
Chelsea v Aston Villa
Meneja wa Arsenal Arsena Wenger, baada ya mstuko wa kupigwa na 'vibonde' Hull City Jumamosi uliomfanya aweweseke hadi kukosea kutaja timu iliyomfunga na kuiita West Brom na kuahidi shoka litatembea kwa Wachezaji kwenye mechi ya jana, alikuwa mtu mwenye furaha kubwa jana baada ya ushindi wa mabao 4-0.
Wenger hakutimiza ahadi yake ya shoka ingawa hakumchezesha Eboue na badala yake Samir Nasri alianza na dakika ya 64 Eboue akambadilisha Nasri.
Wenger alinena kwa furaha: 'Sikufanya mabadiliko kwani sikutaka nionekane natoa adhabu kwa Wachezaji. Ni bora uipe timu nafasi ijirekebishe makosa!'
Sir Alex Ferguson akumbwa na majeruhi!!!
Ingawa Mabingwa wa Ulaya, Manchester United, wamefurahia ushindi wa mabao 3-0 ugenini huko Aalborg, Denmark walipoitwanga Aab Aalborg, ushindi huo pengine umekuja kwa gharama kubwa kutokana na kuumia kwa Wachezaji muhimu sana kwa timu.
Paul Scholes aliumia goti dakika ya 16 tu ya mchezo na akatolewa kwa machela na nafasi kuchukuliwa na Ryan Giggs. Mwishoni mwa mechi Scholes alionekana akitembelea kwa magongo. Ferguson alisema huenda Scholes akawa nje ya uwanja kwa wiki hadi 8.
Pigo la pili lilikuwa kuumia enka kwa Wayne Rooney ingawa taarifa zilisema kutolewa kwake uwanjani ilikuwa ni tahadhari tu na maumivu yake si ya kutisha kama ya Scholes. Nafasi ya Rooney kwenye mechi hiyo ilichukuliwa na Carlos Tevez.
Pigo la tatu ni kuumia kwa Beki chipukizi Rafael kutoka Brazil ambae alikuwa akianza mechi kubwa kwa mara ya kwanza na nafasi yake kushikwa na Wes Brown.
Nae Dimitar Berbatov aliefungua akaunti yake ya kufunga magoli kwa Man U hapo jana alipofunga bao 2 amemkosha Ferguson aliemsifia sana: 'Berbatov amefunga magoli mawili maridadi sana! Magoli hayo ya mwanzo kuifungia Man U yatampa morali kubwa!'
Leo katika mechi ya KUNDI E ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE Mabingwa watetezi Manchester United wako nchini Denmark kwenye mji mdogo uitwao Aalborg kupambana na timu ndogo lakini ndio Mabingwa wa Denmark Aab Aalborg.
Mechi hii itakayoanza saa 3 dakika 45 usiku, saa za bongo, itachezwa kwenye Uwanja uitwao Energi Nord Arena wenye uwezo wa kuchukua Watazamaji 10,000 tu.
Aab Aalborg ilitoka sare kwenye mechi ya kwanza ya Kundi hili ilipocheza ugenini na Celtic huko Scotland. Kipa wa Aab Alborg Karim Zaza toka Morocco alikuwa shujaa alipookoa penalti kwenye mechi hiyo.
Aab Aalborg inaongozwa na Meneja ambae kama Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson ni mtu wa Scotland. Bruce Rioch, mwenye umri wa miaka 61, ni Mchezaji wa zamani wa Aston Villa na ameshawahi kuwa Meneja wa timu za LIGI KUU Middlesbrough na Arsenal.
Bruce Rioch ndie aliemsaini Dennis Berkamp na mwaka 1996 akiwa Meneja wa Arsenal waliwahi kuwafunga Man U kwa bao la Bergkamp.
Kikosi cha Aab Aalborg kina vijana wengi wa Timu ya Taifa ya Denmark ya umri wa chini ya miaka 21 ingawa kuna Wachezaji kadhaa toka nje ya nchi kama Kipa Karim Zaza [Morocco], Marek Saganowski (Poland), Andreas Johansson (Sweden) na Michael Beauchamp (Australia).
Wengi wanahisi hii ni mechi kati ya Klabu ndogo na maskini zidi ya Klabu kubwa na tajiri. Hebu linganisha: Uwanja wa Aalborg, Energi Nord Arena, una uwezo wa kuchukua Watazamaji 10,000 tu wakati Old Trafford wa Man U unapakia watu zaidi ya 76,000! Dau lililolipwa kumnunua Dimitar Berbatov toka Tottenham kuja Man U la Pauni Milioni 30 ni bajeti ya kuiendesha Aab Alborg kwa miaka 7!
