Saturday 13 February 2010

FA Cup: Reading v WBA sare, Birmingham washinda dakika za mwisho!
Birmingham wametinga Robo Fainali ya Kombe la FA kwa goli la ushindi lililofungwa na Liam Ridgewell dakika ya 91 na kuwafanya Birmingham waishinde Derby bao 2-1.
Derby ndio waliopata bao la kwanza dakika ya 55 kupitia McEveley na Birmingham wakarudisha dakika ya 73 mfungaji akiwa Dann.
Na West Bromwich Albion walikuwa nyuma kwa bao 2-1 dhidi ya Reading hadi dakika ya 87 ndipo Mattock akasawazisha na Timu hizi zitarudiana huko Hawthorns, Uwanja wa West Bromwich, hapo Februari 24.
CAF CHAMPIONS LEAGUE: Yanga yadundwa Bongo!!
Leo, katika mechi ya Raundi ya awali kugombea Klabu Bingwa Afrika, Mabingwa wa Bongo, Yanga, wamefungwa 3-2 wakiwa nyumbani na Mabingwa wa Congo DR [ile ya Kabila] FC Saint Eloi Lupopo.
Huko Kenya katika Kombe hilohilo la Klabu Bingwa Afrika, Sofapaka ya Kenya ilitoka sare 0-0 na El Ismaily ya Misri
Capello aweweseka kuhusu Rooney!
Ambembeleza Fergie awe anampumzisha!
Fabio Capello, Meneja wa England, amemwomba Sir Alex Ferguson asimchezeshe Wayne Rooney kila mechi ili apumzike na ikifika Juni kwenye Fainali za Kombe la Dunia awe bado yuko freshi.
Ombi la Capello huenda lisisikilizwe kwa vile Rooney pia ni muhimu sana kwa Manchester United wanaowania kuutwaa Ubingwa wa England kwa mara ya 4 mfululizo, wako Fainali ya Carling watakayocheza na Aston Villa hapo Februari 28 na pia wako Raundi ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na wanacheza mechi mbili na AC Milan katika mtoano huo.
Rooney ndie anaongoza na tegemezi kubwa kwa magoli Manchester United.
Wadau wanahisi ombi la Capello limekuja wakati England ina wasiwasi wa kumpoteza Beki wa kushoto, Ashley Cole, ambae amevunjika enka na imekadiriwa atarudi uwanjani mwezi Mei na kuna hisia muda huo ni mfupi mno kwa Cole kujijenga kuwa fiti tena kwa Fainali za Kombe la Dunia mwezi Juni.
FA Cup: Chelsea, Portsmouth ndani ya Robo Fainali!!
Mabingwa Watetezi wa FA Cup, Chelsea, na Klabu iliyo kwenye msukosuko mkubwa wa kifedha, Portsmouth, leo wametinga Robo Fainali ya Kombe la FA baada ya kuwabwaga wapinzani wao kwa bao 4-1 kila mmoja.
Chelsea wakicheza kwao Stamford Bridge waliitwanga Cardiff City 4-1 kwa bao za Drogba, Ballack, Sturridge na Kalou.
Bao la Cardiff lilifungwa na Michael Chopra.
Portsmouth wakiwa wageni wa Southampton walishinda bao 4-1 huku bao zote za mechi hiyo zikiingia kipindi cha pili.
Portsmouth ndio waliotangulia kwa bao la Owusu-Abeyie lakini Southampton wakasawazisha kupitia Rickie Lambert.
Portsmouth wakaongeza bao 3 zilizofungwa na Arune Dindane, Nadir Belhadj na Jamie O’Hara.
Leo bado kuna mechi nyingine tatu za FA mbili zitaanza baada ya muda si mrefu, Derby v Birmingham na Reading v WBA, na ya tatu, Man City v Stoke, itaanza saa 2 na robo, saa za bongo.
Kadi ya Boateng yafutwa!!
Kiungo wa Hull City, Geoge Boateng, ameondolewa Kadi Nyekundu na hivyo kukwepa kufungiwa mechi 3 baada ya kubandikwa Kadi hiyo na Refa Lee Probert katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa Jumatano huko Ewood Park na wenyeji Blackburn Rovers waliifunga Hull bao 1-0.
Kamisheni Huru ya Nidhamu imeifuta Kadi hiyo ya Boateng aliyopewa baada ya kuridhishwa waligongana vichwa kwa bahati mbaya na Mchezaji wa Blackburn Morten Gamst Pedersen.
Saha anaisapoti, ataka Man United iwe Bingwa!!
Baada ya kuiua Chelsea Jumatano kwa kuiwekea Everton bao 2 toka mguuni kwake na kuipa Everton ushindi wa bao 2-1 na hivyo kuisaidia Klabu yake ya zamani Manchester United kuisogelea Chelsea kwenye msimamo wa Ligi Kuu, Straika Luis Saha amedai Manchester United ndio watakaotwaa Ubingwa msimu huu.
Kabla ya kujiunga na Everton, Saha alikuwa na Manchester United kwa miaka minne lakini muda mwingi alikuwa akijiuguza kwa kuumia mara kwa mara.
Saha ametamka: “Ningefurahi mno kama ningeweza kusema Everton ndie Bingwa lakini hilo haliwezi kutokea! Itakuwa mshikemshike kati ya Chelsea na Man United! Ingawa Chelsea wana nguvu, Ubingwa ni wa Man United kwa vile ni Timu nzuri zaidi! Wakishinda ntafurahi sana!”
Saha ameongeza kwa kusema bado ana mawasiliano ya karibu na Wachezaji wa Manchester United hasa Evra, Rooney na Hargreaves na walimpongeza kwa ushindi wa Jumatano.
Jumamosi ijayo Everton inaikaribisha Manchester United Goodison Park kwenye mechi ya Ligi Kuu.
