Saturday 1 August 2009

Torres: “England ni bora!”
Straika wa Liverpool kutoka Spain, Fernando Torres, amesisitiza kuwa katika uliwengu wa soka England ni bora na Ligi Kuu ndio ligi bora duniani.
Alipoambiwa kuwa kufuatia jinsi vigogo wa Spain, Real Madrid na Barcelona, walivyopapia kununua Wachezaji inaelekea sasa La Liga ndio itatawala, Torres alibisha na kusisitiza bado England ni bora.
Torres alitamka: “Soka ya England ina wafuasi wengi sana dunia nzima! Na hilo si kwa ajili ya Wachezaji tu bali ni kwa sababu ya historia, utamaduni, uwazi na uaminifu, na pia jinsi Viwanja vinavyofurika watu!”
Robinho alimbembeleza Hughes Elano asiuzwe!
Robinho ametoboa kuwa alikwenda kumsihi Meneja wake wa Manchester City, Mark Hughes, asimuuze Mchezaji mwenzake kutoka Brazil, Elano.
Man City imemuuza Elano kwa Klabu ya Uturuki Galataaray kwa Pauni Milioni 8.
Robinho alisema kwa majonzi: “Imenisikitisha sana! Alikuwa mwenzangu na rafiki mkubwa! Namuombea mema kwa Klabu yake mpya.”
Mido arudi kwao Misri!!
Mido amehama Klabu yake Middlesbrough iliyoshuhwa Daraja kutoka Ligi Kuu England na kurudia kwao kwenye Klabu ya Zamalek alikoanzia kucheza soka.
Zamalek imeilipa Boro Pauni Milioni 4 ili Mido acheze huko kwa mkopo kwa msimu mmoja na itawabidi waongeza Pauni Milioni 1 zaidi ikiwa watataka kumchukua moja kwa moja.
Baada ya Boro kushushwa Daraja, Mido, umri miaka 26, aligoma kurudi kuichezea Timu hiyo.
Mido huko nyuma amewahi kuzichezea Klabu za Gent, Ajax, Celta Vigo, Marseille, na Wigan katika kipindi cha miaka 9 iliyopita.
Mido alitimuliwa kwenye Kikosi cha Timu ya Taifa ya Misri baada ya kuzozana na Kocha wa Misri Hassan Shehata alipoamuliwa kutoka uwanjani ili aingizwe Mchezaji mwingine katika mechi ya Nusu Fainali ya kugombea Kombe la Mtaifa ya Afrika mwaka 2006 dhidi ya Senegal.
KOMBE LA EMIRATES: Kuanza leo Nyumbani kwa Arsenal!
Leo jioni, Timu za Arsenal, Glasgow Rangers kutoka Scotland, Paris Saint-Germain [PSG] kutoka Ufaransa na Atletico de Madrid ya Spain zitashuka Uwanja wa Emirates kugombea Kombe la Emirates ikiwa ni maandalizi ya Timu hizo kwa msimu mpya utakaoanza hivi karibuni.
RATIBA: [saa za bongo]
Jumamosi, Agosti 1
Saa 10 jioni: Rangers v PSG
Saa 12 na dak 15 jioni: Arsenal v Attletico
Jumapili, Agosti 2:
Saa 10 jioni: Atletico v PSG
Saa 12 na dak 15 jioni: Arsenal v Rangers
Wolfsburg wakamilisha uhamisho wa Martins!
Mabingwa wa Ujerumani Wolfsburg wametangaza rasmi kuwa Obafemi Martins amesaini mkataba wa miaka minne kwa dau la Pauni Milioni 9.
Martins, anaetoka Nigeria, amekuwa akicheza Newcastle Timu iliyoporomoka Daraja kutoka Ligi Kuu England, tangu atoke Inter Milan mwaka 2006.
Ferguson kubadili mbinu Man U
Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amekiri kuwa inabidi abadilishe mbinu za uchezaji baada ya Mfungaji wao mkuu kwa misimu miwili iliyopita Cristiano Ronaldo kuondoka.
Ferguson amekiri: “Ni pigo kuu Cristiano kuondoka. Inabidi tutafute magoli kwa njia nyingine. Mbinu zitabadilika.”
Msimu uliokwisha Ronaldo alifunga goli 26, Berbatov 14 na Rooney 13.
Ferguson aliongeza: “Huko nyuma, Scholes, Giggs na Beckham kila mmoja alikuwa akifunga mabao 10. Lakini siki hizi magoli toka kwa Viungo wetu yamekauka. Inabidi tushughulike hilo. Pia itabidi kina Park, Nani, Valencia, Welbeck na Macheda wafunge jumla ya goli 40 kati yao!"
Mutu ashindwa rufaa kupinga kulipa Mamilioni!
Adrian Mutu inabidi ailipe Chelsea Pauni Milioni 4.65 baada ya kushindwa rufaa yake iliyopinga uamuzi wa FIFA wa kumtaka alipe kiasi hicho kwa Chelsea ikiwa ni fidia ya kukiuka mkataba.
Mshambuliaji huyo kutoka Rumania alieigharimu Chelsea Pauni Milioni 15 mwaka 2003 alifukuzwa Chelsea mwaka mmoja baadae baada ya kugundulika anatumia cocaine na kufungiwa miezi 7 kutocheza soka.
FIFA iliamua Mutu ailipe Chelsea pesa hizo zikiwa ni fidia lakini Mutu alikata rufaa kupinga uamuzi huo kwa Korti ya Masuala ya Michezo [CAS= Court of Arbitration for Sport].

