Monday 6 October 2008

Michael Owen kaachwa tena Timu ya Taifa ya England!!

Meneja wa England Fabio Capello hakumchagua Michael Owen kwenye kikosi chake cha Wachezaji 23 wa Timu ya Taifa ya England kitakachocheza mechi za mtoano za Kundi la 6 la Nchi za Ulaya ambalo lina timu za Croatia, Ukraine, Belarus, Kazakhstan na Andorra.
Wengi walitegemea Owen ataitwa baada ya kupona lakini ameachwa na badala yake Peter Crouch amechukuliwa.
England Jumamosi inayokuja tarehe 11 Oktoba inacheza na Kazakhstan Uwanja wa nyumbani Wembley na Jumatano tarehe 15 Oktoba 2008 watakuwa ugenini kupambana na Belarus.

Kikosi kamili cha England [kwenye mabano Klabu wanazochezea]:

James (Portsmouth), Green (West Ham), Carson (West Brom); Brown (Manchester United), Johnson (Portsmouth), Terry (Chelsea), Ferdinand (Manchester United), Lescott (Everton), Upson (West Ham), A Cole (Chelsea), Bridge (Chelsea); Beckham (Los Angeles Galaxy), Walcott (Arsenal), Barry (Aston Villa), Jenas (Tottenham), Lampard (Chelsea), Gerrard (Liverpool), Downing (Middlesbrough), Wright-Phillips (Manchester City); Heskey (Wigan), Crouch (Portsmouth), Rooney (Manchester United), Defoe (Portsmouth).

No comments:

Powered By Blogger