CAF CHAMPIONS LEAGUE
Leo na kesho ni mechi za Raundi ya awali kugombea Klabu Bingwa Afrika na Mabingwa wa Bongo, Yanga, watakuwa dimbani kucheza na Mabingwa wa Congo DR [ile ya Kabila] FC Saint Eloi Lupopo.
RATIBA KAMILI:
Jumamosi Februari 13
Yanga v Saint Eloi Lupopo [Congo DR]
Sofapa [Kenya] v El Ismaily [Misri]
Gaborone United [Botswana] v Orlando Pirates [Afrika Kusini]
AS Tempete MOCAF [Afrika ya Kati] v Al Ittihad [libya]
Armed Forces [Gambia] v JS Kabyle [Algeria]
OS Balantas [Guinea-Bissau] v Difaa El Jadida [Morocco]
KWINGINEKO ULAYA: Matokeo Ijumaa, Februari 12
BUNDESLIGA
Borussia Moenchengladbach 2 v Nurnberg 1
SERIE A
AC Milan 3 v Udinese 2
Ni mwezi muhimu kwa Man United
-ULAYA: Jumanne Feb 16 v AC Milan [Uwanjani San Siro]
-LIGI KUU: Jumamosi Feb 20 v Everton [Goodison Park]
-LIGI KUU: Jumanne Feb 23 v West Ham [Old Trafford]
-FAINALI CARLING CUP: Jumapili Feb 28 v Villa [Wembley]
Mwezi Februari ni muhimu mno kwa Mabingwa Watetezi wa England Manchester United wanaowania kutwaa taji la Ubingwa wa England kwa mara ya 4 mfululizo na kuweka rekodi, kutwaa Kombe la Carling na kuingia Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amesema: “Ni kipindi muhimu kwetu. Nilishasema Timu zitapoteza pointi tukielekea ukingoni! Ni muhimu tuwe na matokeo mazuri. Kila mechi ni muhimu na tukishinda badhi ya mechi hizo tuna nafasi ya kutwaa Ubingwa!”
FIFA huenda ikabadili baadhi ya sheria!
FIFA imetoa mapendekezo kwa Bodi ya Soka ya Kimataifa [IFAB] ili kuondoa adhabu tatu kwa mpigo ambazo hutolewa kwa Mchezaji anaemchezea Mchezaji mwingine rafu ndani ya boksi na Refa kuamua Mchezaji huyo aliechezewa rafu alikuwa waziwazi akienda kufunga na hivyo kulazimika kutoa Penalti, Kadi Nyekundu kwa mkosaji na pia baadae mkosaji huyo kufungiwa mechi 3.
FIFA imeona adhabu hizo 3 kwa mpigo ni kubwa mno na hivyo inataka penalti ikitolewa Mchezaji huyo mkosaji apewe Kadi ya Njano tu.
IFAB itakutana Machi 6 kutoa uamuzi
Dondoo nyingine kwenye mkutano huo ni kupiga marufuku Wachezaji wanaopiga penalti kugushi wakati wakikimbia kwenda kupiga mpira kwani sheria ya sasa haikatazi hilo ingawa Refa ana uhuru wa kutoa uamuzi akiona Mpigaji anatenda kinyume cha uanamichezo.
Vingine vitakavyo kuwa kwenye meza ya mjadala ni teknolojia ya kuamua kama mpira umevuka mstari wa golini, na hivyo ni goli au la, na majaribio ya kuwa na Marefa wawili wa ziada wanaokaa nyuma ya kila goli yaliyokuwa yakifanywa kwenye Mashindano ya EUROPA LIGI.

Friday 12 February 2010

MECHI ZA RAUNDI YA 5 KOMBE LA FA Jumamosi & Jumapili
[saa za bongo]
Jumamosi, Februari 13
[saa 9 mchana]
Chelsea v Cardiff
[saa 9 na nusu mchana]
Southampton v Portsmouth
[saa 12 jioni]
Derby County v Birmingham
Reading v West Bromwich
[saa 2 na robo usiku]
Manchester City v Stoke City
Jumapili, Febryari 14
[saa 10 na nusu jioni]
Bolton v Tottenham
[saa 12 jioni]
Fulham v Notts County
[saa 12 dakika 45]
Crystal Palace v Aston Villa
Chelsea v Cardiff
Chelsea ndio Mabingwa Watetezi wa Kombe hili na wataikaribisha Cardiff huko Stamford Bridge katika mechi ya kwanza kabisa ya Wikiendi mahsusi kwa FA Cup tu.
Chelsea watacheza bila ya Wachezaji wao wawili, Nahodha John Terry aliepewa likizo kupumzisha akili baada ya kuandamwa na kashfa nzito ya kutembea na gelfrendi wa Mchezaji mwenzake Wayne Bridge na Mchezaji mwingine atakaekosekana ni Ashley Cole alievunjika enka.
Southampton v Portsmouth
Klabu iliyo mashakani nje na ndani ya uwanja, Portsmouth, bado inadunda kwenye FA Cup na wanakwaana na jirani zao Southampton inayocheza Daraja la chini.
Portsmouth wako kwenye mtihani mkubwa wa kutaka kufilisiwa na Mamlaka ya Kodi kwa kutolipa Kodi na kesi ipo Mahakamani.
Uwanjani, Portsmouth ndio wanashikilia mkia kwenye Ligi Kuu.
Derby County v Birmingham
Hii pia ni mechi ya Klabu zitokazo maeneo ya pamoja na Birmingham ipo Ligi Kuu na Derby iko Daraja la chini.
Reading v West Bromwich Albion
Reading, walizibwaga Klabu za Ligi Kuu Liverpool na Burnley katika Raundi zilizopita za FA Cup, Raundi hii wanakutana na kigogo wa Daraja la Championship, West Bromwich Albion, ambao wengi wanategemea watarudi Ligi Kuu msimu ujao.
