Monday 6 October 2008


UEFA KUFANYA DRO YA UEFA CUP KESHO

Klabu za Uingereza Tottenham, Manchester City, Portsmouth na Aston Villa kesho zitajua ni wapinzani gani watakuwa nao kwenye Makundi ya kugombea Kombe la UEFA [UEFA CUP]. Kwa taratibu za UEFA CUP timu za nchi moja haziwezi kuwekwa kwenye Kundi moja hivyo timu hizi za Uingereza haziwezi kukutana kwenye hatua hii ya Makundi.
Klabu 40 za Ulaya zimegawanywa katika Vikapu vitano na dro itafanyika ili kupata Makundi manane ya timu 5 kila moja. Katika kila Kundi timu moja itacheza mechi 2 nyumbani na 2 ugenini na wapinzani tofauti.
Timu 3 za juu za kila Kundi zitaingia hatua inayofuata ya mtoano itakayojumuisha timu 8 zitakazochukua nafasi ya tatu katika Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

VIKAPU VYA DRO VIMEGAWANYWA IFUATAVYO:

KAPU LA 1: AC Milan, Sevilla, Valencia, Benfica, Schalke 04, CSKA Moscow, TOTTENHAM, Hamburg.

KAPU LA 2: VfB Stuttgart, Ajax, Olympiacos, Deportivo La Coruna, Club Brugge, Spartak Moscow, Paris SG, Heerenveen.

KAPU LA 3: Rosenborg, Udinese, Feyenoord, SC Braga, Slavia Prague, MANCHESTER CITY, Galatasaray, Sampdoria.

KAPU LA 4: Hertha Berlin, Partizan Belgrade, Nancy, PORTSMOUTH, ASTON VILLA, Racing Santander, FC Copenhagen, Dinamo Zagreb.

KAPU LA 5: Saint-Etienne, VfL Wolfsburg, Standard Liege, FC Twente, NEC Nijmegen, Metalist

No comments:

Powered By Blogger