

John Terry hakufanya mazoezi ya Timu ya England hapo jana na nafasi yake kwenye mechi hiyo huenda ikachukuliwa na mmoja kati ya Matthew Upson, Wes Brown au Joleon Lescott.
Endapo hatocheza basi Unahodha wakati wa mechi utachukuliwa na Rio Ferdinand ambae ni Naibu Nahodha wa England.
FLETCHER ATEULIWA NAHODHA SCOTLAND

Darren Fletcher amechukua nafasi ya Nahodha wa siku zote Barry Ferguson ambae ameumia enka na Naibu wake Stephen McManus amefungiwa mechi kwa kuwa na adhabu ya kadi.
Darren Fletcher, mwenye umri wa miaka 24, ni mara ya nne kuteuliwa kuwa Nahodha wa Nchi yake Scotland.
No comments:
Post a Comment