Manchester City v Stoke City
Manchester City v Stoke ni pambano la pili la Raundi hii linalozikutanisha Timu za Ligi Kuu pekee kwenye Raundi hii ya 5 ya FA Cup.
Man City walitolewa kwenye Nusu Fainali ya Kombe la Carling na Wapwa zao Man United hivyo watakaza uzi ili wasibwagwe nje kwenye Kombe hili pia.
Bolton v Tottenham
Mechi hii ndio ya kwanza katika mechi 3 za Jumapili na ni ya pili inayozikutanisha Timu za Ligi Kuu pekee.
Fulham v Notts County
Notts County waliibwaga Wigan Raundi iliyopita na watataka tena kuibwaga Timu ya Ligi Kuu watakapocheza na Fulham ambayo ina majeruhi kibao.
Crystal Palace v Villa
Crystal Palace ipo kwenye matatizo makubwa kifedha na sasa ipo mikononi mwa Wasimamiza wanaotaka kuifilisi lakini hilo halikuwasimamisha kuibwaga Timu ya Ligi Kuu Raundi iliyopita walipoipiga kumbo Wolves.
Safari hii wapo vitani na Aston Villa Timu ambayo tayari ipo Fainali ya Kombe la Carling na itacheza na Manchester United kwenye Fainali hiyo hapo Februari 28.
Togo yakata rufaa Mahakamani!!
Shirikisho la Soka la Togo limefaili rufaa yao kwenye Mahakama ya Usuluhishi katika Michezo [CAS] huko Uswisi kupinga adhabu waliyopewa na CAF ya kufungiwa kucheza Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mawili yajayo kwa kile kilichoitwa Serikali ya Togo kuingilia masuala ya soka.
Togo walijitoa kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika yaliyofanyika mwezi uliokwisha huko Angola kufuatia Basi walilokuwa wakisafiria kutoka Congo kuingia Angola Jimbo la Cabinda kushambuliwa kwa risasi na Waasi waliowaua Dereva wa Basi hilo pamoja na Maafisa wawili wa Timu ya Togo.
CAF imedai kuwa Wachezaji wa Togo walikuwa tayari kuendelea na mechi lakini Serikali yao iliwarudisha nyumbani.
Katika Soka Togo kwa sasa inaongozwa na Kamati ya Muda iliyowekwa Januari na FIFA kufuatia mgogoro kwenye Chama cha Soka na Kamati hiyo ndio iliyokata rufaa.
Grant matatani na FA!
Meneja wa Timu taabani ndani na nje ya Uwanja, Portsmouth, Avram Grant, ameshtakiwa na Chama cha Soka cha England, FA, baada ya kumvaa Refa Kevin Friend wakati wa mapumziko na kumshambulia kwa maneno Februari 9 huko Fratton Park katika mechi ya Ligi Kuu kati ya Portsmouth na Sunderland iliyokwisha 1-1. Pia, mashitaka hayo yanahusishwa na matamshi yake baada ya mechi.
Grant amepewa mpaka Alhamisi ijayo kutoa utetezi wake.
Grant alikasirishwa na Refa Friend aliewanyima penalti mbili na kumpa Kadi Nyekundu Mchezaji wake Ricardo Rocha na kutoa penalti dhidi yao iliyotoa bao walilofungwa dakika ya 12 ya mchezo.
Refa huyo Friend katika mechi hiyo pia aliwatoa Wachezaji Lee Cattermole na David Meyler wa Sunderland lakini Grant amedai wao ndio walikuwa wakionewa kwa maamuzi yake.
Grant alisema: “Marefa ni wakweli lakini hali ya uwanjani na wao kusoma magazeti kunawatia kasumba! Siwezi kupigana na dunia nzima! Klabu hii imeandamwa kila kona, hatuwezi kusajili, Marefa wanatusakama! Tulipocheza na Man City tulinyimwa penalti na walipata goli la ofasaidi! Na Fulham, ofsaidi ya Zamora! Na Man United, wako mbele 1-0, Evra anashika kwa mikono miwili, hamna penalti! Na Sunderland, penalti mbili! Naweza kupigana na kila kitu lakini saa nyingine huwezi! Pengine ni rahisi kutuonea!”
Refa Mama aweka historia!!
Refa Amy Fearn anawania kuchezesha Ligi Kuu England baada ya kuwa Refa wa kwanza Mwanamke kuchezesha pambano la Ligi Daraja la Championship, ambalo ni chini tu ya Ligi Kuu, alipochezesha dakika 20 za mwisho za mechi ya Ligi kati ya Coventry City na Nottingham Forest waliyoshinda Coventry 1-0 Jumanne iliyopita baada ya Refa Tony Bates kuumia na kulazimika kutoka nje dakika ya 71 ya mchezo.
Mwenyewe Fearn, miaka 31, amesema: “Itakuwa vyema kuchezesha Ligi Kuu lakini najua kupata nafasi ni ushindani mkubwa!”
Fearn alianza kuwa Refa tangu akiwa na miaka 16 na amesema ni matumaini yake kuweka historia hiyo kutakuwa ni changamoto kwa Wanawake wengine kushiriki katika soka.
Fearn alisema: “Uamuzi wa nani anaingia kama Refa wa Akiba hufanywa kabla ya mechi. Refa alietoka, Bates, aliniambia nitulie na nijitahidi tu! Najua Washabiki walivutwa na kuchangamshwa na kuingia kwangu lakini sikumbuki walivyoshangilia! Ilikuwa vyema hamna utata uliotokea dakika zile 20 ingawa Forest walikazana kurudisha bao! Soka inahusu Wachezaji si Marefa!”
Mchezaji alielaumu Refa achunguzwa na FA!!!
Straika wa Bolton Kevin Davies liemponda Refa Mark Clattenburg baada ya kulikataa goli lake safi ambalo lingeipatia ushindi Timu yake ilipocheza na Fulham katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa Reebok Stadium na kwisha 0-0 hivi karibuni anachunguzwa na FA kwa matamshi yake.