Baada ya kutimuliwa Chelsea, Mutu alijiunga na Juventus Januari 2005 na msimu mmoja baadae akaenda Fiorentina ambako yuko mpaka leo.
Spurs yatwaa Kombe la Asia: Spurs 3 Hull 0
Tottenham Hotspurs, wakicheza Beijing, wameifunga Hull City mabao 3-0 na kushinda Kombe la Asia.
Mabao ya Spurs yalifungwa na Robby Keane, mawili, na Aaron Lennon bao moja.
Sir Bobby Robson afariki!
Meneja wa zamani wa England, Newcastle na Ipswich Town, Sir Bobby Robson, miaka 76, amefariki dunia.
Robson, aliewahi pia kuwa Kocha wa Klabu za PSV Eindhoven, Sporting Lisbon, Porto na Barcelona, amekuwa akisumbuliwa na kansa.
Mwaka 1990 aliifikisha England Nusu Fainali ya kombe la Dunia huko Italia lakini ikakosa kuingia Fainali baada ya kubwagwa kwa penalti na Ujerumani.
Roy Keane aipeleka Ipswich Town Kambi ya Jeshi kupata mafunzo ya kijeshi kuongeza nguvu!
Roy Keane, ambae sasa ni Meneja wa Ipswich Town Timu ambayo ipo Daraja la chini tu ya Ligi Kuu England na ambae ndio kwanza tu anaanza kazi hiyo na timu hiyo, ameipeleka Timu yake hiyo mpya kwenye Kambi ya Kijeshi ya Jeshi la Uingereza kupata mafunzo ya kijeshi ili kujenga stamina na kuongeza nguvu zaidi.
FK Vetra 0-3 Fulham
Wakicheza mechi yao ya kwanza ugenini kwenye Kombe jipya la EUROPA LEAGUE, Fulham wameishinda FK Vetra bao 3-0 huko Lithuania.

Timu hizi ztarudiana mjini London wiki ijayo Uwanja wa Craven Cottage nyumbani kwa Fulham.
Timu nyingine za Ligi Kuu zinazocheza EUROPA LEAGUE ni Aston Villa na Everton ambazo zitaanza kushirikishwa raundi ijayo kwani zilimaliza Ligi nafasi ya 5 na ya 6.

Fulham ilimaliza nafasi ya 7.

Friday 31 July 2009

Bayern Munich washinda kwao AUDI CUP kwa matuta
Bayern Munich ikicheza Allianz Arena, ngome yao, walitwaa Kombe la AUDI baada ya kuibwaga Manchester United kwa penalti baada ya mechi kumalizika suluhu 0-0.