Juu ya yote hayo, Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema: 'Timu za Denmark ni wapiganaji! Hatuwadharau hivyo ntashusha kikosi changu kamili.'
MENEJA MPYA WA NEWCASTLE KUANZA KAZI AKIWA AMEKAA KWA WATAZAMAJI!
Joe Kinnear ambae ameteuliwa wiki iliyopita kuwa Meneja wa Muda wa Newcastle hadi mwisho wa mwezi wa Oktoba inapotegemewa Klabu huenda ikapata mmiliki mpya ataanza kazi yake kwa kukaa na Watazamaji badala ya benchi la Timu yake baada ya FA , Chama cha Soka Uingereza, kufafanua kuwa Meneja huyo bado hajatumikia adhabu aliyopewa mwaka 2004 ya kufungiwa mechi mbili na hivyo kutokukaa benchi la timu.
Joe Kinnear alipewa adhabu hiyo mwaka 2004 alipokuwa Meneja wa Nottingham Forest baada ya mechi waliyofungwa na Gillingham alipomwita Refa wa mechi hiyo 'ze comedy' yaani Msanii Mwigizaji na Mchekeshaji!
Wakati huo Kinnear alijitetea kuwa aliuliza: 'Huyu Refa anafanya shughuli gani na nikaambiwa ni Mwigizaji/Mchekeshaji basi nikaamua kumwita jina la 'COCO' yule Mchekeshaji maarufu!'
Tangu wakati huo mwaka 2004 Joe Kinnear alikuwa nje ya soka hadi wiki iliyopita.
Hivyo FA imetamka kifungo chake kimeanza kwa mechi ya Jumamosi walipofungwa 2-1 na Blackburn na mechi ya pili atakayoikosa ni ya tarehe 5 Oktoba 2008 watakapocheza na Everton.
WIGAN 2 MANCHESTER CITY 1
Wakiwa na Wachezaji watatu ambao wamo Timu ya Taifa ya Brazil, Manchester City walijikuta wakibebeshwa bao 2-1 na Wigan katika mechi ya LIGI KUU iliyochezwa nyumbani kwa Wigan JJB Stadium.
Manchester City wakiwa na Wabrazil wao Robinho, Elano na Jo walishindwa kufurukuta kwa timu ya Wigan iliyocheza nguvu kazi tangu dakika ya kwanza hadi mwisho huku Mshambuliaji wao toka Misri Amr Zaki bila shaka ndie Mchezaji Bora wa mechi.
Wigan walitangulia kupata bao la kwanza kupitia kwa Valencia aliefunga kwa shuti murua na Manchester City wakasawazisha kibahati baada ya mpira kumbabatiza beki wao Kompany na kutikisa nyavu kufuatia frikiki.
Lakini Amr Zaki aliwafungia Wigan bao la ushindi kwa penalti baada ya Palacios wa Wigan kuchezewa rafu na Javier Garrido wa Manchester City.
Kipindi cha pili ingawa mechi ilichangamka sana hakuna mabao mengine yaliyopatikana.
Sasa kibarua kinazidi kuwa kigumu kwa Meneja wa Tottenham kutoka Spain Juande Ramos baada ya Tottenham kupata kipigo kingine kwenye LIGI KUU leo walipofungwa 2-0 na Portsmouth kwenye Uwanja wa Portsmouth Fratton Park.
Tottenham ndio wameshika mkia kwenye msimamo wa LIGI KUU wakiwa na pointi mbili tu katika mechi 6 walizocheza.
Mabao yaliyowaua Tottenham yalifungwa na Jermaine Defoe na Peter Crouch. Ingawa Portsmouth walimaliza mechi wakiwa 10 baada ya Kiungo wao Lassana Diara kupata kadi mbili za njano na hivyo kutolewa kwa kadi nyekundu Tottenham walionyesha dhahiri hawana ubavu wowote.
Portsmouth: James, Johnson, Campbell, Distin, Belhadj, Little, Diarra, Hughes, Armand Traore, Crouch, Defoe. AKIBA: Ashdown, Kaboul, Hreidarsson, Pamarot, Utaka, Mvuemba, Kanu.
Tottenham: Gomes, Corluka, Dawson, Woodgate, Assou-Ekotto, Bentley, Jenas, Zokora, O'Hara, Gilberto, Pavlyuchenko. AKIBA: Cesar, Huddlestone, Lennon, Bent, Modric, Gunter, Giovani.
REFA: Mike Dean (Wirral).