FA imemwandikia Mchezaji huyo kumtaka ajieleze kuhusu matamshi hayo na maelezo hayo ndio yatatolewa uamuzi ashtakiwe au la.
Davies alidai: “Kila mara akituchezesha, Clattenburg anatuonea! Nilipojua Refa ni nani nilijua hatupati kitu! Siku zote naamini Refa huyo ana chuki binafsi na sisi au mimi!!”
Hata hivyo, Meneja wake wa Bolton Owen Coyle ametetea Mchezaji huyo na kusema alikuwa na haki ya kulalamika na akadai itasikitisha sana ikiwa atashtakiwa kwa kuwa mkweli.
NI MAJERUHI TU:
• Ashley Cloe nje miezi mitatu, Kombe la Dunia hatihati kwake!
• Giggs auti mwezi!
• Arsenal wapo kibao!
Mechi za Ligi Kuu za katikati ya wiki zimezua balaa kwa baadhi ya Klabu na zitapoteza Wachezaji wao muhimu katika kipindi hiki muhimu tukielekea ukingoni mwa Ligi.
Ashley Cole wa Chelsea alitolewa kipindi cha pili cha mechi ya Jumatano ambayo Chelsea walifungwa 2-1 na Everton na jana imethibitika kuwa amevunjika enka na atakuwa nje kwa miezi mitatu.
Hilo ni pigo kubwa si tu kwa Chelsea bali pia kwa England kwani Cole ni Beki wa kushoto wa kutumainiwa na kuumia huku kuna maana atarudi uwanjani mwezi Mei wakati Kombe la Dunia England inacheza mechi ya kwanza Juni 12 na USA.
Klabuni kwake, nafasi ya Cole inaweza kuzibwa na Yuri Zhirkov na hata Beki wa kulia Paulo Ferrera.
Kwa England, nafasi yake huenda ikazibwa na Wayne Bridge Mchezaji alievutwa kwenye kashfa ya John Terry kwani gekfrendi wake wa zamani ambae amezaa nae mtoto anadaiwa kutembea na John Terry, ambae ni mwanandoa, na hilo limesababisha Terry atimuliwe Unahodha wa England.
Kashfa hiyo inadaiwa kutokea wakati wote Bridge na Terry ni Wachezaji wa Chelsea.
Kwa sasa Bridge yupo Manchester City.
Huko Manchester United kuna pigo la kumkosa Mkongwe Ryan Giggs ambae alivunjika mkono kwenye droo ya 1-1 ya Ligi Kuu na Aston Villa baada ya kugongana na Steve Sidwell wa Villa na ikabidi abadilishwe.
Man United imethibitisha Giggs atakosekana kwenye mechi ijayo ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE huko Milan, Italia watakapocheza na AC Milan Jumanne Februari 16.
Vilevile, atazikosa mechi za Ligi Kuu dhidi ya Everton, Wolves na West Ham na pia Fainali Kombe la Carling hapo Februari 28 Man U watakapovaana na Aston Villa Wembley Stadium.
Man United imesema mechi ya kwanza ambayo Giggs ataweza kucheza ni ile ya marudiano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na AC Milan hapo Machi 10 uwanjani Old Trafford.
Nao Arsenal, ambao hawana mechi wikiendi hii kwa vile wameshatolewa Kombe la FA, mechi yao inayofuata ni Jumatano huko Ureno watakapocheza na FC Porto kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE, wanakabiliwa na kuumia kwa Andrey Arshavin na Alex Song kwenye mechi ya Ligi Jumatano na Liverpool ambayo walishinda 1-0.
Meneka wa Arsenal, Arsene Wenger, amesema inabidi uchunguzi ufanywe kwa Wachezaji hao.
Hata hivyo, Fowadi wao wa Croatia mwenye asili ya Brazil Eduardo amepona na huenda akachezeshwa mechi hiyo na FC Porto.

Thursday 11 February 2010

Fabregas ang’aka dili ya Barca!!!
Kepteni wa Arsenal Cesc Fabregas amezikataa taarifa kuwa amekubaliana na Barcelona ili ajiunge nao msimu ujao.
Ripoti ambazo chanzo chake ni Spain zimedai kuwa Fabregas amefikia makubaliano kimdomo ili ajiunge na Barcelona ingawa Klabu ya Barcelona haraka imezikana taarifa hizo.
Fabregas amesema: “Wao Barca wamezikataa taarifa hizo, na mimi nazikataa! Mie mawazo yangu yote ni Arsenal tu! Nadhani tunahitaji kuheshimiwa.”
Nae Bosi wa Arsenal, Arsene Wenger, amezitupilia mbali taarifa hizo na kuziita ni upuuzi.
Lakini Baba yake Fabregas amedai mwanawe ataongea na Barcelona mwishoni mwa msimu si kwa sasa kwa vile yupo tu kupigania Ubingwa Arsenal na vile vile amedai ni wajibu wa Klabu hizo mbili kujadiliana mwishoni mwa msimu.
Meneja wa Tottenham atinga kwa Pilato!!!
Harry Redknapp, Meneja wa Tottenham, leo ametinga Mahakamani kujibu mashitaka mawili ya kukwepa kodi aliyoshitakiwa na mwenzake Milan Mandaric ambae ni Mwenyekiti wa Klabu ya Soka Leicester City iliyo Daraja la chini.
Wote wawili wameachiwa nje kwa dhamana hadi Aprili 14 kesi yao itakapoendelea.
Mashitaka haya yanahusu makosa yaliyodaiwa kutendeka wakati Harry Redknapp akiwa Meneja wa Portsmouth na Milan Mandaric akiwa Mwenyekiti wa Klabu hiyo.
Arsenal na Hull City watwangwa faini!!!