Thursday 30 July 2009

FIFA: VUVUZELA RUKSA FAINALI KOMBE LA DUNIA 2010 HUKO BONDENI!!!!
FIFA imethibitisha kuwa Vuvuzela, zile tarumbeta za plastki za kila rangi ambazo Mashabiki wa Afrika Kusini ni utamaduni wao kuingia nazo uwanjani na kuzipuliza zikitoa sauti mithili ya Kundi la Tembo linalofanya uvamizi, zitaruhusiwa kwenye mechi za Fainali za Kombe la Dunia mwakani huko Afrika Kusini.
Vuvuzela lilipata umaarufu maradufu hivi karibuni wakati wa Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara la huko Afrika Kusi lililobebwa na Brazil huku baadhi ya Timu, hasa Spain, kudai linaudhi na ndilo lililowafanya wakose kushinda.
FIFA wamesema Vuvuzela ni ruksa labda ibainike ni hatari kwa usalama wa watu.

Alonso aomba rasmi uhamisho!
Kiungo wa Liverpool Xabi Alonso, miaka 27, hatimae amewasilisha maombi rasmi ya kutaka kuhama Klabu yake na kwenda Real Madrid.
Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Spain ameng’ang’ania kuhama baada ya kuudhiwa na kitendo cha Liverpool kutaka kumuuza msimu uliokwisha ili wamchukue Gareth Barry wa Aston Villa wakati huo.
Barry hivi majuzi amehamia Manchester City.
Ingawa Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, amekuwa akisema Alonso hauzwi inaaminika kuhama kwa Alonso kupo ikiwa tu Klabu hizo mbili zitaafikiana dau lake huku Liverpool wakitaka Pauni Milioni 30 na Real wako tayari kutoa Pauni Milioni 25.
Taarifa hizi zimeendelea kudai kuwa kwa sababu sasa Alonso ameshatoa msimamo wake kimaandishi basi Liverpool watalazimika kumuuza.
Alonso alinunuliwa na Liverpool mwaka 2004 na kwa Pauni Milioni 10.5.
Wenger haingii sokoni licha ya kuwauza Ade na Kolo!!!
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ametoboa kuwa hatoenda sokoni kwa kiwewe cha kuwakosa Adebayor na Kolo Toure ambao wamenunuliwa na Manchester City.
Kuna baadhi ya Wadau wa Soka wa Arsenal wamemlaumu sana Wenger kwa kuruhusu kuuzwa kwa Wachezaji hao ambao Wadau hao wanaamini ni nguzo kubwa kwa Klabu hiyo.
Mpaka sasa Wenger amenunua Mchezaji mmoja ambae ni Mlinzi Thomas Vermaelen kutoka Ajax.
Hata hivyo kuna habari ambazo zimeanza kuota mizizi kuwa Nahodha wao wa zamani Patrick Viera anataka kurudi Arsenal akitoka Inter Milan.
Elano ahamia Galatasaray
Galatasaray ya Uturuki imekamilisha taratibu za kumchukua Kiungo wa Brazil, Elano, miaka 28, anaecheza Manchester City kwa mkataba wa miaka minne.
Elano alisainiwa na Man City mwaka 2007 kwa dau la Pauni Milioni 8 kutoka Klabu ya Ukraine Shakhtar Donetsk na ameichezea Man City mechi 80 na kufunga mabao 18.
Mpaka sasa Man City ishawachukua Washambuliaji Roque Santa Cruz, Carlos Tevez na Emmanuel Adebayor, Kiungo Gareth Barry na Mlinzi Kolo Toure.
Jitihada zao za kuwabeba Walinzi John Terry kutoka Chelsea na Joleon Lescott kutoka Everton mpaka sasa zimepiga mwamba baada ya Klabu zao kugoma kumuuza.
AUDI CUP: Fainali Bayern v Man U!!
Bayern yaitandika AC Milan 4-1!!
Wenyeji Bayern Munich wakicheza Uwanja wa nyumbani Allianz Arena mjini Munich jana waliikung’uta AC Milan mabao 4-1 na leo watakutana na Manchester United kwenye Fainali ya Kombe la Audi.
Man U jana waliitoa Boca Juniors bao 2-1.
AC Milan leo watacheza na Boca kutafuta mshindi wa tatu.
Mabao ya Bayern Munich yalifungwa na Thomas Muller, bao 2, Schweinsteger na Sene bao 1.

