Monday 6 October 2008

KOMBE LA DUNIA: MECHI ZA MAKUNDI YA ULAYA

Timu za Mataifa ya Ulaya siku ya Jumamosi tarehe 11 Oktoba na Jumatano tarehe 15 Oktoba 2008 zitajimwaga viwanja mbalimbali katika mechi za Makundi ya Nchi za Ulaya kuwania nafasi za kuingia Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika huko Afrika Kusini mwaka 2010.
Nchi hizi za Ulaya zimegawanywa Makundi 9 na bingwa wa kila Kundi anaingia moja kwa moja Fainali hizo. Washindi wa pili Wanane Bora kutoka kwenye Makundi hayo 9 watagawanywa mechi 4 za mtoano za nyumbani na ugenini ili kupata timu nyingine nne zitakazoenda Fainali.
Uingereza ambayo ipo Kundi la 6 pamoja na Croatia, Ukraine, Belarus, Kazakhstan na Andorra inaongoza Kundi hilo ikiwa na pointi 6 baada ya kushinda mechi zake mbili za kwanza ilipozifunga Andorra 2-0 na Croatia 4-1.
Uingereza Jumamosi inacheza na Kazakhstan Uwanja wa nyumbani Wembley na Jumatano watakuwa ugenini kupambana na Belarus.

RATIBA: Jumamosi, 11 Oktoba 2008 [saa zilizotajwa ni zabongo]

Belgium v Armenia, [Kundi la 5, saa 3:45]

Bulgaria v Italy, Kundi la 8, saa 3:15]

Denmark v Malta, [Kundi la 1, saa 3:15]

England v Kazakhstan, Kundi la 6, saa 1:15]

Estonia v Spain, [Kundi la 5, saa 3:45]

Faroe Islands v Austria, [Kundi la 7, saa 12:00]

Finland v Azerbaijan, [Kundi la 4, saa 11:00]

Georgia v Cyprus, [Kundi la 8, saa 1:30]

Germany v Russia, [Kundi la 4, saa 3:45]

Greece v Moldova, [Kundi la 2, saa 3:30]

Holland v Iceland, [Kundi la 9, saa 3:45]

Hungary v Albania, [Kundi la 1, saa 2:45]

Luxembourg v Israel, [Kundi la 2, saa 3:15]

Poland v Czech Republic, [Kundi la 3, 1saa 3:30]

Romania v France, [Kundi la 7, saa 2:15]

San Marino v Slovakia, [Kundi la 3, saa 3:30]

Scotland v Norway, [Kundi la 9, saa 11:00]

Serbia v Lithuania, [Kundi la 7, saa 3:15]

Slovenia v Northern Ireland, [Kundi la 3, saa 3:45]

Sweden v Portugal, [Kundi la 1, saa 3:00]

Switzerland v Latvia, [Kundi la 2, saa 12:45]

Turkey v Bosnia-Herzegovina, [Kundi la 5, saa 3:00]

Ukraine v Croatia, [Kundi la 6, saa 4:00]

Wales v Liechtenstein, [Kundi la 4, saa 1:30]

No comments:

Powered By Blogger