Chama cha Soka cha England, FA, kimezipiga faini Klabu za Arsenal na Hull City kwa kosa la kushindwa kuwadhibiti Wachezaji wao kufuatia purukushani iliyotokea Desemba 19 mwaka jana wakati Timu hizo zilipokutana Uwanja wa Emirates.
Vurugu hizo za Wachezaji zilianza kabla ya haftaimu wakati Samir Nasri wa Arsenal alipomtimba Richard Garcia wa Hull City na Stephen Hunt akavutana na Samir Nasri kuhusu tukio hilo na Wachezaji wengine wakajumuika katika shika nikushike hiyo mbele ya Refa Steve Bennett ambae aliwapa Kadi za Njano Nasri na Hunt kwa vurumai hiyo.
Hata hivyo FA ikaamua kuzishitaki Klabu zote mbili na Hull wakakiri kosa lakini Arsenal wakalikataa.
Kamisheni ya Sheria ya FA imeamua Klabu zote zipigwe faini.
Hull City wametakiwa walipe Pauni Elfu 40 na Arsenal Pauni Elfu 20 huku Klabu zote zikipewa onyo la kuchunga mwenendo wao.
Wachezaji Man U wapewa ofu
Sir Alex Ferguson ameipa Timu yake ofu mara baada ya mechi ya Ligi Kuu ya hapo jana waliyocheza na Aston Villa kwa vile wikiendi hii hawana mechi yeyote kwani hii ni wikiendi ya mechi za Kombe la FA na Manchester United wameshatolewa kwenye kinyang’anyiro hicho.
Mechi inayofuata ya Manchester United ni ile ya mtoano wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE itakayochezwa huko Milan, Italia dhidi ya AC Milan Jumanne Februari 16.
Ferguson amesema: “Ni matayarisho mazuri kwetu! Wachezaji wapumzike siku chache na Jumamosi watajumuika tena kwa mazoezi ya mechi hiyo ya Ulaya!”
Kiungo Darren Fletcher ameshangilia ofu hiyo na kusema wanastahili hasa baada ya kucheza mechi ya jana na Aston Villa waliyotoka droo ya 1-1 wakiwa mtu 10 kwa zaidi ya dakika 60 baada ya mwenzao Nani kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
Blatter asanifu Kashfa ya Terry!!
Sepp Blatter, Rais wa FIFA, ameleta mzaha kwenye kashfa iliyomkumba Nahodha wa Chelsea John Terry iliyohusu kutembea na gelfrendi wa Mchezaji mwenzake wa Chelsea wakati huo na pia England, Wayne Bridge, ambayo imemsababisha afukuzwe Unahodha wa England kwa kusema kashfa hiyo ingesifiwa katika Nchi nyingine hasa zile za Kilatino.
Blatter alitoa mzaha huo akiwa Mjini Vancouver huko Canada akihudhuria Mkutano wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki na amesema Nchi kama Ufaransa, Italia na Spain ufuska wa Terry usingezua zogo.
Huko England kumekuwa na presha kubwa iliyomsababisha Kocha wa England, Fabio Capello, amwondoe Unahodha John Terry na kumpa aliekuwa Msaidizi wake Rio Ferdinand, Beki wa Manchester United.
Pichani ni Wayne Bridge na John Terry.
KWINGINEKO ULAYA: Ratiba
BUNDESLIGA
Ijumaa, Februari 12
Borussia Moenchengladbach v Nurnberg
Jumamosi, Februari 13
Stuttgart v Hamburg
Bayer Leverkusen v Wolfsburg
Hertha Berlin v Mainz 05
Hannover v Werder Bremen
Bochum v 1899 Hoffenheim
Bayern Munich v Borussia Dortmund
Schalke v Cologne
Eintracht Frankfurt v Freiburg
LA LIGA
Jumamosi, Februari 13
Xerez v Real Madrid
Villareal v Athletic Bilbao
Sporting Gijon v Valencia
Getafe v Almerica
Jumapili, Februari 14
Valladoid v Real Zaragoza
Sevilla v Osasuna
SERIE A
Ijumaa, Februari 12
AC Milan v Udinese
Jumamosi, Februari 13
Sampdoria v Fiorentina
Roma v Palermo
Jumapili, Februari 14
Parma v Lazio
Napoli v Inter Milan
Juventus v Genoa
Terry apewa mapumziko
Chelsea imethibitisha kuwa Nahodha wao John Tery hataonekana kwenye mechi ya FA Cup watakapocheza na Cardiff siku ya Jumamosi kwa sababu amepewa mapumziko mafupi na atarudi Uwanjani Februari 20 Chelsea watakapocheza na Wolves kwenye Ligi Kuu.
Terry, ambae anakabiliwa na kashfa nzito ya kutembea na gelfrendi wa Wayne Bridge aliekuwa Mchezaji mwenzake Chelsea na hata kusababisha kutimuliwa Unahodha England, jana alicheza katika kipigo cha Chelsea cha 2-1 walichokipata toka kwa Everton na goli zote zinadaiwa ni makosa ya Terry.
Inaaminika Terry atafunga safari kwenda Dubai aliko Mkewe ili kutafuta amani kufuatia kashfa yake. 
Ferguson: Nyekundu kwa Nani sawa!
Wengi waliamini Kadi Nyekundu aliyopewa Winga Nani kwenye mechi ya Ligi Kuu hapo jana kati ya Aston Villa na Manchester United ilikuwa ni makosa kwa vile alionekana wazi kuucheza mpira, Meneja wake, Sir Alex Ferguson, amekiri Refa Peter Walton alikuwa sahihi kumpa Kadi Nyekundu Nani.
Kutolewa huko kwa Nani kunamaanisha kafungiwa mechi 3 na hivyo hawezi kucheza Fainali ya Kombe la Carling dhidi ya Aston Villa hapo Februari 28 na pia atazikosa mechi za Ligi kabla ya hapo za Everton na West Ham.