Bao la AC Milan lilipachikwa na Andreas Pirlo.
MATOKEO UEFA CHAMPIONS LEAGUE: MECHI ZA MCHUJO JANA:
Apoel Nicosia 2 v Partizan Belgrade 0,
Celtic 0 v Dinamo Moscow 1,
FC Copenhagen 3 v Stabaek 1,
FC Levadia Tallinn 0 v Debreceni VSC 1,
FC Sheriff Tiraspol 0 v Slavia Prague 0,
FC Zurich 2 v NK Maribor 3,
FK Ventspils 1 v BATE Borisov 0,
Shakhtar Donetsk 2 v FCU Politehnica Timisoara 2,
Slovan Bratislava 0 v Olympiacos 2,
Sporting 0 v FC Twente 0,
MECHI YA KIRAFIKI:
Hannover 0 Arsenal 1
Obafemi Martins kwenda Wolfsburg?
Habari ambazo hazijathibitishwa na Newcastle zimesema Mshambuliaji kutoka Nigeria Obafemi Martins yuko mbioni kuihama Timu hiyo iliyoporomoka Daraja kutoka Ligi Kuu na kujiunga na Mabingwa wa Ujerumani Klabu ya Wolfsburg.
Imeelezwa Newcastle wameikubali ofa ya Wolfsburg ya Pauni Milioni 9.

Wednesday 29 July 2009

MAN U 2 BOCA 1
Manchester United wakicheza mjini Munich Uwanja uitwao Allianz Arena wamewafunga magwiji wa Marekani ya Kusini Boca Juniors ya Argentina mabao 2-1 na kuingia Fainali ya Kombe la Audi.
Man U wanasubiri mshindi kati ya Bayern Munich au AC Milan watakaocheza leo.
Alikuwa ni Anderson alieipatia Man U bao la kwanza, hilo likiwa bao lake la kwanza kabisa kuifungia Man U [ukitoa la penalti Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE dhidi ya Chelsea] na alilifunga dakika ya 22 kwa frikiki nzuri sana.
Nae Luis Antonio Valencia, akicheza mechi yake ya kwanza kwa Man U, alifunga bao la pili dakika ya 41 na hilo likiwa pia bao lake la kwanza kwa Man U.
VIKOSI VILIKUWA:
Boca Juniors: Abbondanzieri; Soto, Lopez, Forlin; Diaz (Chavez 46), Battaglia, Riquelme (Marino 88), Insua (Gaitan 67), Lopez; Noir (Mouche 46), Palermo (Viatri 81).Akiba hawakucheza: Garcia (GK), Gunino, Krupoviesa, Philippe, Monzon.

