

Timu za Taifa za Nchi za Marekani Kusini zinaingia tena dimbani kuanzia Jumamosi hii katika mapambano ya Kundi lao ambalo lina Nchi 10. Mpaka sasa kila Nchi ishacheza mechi 8 na ikifika Jumatano ya tarehe 15 Oktoba 2008 watakuwa wameshavuka nusu ya mechi wanazotakiwa kucheza na hivyo kuleta picha kidogo nani anaweza akaingia FAINALI huko AFRIKA KUSINI mwaka 2010.
Baada ya mechi 8 kwa kila timu, Paraguay yuko kileleni akiwa na pointi 17 akifuatiwa na Brazil mwenye pointi 13 sawa na Argentina na Chile lakini Brazil yuko mbele kwa kufunga magoli mengi. Uruguay ana pointi 12, Colombia 10, Ecuador 9, Venezuela na Peru wana 7 kila mmoja na mkiani yuko Bolivia mwenye 5.
Timu nne za juu za Kundi hili zitaingia moja kwa moja FAINALI huko AFRiKA KUSINI mwaka 2010.