Wakati huo huo, Ferguson amesema Veterani Ryan Giggs alipelekwa Hospitali kupiga eksirei mkono wake baada ya kuumizwa na Steve Sidwell hapo jana kwenye mechi ya Ligi na Aston Villa na haijajulikana ameumia kiasi gani na huenda akaikosa mechi ijayo na AC Milan.
Wikiendi hii Manchester United haina mechi kwa vile kuna mechi za FA Cup tu na wao washatolewa.
Mechi yao inayofuata ni Jumanne Februari 16 huko Milan, Italia watakapocheza na AC Milan kwenye Raundi ya Mtoano wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
KANDANDA MWEZI MZIMA-RATIBA KAMILI
[saa za bongo]
FA CUP
Jumamosi, Februari 13
[saa 9 mchana]
Chelsea v Cardiff
[saa 9 na nusu mchana]
Southampton vPortsmouth
[saa 12 jioni]
Derby County v Birmingham
Reading v West Bromwich
[saa 2 na robo usiku]
Manchester City v Stoke City
Jumapili, Febryari 14
[saa 10 na nusu jioni]
Bolton v Tottenham
[saa 12 jioni]
Fulham v Notts County
[saa 12 dakika 45]
Crystal Palace v Aston Villa
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
Jumanne, 16 Februar1 2010
AC Milan v Man United
Lyon v Real Madrid
Jumatano, 17 Februari 2010
Bayern Munich v Fiorentina
FC Porto v Arsenal
Jumanne, 23 Februari 2010
Olympiakos v Bordeaux
VfB Stuttgart v Barcelona
Jumatano, 24 Februari 2010
CSKA Moscow v Sevilla
Inter Milan v Chelsea
LIGI KUU
Jumanne, Februari 16
[saa 4 dak 45 usiku]
Stoke v Man City
Jumatano, Februari 17
[saa 5 usiku]
Wigan v Bolton
Jumamosi, Februari 20
[saa 9 dak 45 mchana]
Everton v Man United
[saa 12 jioni]
Arsenal v Sunderland
West Ham v Hull City
Wolves v Chelsea
[saa 2 na nusu usiku]
Portsmouth v Stoke
Jumapili, Februar 21
[saa 11 jioni]
Aston Villa v Burnley
[saa 12 jioni]
Fulham v Birmingham]
Man City v Liverpool
[saa 1 na robo usiku]
Wigan v Tottenham
Jumatatu, Februari 22
[saa 5 usiku]
Blackburn v Bolton
Jumanne, Februari 23
[saa 5 usiku]
Man United v West Ham
Jumamosi, February 27
[saa 9 dak 45 mchana]
Chelsea v Man City
[saa 12 jioni]
Birmingham v Wigan
Bolton v Wolves
Burnley v Portsmouth
[saa 2 na nusu usiku]
Stoke v Arsenal
Jumapili, Februari 28
[saa 10 jioni]
Tottenham v Everton
[saa 12 jioni]
Liverpool v Blackburn
Sunderland v Fulham
FAINALI CARLING CUP
Jumapili, Februari 28
[saa 12 jioni]
Manchester United v Aston Villa
LIGI KUU: MATOKEO Mechi za Jumatano 
Chelsea yafa, Arsenal kidedea, Man United ngoma ngumu!!
MATOKEO KAMILI:
Blackburn 1 Hull City 0
Everton 2 Chelsea 1
Arsenal 1 Liverpool 0
Aston Villa 1 Manchester United 1
West Ham 2 Birmingham 0
Wolves 1 Tottenham 0
Arsenal 1 Liverpool 0
Bao la Abou Diaby limewapa ushindi Arsenal dhidi ya Liverpool na kuwapa faraja kubwa wapenzi wa Arsenal baada ya kupata vipigo viwili mfululizo.
Arsenal wanaendelea kushikilia nafasi ya 3 kwenye Ligi na wako pointi 5 nyuma ya Man United ambao ni wa pili huku Chelsea wakiwa juu pointi moja mbele ya Man United.
Vikosi:
Arsenal: Almunia, Eboue, Gallas, Vermaelen, Clichy, Fabregas, Song, Diaby, Nasri, Bendtner, Arshavin.
Akiba: Fabianski, Sagna, Rosicky, Walcott, Denilson, Traore, Campbell.
Liverpool: Reina, Carragher, Skrtel, Agger, Insua, Lucas, Mascherano, Kuyt, Gerrard, Maxi, Ngog.
Akiba: Cavalieri, Riera, Aurelio, Babel, Spearing, Degen, Kelly.
Refa: Howard Webb
Everton 2 Chelsea 1
Mabao mawili ya Luis Saha yamewaua Chelsea na kuwapa ushindi Everton wakiwa kwao Goodison Park lakini Chelsea bado wako juu Ligi Kuu kwa pointi 1 baada ya Man United kutoka sare na Aston Villa.
Chelsea ndio waliopata bao la kuongoza kupitia Malouda dakika ya 17 lakini Everton wakarudisha kupitia Saha.
Katika dakika za mwisho za kipindi cha kwanza Everton walipewa penalti baada ya Carvalho kumwangusha Donovan ndani ya boksi na Saha akakosa kufunga.
Kipindi cha pili, Saha akafunga bao na kuipa ushindi Everton.
Vikosi:
Everton: Howard, Neville, Heitinga, Distin, Baines, Donovan, Arteta, Osman, Bilyaletdinov, Cahill, Saha.
Akiba: Nash, Vaughan, Gosling, Yakubu, Senderos, Rodwell, Coleman.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Carvalho, Terry, Ashley Cole, Lampard, Mikel, Zhirkov, Anelka, Drogba, Malouda.
Akiba: Hilario, Ballack, Paulo Ferreira, Kalou, Sturridge, Matic, Bruma.