Manchester United: Kuszczak; O'Shea, Cathcart, Brown (Ferdinand 37), Fabio (Evra 77); Valencia (Nani 68), Anderson (Fletcher 77), Carrick (Scholes 77), Park (Giggs 68); Rooney, Macheda (Berbatov 68).Akiba hawakucheza: Foster, Tosic, Vidic, Evans, Gibson.
UZI MPYA WA MAN U MECHI ZA UGENINI WAANIKWA!!
Mabingwa Manchester United wameuonyesha uzi wao mpya watakaoutumia kucheza mechi za ugenini za msimu wa 2009/10.
Jezi hizo ni za rangi nyeusi zikiwa na mstari wa v kifuani, bukta na stokingi pia ni nyeusi.
Man U watazivaa Jezi hizo kwa mara ya kwanza kesho huko Ujerumani watakapocheza na Bayern Munich au AC Milan kwenye Kombe la Audi.
Mechi hiyo ya kesho itakuwa ni ama Fainali ya Kombe hilo au mechi ya kutafuta mshindi wa tatu yote yakitegemea matokeo ya mechi za leo wakati ni Man U v Boca Juniors na Bayern Munich v AC Milan.
Kolo Toure aafikiana na Man City!
Kolo Toure amefikia makubaliano na Klabu ya Manchester City kuhusu maslahi yake na sasa atapimwa afya ili kukamilisha uhamisho wake kutoka Arsenal kwa dau linaloaminika ni zaidi ya Pauni Milioni 15.
Toure amekuwa akiichezea Arsenal tangu mwaka 2002 wakati Arsene Wenger alipomtoa kwao Ivory Coast kwa dau dogo sana.
Inaaminika Toure amesaini mkataba wa miaka minne na yeye atakuwa Mchezaji wa pili wa Arsenal kuhamia Man City baada ya Emmanuel Adebayor kuhamia huko hivi karibuni.
Liverpool wathibitisha Arbeloa kauzwa Real!!!
Liverpool imetoa uthibitisho kwamba wamefikia makubaliano na Real Madrid ili Beki wao Alvaro Arbeloa ahamie Real Madrid.
Uhamisho huo utaigharimu Real Pauni Milioni 3 na nusu na inasemekana Arbeloa atasaini mkataba wa miaka mitano.
Arbeloa alianza uchezaji wake wa soka Real Madrid na kisha kuhamia Deportivo La Coruna na baadae Liverpool.
KOMBE LA ASIA: Tottenham waitungua West Ham na kutinga Fainali! Hull City watinga Fainali kwa matuta!!
Wakicheza vizuri sana, leo huko Beijing, Uchina, Tottenham wamewatundika wenzao wa Ligi Kuu England West Ham bao 1-0 bao lililofungwa na Jermain Defoe dakika ya 75.
Mechi hiyo iliingia dosari baada ya Mchezaji wa West Ham Luis Boa Morte kuumia goti na taarifa zimesema huenda akawa nje ya Uwanja kwa muda mrefu.
Katika mechi iliyofuata, Hull City walitoka sare na wenyeji wao Beijing Guoan bao 1-1 na ndipo zikapigwa penalti tano na ngoma ikawa tena droo baada ya kila Timu kukosa moja.
Lakini Hull City wakaibuka kidedea baada ya kufunga penalti yao ya 6 na Beijing Guoan kupaisha ya kwao.
Sasa Fainali ni kati ya Tottenham na Hull City.
Kurudi Hargreaves uwanjani kuna utata!!!
Kiungo wa Manchester United Owen Hargreaves ambae yuko nje ya uwanja tangu mwaka jana Septemba kwa matatizo ya magoti yake yaliyomlazimu kufanyiwa upasuaji kila goti lake huko Marekani huenda akalazimika kuwa nje ya uwanja kwa muda zaidi baada ya kuambiwa na Madaktari bado inabidi aendele na tiba huko huko Marekani.
Akiongea huko Ujerumani ambako Manchester United leo wanapambana na Boca Juniors ya Argentina katika mashindano ya Audi Cup, Sir Alex Ferguson amesema: ‘Tulitegemea atakuja hapa Ujerumani kuungana na sisi lakini imeonekana bora aendelee na matibabu zaidi huko Marekani.’
Kombe la AUDI Ujerumani: Makocha wa Klabu zinazoshiriki waikandya Real Madrid!
Kombe la Audi ili kusherehekea miaka 100 ya Kampuni ya kutengeneza magari aina ya Audi linaanza kushindaniwa leo huko Ujerumani na washiriki ni Klabu za Boca Juniors kutoka Argentina, Klabu za Ulaya wenyeji Bayern Munich, AC Milan na Manchester United.

