa Liverpool Carragher akajifunga mwenyewe dakika ya 22.
Nahodha wa Liverpool Steve Gerrard akaokoa jahazi kwa kurudisha mabao yote kwenye dakika za 24 na 32.
Arsenal waliocheza ugenini uwanjani Riverside dhidi ya Middlesbrough, walipata bao dakika ya 17 kupitia Adebayor lakini Boro wakasawazisha kupitia Mchezaji wao ambae zamani alikuwa Arsenal Aliadiere dakika ya 29.
Nao Mabingwa Man U wakicheza ugenini White Hart Lane nyumbani kwa Tottenham, walilazimishwa sare ya 0-0 huku Kipa wa Spurs Gomez akiibuka nyota kwa kuokoa mipira mingi ya hatari ya Wachezaji wa Man U.
Ronaldo alifanikiwa kupachika bao lakini Mwamuzi Mike Dean alilikataa kwa kudai aliunawa kabla ya kufunga.

MATOKEO MECHI NYINGINE:

Aston Villa 4 Bolton 2

Man City 0 Everton 1

Stoke o Fulham 0

Sunderland 4 West Brom 0

Wigan 3 Blackburn 0

MECHI ZA LEO:

Portsmouth v Newcastle [saa 10 na nusu mchana]

Chelsea v West Ham [saa 1 usiku]

LA LIGA: Barcelona 2 Real Madrid 0

Magoli yaliyofungwa na Samuel Etoo dakika ya 80 na Lionel Messi kwenye dakika za majeruhi yamewaua Mahasimu Real Madrid na kuwafanya Barcelona waendelee kuongoza Ligi ya Spain na kuwa pointi 12 mbele ya Real Madrid.

FIFA CLUB WORLD CUP:

Leo ni mechi kati ya Mabingwa wa Asia, Gamba Osaka ya Japan na Adelaide United ya Australia ambao ni Washindi wa pili wa Klabu Bingwa Asia.
Katika mechi ya awali, Adelaide United waliifunga Waitakere United ya New Zealand 2-0.
Mshindi wa mechi hii atapambana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United siku ya Alhamisi Desemba 18 katika Nusu ya pili.
Powered By Blogger