Refa: Alan Wiley
Aston Villa 1 Manchester United 1
Manchester United wakicheza mtu 10 kwa muda mrefu baada ya Mchezaji wao Nani kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu ambayo Wadau wengi wanaamini ili kuwa ni kali mno kupewa kwani aliucheza mpira, walifanikiwa kutoka droo na Aston Villa wakiwa nyumbani Villa Park.
Villa ndio walitangulia kwa bao la kichwa la Carlos Cuellar dakika ya 18.
Man United walisawazisha dakika 3 baadae baada ya krosi ya Nani kumkuta Giggs aliefumua shuti lililombabatiza James Collins na kutinga.
Vikosi:
Aston Villa: Friedel, Cuellar, Collins, Dunne, Luke Young, Petrov, Ashley Young, Milner, Delph, Downing, Agbonlahor.
Akiba: Guzan, Sidwell, Carew, Delfouneso, Davies, Salifou, Beye.
Man United: Van der Sar, Rafael Da Silva, Brown, Jonathan Evans, Evra, Scholes, Carrick, Fletcher, Nani, Rooney, Giggs.
Akiba: Foster, Neville, Owen, Berbatov, Park, Valencia, Gibson.
Refa: Peter Walton

Wednesday 10 February 2010

LIGI KUU: Kivumbi leo!!!
RATIBA: Jumatano, Februari 10
[saa 4 dak 45 usiku]
Arsenal v Liverpool
Aston Villa v Man Utd
Blackburn v Hull
West Ham v Birmingham
Wolverhampton v Tottenham
[saa 5 usiku]
Everton v Chelsea
TATHMINI: Baadhi ya Mechi
Aston Villa v Manchester United
Mechi ipo Villa Park, nyumbani kwa Aston Villa, na Aston Villa watataka waifunge kwa mara ya pili Manchester United kwani katika mechi ya kwanza huko Old Trafford walishinda bao 1-0.
Lakini Man United watataka kusawazisha rekodi yao kwa Villa kwani ushindi huo wa Villa ulikuwa ni wa kwanza katika mechi 25 kati yao.
Katika mechi hii huenda Villa wakamkosa Mshambuliaji Emile Heskey ambae alitolewa katika mechi ya Jumamosi na Tottenham huku akichechemea baada ya kuumia mguu.
Man United watamkosa Rio Ferdinand ambae anatumikia kifungo cha mechi 4 na hii ni mechi yake ya 3 kuikosa.
Vikosi vitatokana na:
Aston Villa: Friedel, Guzan, Beye, Cuellar, Collins, Dunne, L Young, A Young, Petrov, Milner, Downing, Delph, Agbonlahor, Carew, Heskey, Delfouneso, Sidwell, Davies, Clark.
Man United: Van der Sar, Kuszczak, Neville, Brown, Rafael, De Laet, Vidic, Evans, Evra, Fabio, Park, Nani, Valencia, Carrick, Scholes, Fletcher, Gibson, Anderson, Giggs, Rooney, Owen, Berbatov, Diouf.
Refa : Peter Walton
Arsenal v Liverpool
Mechi hii ipo Emirates Stadium ambako katika mechi yao ya mwisho hapo nyumbani Arsenal walitandikwa 3-1 na Manchester United na mechi iliyofuata, siku ya Jumapili, Arsenal walifungwa 2-0 na Chelsea.
Wenyewe Arsenal washatamka mechi hii ni lazima washinde ingawa ni kivumbi kwa vile Liverpool kwa sasa imefufuka na ipo kwenye wimbi la ushindi.
Liverpool watamkosa Difenda wao Sotirios Kyrgiakos anaetumikia kifungo cha mechi 3 baada ya kutolewa kwa Kadi Nyekundu walipocheza na Everton.
Vikosi vitatokana na:
Arsenal: Almunia, Sagna, Vermaelen, Gallas, Clichy, Arshavin, Fabregas, Walcott, Song, Nasri, Diaby, Fabianski, Campbell, Denilson, Fabianski, Ramsey, Eboue, Bendtner, Rosicky, Eastmond.
Liverpool: Reina, Skrtel, Agger, Carragher, Insua, Gerrard, Lucas, Rodriguez, Riera, Ngog, Kuyt, Cavalieri, Pacheco, Spearing, Darby, Babel, Aurelio, Degen.
Refa : Howard Webb
Everton v Chelsea
Vinara wa Ligi, Chelsea, leo wapo Goodison Park wakiwa wageni wa Everton huku wakiomba wapinzani wao Man United na Arsenal wakwame katika mechi zao na wao waishinde Everton na kuongeza gepu kwenye pointi.
Everton itamkosa Winga wao machachari kutoka Afrika Kusini Steven Pienaar aliepewa Kadi Nyekundu mechi ya Jumamosi walipocheza na Liverpool.
Pia, Everton itamkosa Kiungo Marouane Fellaini alieumia enka siku na Liverpool.
Chelsea nao watawakosa majeruhi wao wa muda sasa kina Michael Essien, Juliano Belletti na Jose Bosingwa.
Katika mechi ya kwanza huko Stamford Bridge, Timu hizi zilitoka sare 3-3.
Vikosi vitatokana na:
Everton: Howard, Neville, Heitinga, Distin, Baines, Senderos, Yobo, Cahill, Rodwell, Arteta, Osman, Bilyaletdinov, Coleman, Saha, Donovan, Yakubu, Anichebe, Vaughan, Duffy, Baxter, Nash.
Chelsea: Cech, Hilario, Turnbull, Ivanovic, Carvalho, Terry, A Cole, Ballack, Deco, Lampard, J Cole, Malouda, Anelka, Sturridge, Borini, Ferreira, Alex, Zhirkov, Kakuta, Obi.