Jana kwenye mahojiano ya pamoja na Waandishi wa Habari, Makocha wa Timu 3 Wakongwe wa Ulaya wote kwa pamoja waliishambulia Real Madrid kwa msimamo wao wa kununua Wachezaji kwa bei mbaya na wote walionyesha kushangazwa na kutojua jinsi Timu itakavyopangwa kwani mpaka sasa Timu hiyo haina Walinzi wazuri na hivyo itakosa uwiano kiwanjani.
Makocha wa Manchester United na AC Milan, Sir Alex Ferguson na Leonardo, wote wamewapoteza Wachezaji wao nyota, Ronaldo na Kaka, waliokimbilia Real kwa kitita cha kustusha. Kocha wa Bayern Munich, Louis van Gaal, mpaka sasa anapigana nyota wake Franck Ribery asikimbilie Real Madrid.
Ferguson alisema Real Madrid itakuwa haina uwiano Uwanjani na hata alimtahadharisha Ronaldo kuwa itakuwa si ajabu kama akiishia kucheza Sentahafu Klabuni hapo! Ferguson aliongeza tofauti na Real, Barcelona wamekuwa wakijenga Timu polepole kwa kununua Mchezaji mmoja au wawili kila msimu.
Ferguson alitamka: ‘Kuna mfano mzuri huko England katika miaka ya nyuma Sunderland ilitumia pesa nyingi kununua Wachezaji na ikabatizwa jina Benki ya England! Hawakufanikiwa na matokeo yake wakashushwa Daraja! Sisemi Real watashuka ila watapata matatizo upangaji Timu!’
Mameneja wenzake wakamuunga mkono Ferguson na Van Gaal akasema kuwa kuna Makocha, kama Ferguson na yeye, wanaweza kuunda Timu upya lakini hadhani Real itakuwa tishio kwa sababu timu inajengwa na si kununuliwa!
Nae Leonardo, ingawa alikubali Real wana uzito kifedha, aliwakumbusha watu kuwa wakati Real ilipokuwa na ‘Galactico’ [vizito] Zidane, Figo na Beckham timu ilipoteza mwelekeo kadiri ‘vizito’ wengine walipoongezwa na akasisitiza ni vigumu kuwamiliki Masupastaa wote kama Kaka, Ronaldo na Benzema katika timu moja.
MATOKEO UEFA CHAMPIONS LEAGUE: RAUNDI ZA MCHUJO
Jumanne, 28 Julai 2009
Anderlecht 5 v Sivasspor 0
FC Aktobe 0 v Maccabi Haifa 0
FK Baku 0 v Levski Sofia 0
Sparta Prague 3 v Panathinaikos 1
RATIBA LEO:
-KOMBE LA ASIA:
West Ham v Tottenham
Hull City v Beijing Guoan
-MECHI YA KIRAFIKI:
Hannoverscher v Arsenal

Tuesday 28 July 2009


UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Raundi ya Mchujo ni leo na kesho!
Yale mashindano ambayo hungojewa na wengi kwa hamu, yaani Klabu Bingwa Barani Ulaya maarufu kwa jina la UEFA CHAMPIONS LEAGUE, kwa sasa yapo hatua za mchujo ili kupata Timu zitazobakia na kuingizwa kwenye dro ya kupanga Makundi yatakayocheza kwa mtindo wa ligi kwa mechi za nyumbani na ugenini.
Mechi za leo na kesho ni kama ifuatavywo:
Jumanne, 28 Julai 2009
Anderlecht v Sivasspor,
FC Aktobe v Maccabi Haifa,
FK Baku v Levski Sofia,
Sparta Prague v Panathinaikos,
Jumatano, 29 Julai 2009
Apoel Nicosia v Partizan Belgrade,
Celtic v Dinamo Moscow,
FC Copenhagen v Stabaek,
FC Levadia Tallinn v Debreceni VSC,
FC Sheriff Tiraspol v Slavia Prague,
FC Zurich v NK Maribor,
FK Ventspils v BATE Borisov,
Shakhtar Donetsk v FCU Politehnica Timisoara,
Slovan Bratislava v Olympiacos,
Sporting v FC Twente,
AUDI CUP KESHO HUKO UJERUMANI: Man U v Boca Juniors na Bayern Munich v AC Milan
Kesho huko Ujerumani saa moja na nusu usiku saa za bongo, Manchester United wanashuka dimbani kupambana na vigogo wa Marekani ya Kusini, Boca Juniors kutoka Argentina, kwenye pambano la kwanza kugombea Kombe la Audi na mechi hiyo itafuatiwa na ile ya Wenyeji Bayern Munich kucheza na AC Milan ya Italy.
Washindi wa mechi hizo watakutana Fainali Alhamisi saa 3 dakika 45 usiku mechi itakayotanguliwa na ile ya kutafuta Mshindi wa Tatu ambayo itachezwa baina ya timu zitakazofungwa kesho.
Uhamisho wapamba moto: Crouch katua Spurs, Ibrahimovic na Eto’o wabadilishana Klabu, Toure kuhama Arsenal kumfuata Adebayor?
Tottenham imemsaini Fowadi wa England Peter Crouch, miaka 28, kutoka Portsmouth kwa dau la Pauni Milioni 9.
Sasa anajumuika tena na Meneja Harry Redknapp ambae alikuwa Portsmouth kabla ya kuhamia Tottenham.
Nae Mchezaji wa Kimataifa wa Sweden Zlatan Ibrahimovic amesaini mkataba wa miaka mitano na Barcelona akitokea Inter Milan alipokaa miaka mitatu na ambapo Barca wamelipa dau la Euro Milioni 45 pamoja na kumtoa Samuel Eto’oo kuhamia Inter na pia kuruhusu Alexander Hleb kucheza Inter kwa mkopo ikiwa ni makubaliano kati ya Klabu hizo mbili.
Wakati huo huo, Manchester City wako karibu sana kumsaini Mlinzi wa Arsenal Kolo Toure, umri miaka 28, kwa dau la Pauni Milioni 15.
Toure aliichezea Arsenal jana usiku huko Hungary kwenye mechi ya kirafiki na habari hizi za uhamisho pia ziliguswa na Arsene Wenger alietamka: ‘Tuataangalia nini kitatokea katika masaa 24 yajayo. Bado hamna kitu kilichokamilika. Tunao Msentahafu 7 ingawa Kolo ni Mchezaji mzuri.’

