Wednesday 17 December 2008

Liga de Quito yatinga FAINALI!

Klabu ya Liga de Quito ya Ecuador ambao ndio Mabingwa wa Marekani Kusini wametinga Fainali ya KLABU BINGWA DUNIANI baada ya kuipiga Pachuca bao 2-0 na watakutana na mshindi kati ya Gamba Osaka na Manchester United wanaocheza kesho.
Mabao ya Claudio Bieler dakika ya 4 na Luis Alberto Bolanos dakika ya 25 ndio yaliwaua Pachuca.
Sasa Liga de Quito wako FAINALI itakayochezwa JUMAPILI tarehe 21 DESEMBA 2008 mjini Yokohama, Japan.

No comments:

Powered By Blogger