Sunday 26 July 2009

Celtic wabeba Kombe la Wembley!
Klabu ya Scotland, Celtic, leo imebeba Kombe la Wembley walipoifunga Tottenham bao 2-0 magoli yote yakipatikana kipindi cha kwanza na kufungwa na Chris Killen, dakika ya 9, na Georgios Samaras, dakika ya 40.
Katika mechi ya kwanza Celtic iliibamiza El Ahly ya Misri mabao 5-0.
Tottenham walitoka suluhu na Barcelona 1-1
Man City wadodondoshwa Bondeni!
Manchester City wamemaliza ziara yao huko Afrika Kusini kwa kufungwa mechi ya pili kati ya tatu walizocheza na jana walipigwa bao 1-0 na Kaizer Chiefs kwa bao la utata baada ya mfungaji wa Kaizer Chiefs Jeffrey Ntuka kuumiliki mpira kwa mkono na kisha kufunga katika dakika ya 42.

Emmanuel Adebayor jana alicheza mechi yake ya kwanza akivaa Jezi ya Bluu ya Man City na akaikosesha bao la wazi dakika ya 55 alipofumua shuti juu ya posti.
Terry kubaki Chelsea!!
Nahodha wa Chelsea na England, John Terry, amewakata maini Manchester City kwa kuibuka na kutamka waziwazi kuwa yeye anabaki Chelsea.
Wiki za hivi karibuni kumekuwa na mazungumzo mazito kwamba Terry atakwenda Man City kwa kitita cha zaidi ya Pauni Milioni 40 habari zilizopamba moto hasa kutokana na ukimya wa Terry mwenyewe ingawa Klabu yake Chelsea ilikataa moja kwa moja kuwa Mchezaji huyo hauzwi.
Leo Terry ametamka: ‘Mimi nipo Chelsea kwa moyo wangu wote, kwa siku zote! Kuhama? Haiwezekani!’
Pengine msimamo wa Terry ni habari murua kwa Chelsea ambayo imekuwa ikyumba kwa zaidi ya miaka miwili sasa huku ikibadilisha Mameneja mara 5 na kushinda Kombe moja tu na nalo ni la FA msimu uliopita.
Mido kuiaga Boro!!
Mchezaji wa Misri, Mido, ambae alitwangwa faini ya Mishahara ya wiki mbili baada ya kuchelewa kuripoti klabuni baada ya likizo, sasa atauzwa kwa Klabu nyingine ambayo imetoa ofa isiyoweza kukataliwa na Middlesbrough kufuatana na Meneja wao Gareth Southgate.
Southgate ametangaza kuwa Boro wameikubali ofa hiyo lakini ni juu ya Mido sasa kuikubali au la na pia kukubaliana na Klabu hiyo ambayo hakuitaja.
Msimu uliokwisha Mido alikuwa akichezea Wigan kwa mkopo na kwa sasa Middlesbrough imeshushwa Daraja kutoka Ligi Kuu na itacheza Coca Cola Championship msimu ujao.
Ferguson: ‘Man City ni Klabu Ndogo!’
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amesema Manchester City ni ‘Klabu ndogo yenye falsafa finyu!’
Kauli hiyo ya Ferguson imefuatia kutundikwa bango kubwa sana katikati ya Jiji la Manchester la rangi ya kibluu, ambayo ndiyo rangi ya Man City, likiwa na picha ya Carlos Tevez na maandishi: ‘Carlos Tevez, karibu Manchester.’
Alipoulizwa, Ferguson nae akahoji: ‘Ni Man City sio? Wao ni Klabu ndogo yenye falsafa finyu! Siku zote hawana la kuongea ila Manchester United! Wanadhani kumchukua Tevez ni ushindi! Ni upuuzi tu!’
Hivi karibuni, Man City wametumia pesa nyingi sana kuwanunua Emmanuel Adebayor kutoka Arsenal kwa Pauni Milioni 25, Gareth Barry kutoka Aston Villa Pauni Milioni 12, Roque Santa Cruz kutoka Blackburn Pauni Milioni 18 na Tevez kwa Pauni Milioni 25.
Ferguson, akiwa China kwenye ziara ya Asia pamoja na Timu yake, pia alidai Adebayor alijaribu ‘kujiuza’ Man U kabla ya kukamilisha usajili Man City.
Ferguson amesema: ‘Mtu akikupa kitita kama cha Man City ni vigumu kukataa! Ndio maana Wachezaji wanaenda huko. Katika dakika za mwisho kabla Adebayor hajasaini Man City, yeye au Wakala wake, walitupigia simu na waliwapigia simu Chelsea! Adebayor alikuwa akihaha kuhamia kwetu au Chelsea!’
Hatimaye Liverpool wapata ushindi wa kwanza mechi za kirafiki!
Leo, Liverpool hatimaye wamepata ushindi wao wa kwanza katika mechi za kirafiki za matayarisho kwa ajili ya msimu mpya waliposhinda huko Singapore kwa kuifunga Timu ya Taifa ya Singapore bao 5-0.
Mabao ya Liverpool yalifungwa na Kijana kutoka Hungary, Krisztian Nemeth, bao 2, Andriy Voronin, Allbert Riera na Fernando Torres.
Kombe la Wembley: Leo Barcelona 4 El Ahly 1, Tottenham v Celtic kucheza baadae leo!
Katika mashindano ya kugombea Kombe la Wembley yanayochezwa mjini London Uwanjani Wembley, El Ahly ya Misri, leo imepata kipigo cha pili, cha kwanza kikiwa 5-0 walichokung’utwa na Celtic ya Scotland siku ya Ijumaa, na leo Barcelona wakawapiga 4-1.
Mechi nyingine ya Kombe hilo ilichezwa Ijumaa wakati Tottenham na Barcelona kutoka suluhu 1-1.
Leo, saa 12 saa za bongo, Tottenham watakumbana na Celtic.
Portsmouth wathibitisha Crouch kwenda Tottenham
Meneja wa Portsmouth, Paul Hart, amethibitisha kuwa Mshambuliaji ‘ngongoti’, Peter Crouch, miaka 28,atanunuliwa na Tottenham Hotspurs baada ya Klabu hizo mbili kufikia makubaliano yanayosadikiwa kuwa ni ada ya Pauni Milioni 10.
Crouch, ambae alianzia kuichezea Tottenham siku za nyuma, amecheza na Portsmouth msimu mmoja tu toka ahamie hapo kutoka Liverpool.
Hangzhou Greentown 2 Man U 8
Manchester United leo wamemaliza ziara yao ya Asia kwa kishindo pale walipopata ushindi wa kishindo baada ya kuwakung’uta wenyeji wao Hangzhou Greentown mabao 8-2.
Mpaka mapumziko, Man U walikuwa mbele mabao 4-0, wafungaji wakiwa Michael Owen, bao 2, Berbatov na Zoran Tosic bao 1 kila mmoja. Kipindi cha pili Ryan Giggs akafunga 3 na Nani akafunga bao
1.
Powered By Blogger