Refa : Alan Wiley
MECHI ZA JANA LIGI KUU:
Portsmouth 1 Sunderland 1
Portsmouth walinusurika kufungwa pale Aruna Dindane alipowasawazishia dakika ya 96
na kuifanya mechi na Sunderland imalizike 1-1.
Sunderland walipata bao lao kupitia Darren Bent kwa penalti baada ya Beki wa Portsmouth Ricardo Rocha kumuangusha Bent ndani ya boksi na Refa akatoa penalti na kumpa Kadi Nyekundu Rocha.
Man City 2 Bolton 0
Mabao ya Tevez na Adebayor yamewawezesha Manchester City kutinga nafasi ya 5 kwenye Ligi baada ya kuifunga Bolton 2-0 hapo jana.
Bao la Tevez lilifungwa kwa penalti baada ya Paul Robinson wa Bolton kumuangusha Adam Johnson ndani ya boksi.
Fulham 3 Burnley 0
Fulham walipata ushindi wa 3-0 dhidi ya Burnley kwa mabao ya Danny Murphy, Elm na Bobby Zamora.
Mpaka mapumziko Fulham walikuwa mbele kwa mabao mawili ambayo wengi wanaamini hayakustahili kwa vile tote yalifungwa wakati kulikuwa na ofsaidi za wazi.
Baada ya mechi Meneja wa Burnley, Brian Laws, alilalamika: “Tuliona wazi bao zao mbili ni ofsaidi! Ingawa hatukucheza vizuri lakini siku zote unataka haki kwa Refa!”
Wigan 1 Stoke City 1
Tuncay aliisawazishia Stoke na kuifanya Timu yake iwe haijafungwa mwaka huu na kuwanyima ushindi Wigan waliopataka bao lao kupitia Paul Scharner.
Meneja wa Stoke Tony Pulis alieleza: “Wigan walikuwa bora kipindi cha kwanza lakini sie tulibadilika baadae!”
Nae Roberto Martinez wa Wigan alisema: “Inavunja moyo ukiongoza halafu ukaukosa ushindi lakini angalau tumepata pointi moja!”
Ronaldinho nje Brazil!!
Ronaldinho,miaka 29, ambae sasa ameanza kung’ara tena na Klabu yake AC Milan hayumo kwenye Kikosi cha Brazil kilichoteuliwa kucheza mechi ya kirafiki hapo Machi 2 na Ireland kwenye Uwanja wa Emirates, nyumbani kwa Arsenal, na hivyo kuleta hisia huenda asiwemo kwenye Timu ya Brazil itakayocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwezi Juni.
Ronaldinho hajaichezea Brazil tangu mwanzoni mwa 2009 na licha ya kelele za Mashabiki huko Brazil na hata wito kutoka Mchawi Pele wa kutaka Ronaldinho aingizwe Kikosini, Kocha wa Brazil Dunga amemuacha Nyota huyo.
Kikosi kamili cha Brazil na Klabu wanazotoka ni:
MAKIPA: Julio Cesar (Inter Milan), Doni (Roma).
WALINZI: Maicon (Inter Milan), Daniel Alves (Barcelona), Gilberto (Cruzeiro), Michel Bastos (Lyon), Juan (Roma), Lucio (Inter Milan), Luisao (Benfica), Thiago Silva (AC Milan).
VIUNGO: Gilberto Silva (Panathinaikos), Josue (Wolfsburg), Felipe Melo (Juventus), Lucas (Liverpool), Kaka (Real Madrid), Ramires (Benfica), Elano (Galatasaray), Julio Baptista (Roma), Kleberson (Flamengo).
MAFOWADI: Robinho (Santos), Adriano (Flamengo), Nilmar (Villarreal), Luis Fabiano (Seville).

Tuesday 9 February 2010

Rio afuta rufaa yake!!
Beki wa Manchester United Rio Ferdinand ameiondoa rufaa yake ya kupinga nyongeza ya adhabu ya kufungiwa mechi moja zaidi aliyopewa baada ya rufaa yake ya awali kupinga kufungiwa mechi 3 kwa kosa la kumpiga na mkono Craig Fagan wa Hull City kwenye mechi ya Ligi Kuu kukataliwa.
Ferdinand, ambae amechukua wadhifa wa kuwa Nahodha wa Timu ya Taifa ya England baada ya kutimuliwa John Terry, anatumikia adhabu yake ya kufungiwa mechi 4 na tayari amezikosa mechi mbili zilizopita dhidi ya Portsmouth na Arsenal na pia atakosa mechi mbili zijazo za Aston Villa na Everton.
Ferdinand ataanza tena kucheza kwenye mechi ya Fainali ya Kombe la Carling hapo Februari 28 Man United watakapokutana na Aston Villa.
Hata hivyo adhabu hii haihusu mechi za UEFA na Ferdinand yuko huru kuichezea Timu yake wiki ijayo itakapokutana na AC Milan kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE huko Milan, Italia Februari 16.
Kwa kuifuta rufaa yake hii Ferdinand ameepuka kuongezewa adhabu ya mechi moja zaidi na kuikosa Fainali ya Kombe la Carling endapo rufaa ingeshindwa.
TATHMINI MECHI ZA LIGI KUU LEO:
-Man City v Bolton
Alipoingia Meneja mpya Roberto Mancini Manchester City ilianza kwa wimbi la ushindi lakini hilo limekwisha baada ya kupata vipigo viwili mfululizo kwenye Ligi kutoka kwa Everton na Hull City.
Bolton wako pointi moja tu juu ya Timu tatu za chini.
Timu hizi zilitoka sare 3-3 katika mechi yao ya kwanza ya Ligi lakini wakati huo walikuwa chini ya Mameneja wengine, Mark Hughes kwa City na Gary Megson kwa Bolton, na wote wamefukuzwa.
-Portsmouth v Sunderland
Portsmouth ndio wako mkiani Ligi Kuu na wanakabiliwa na matatizo makubwa nje ya uwanja yakiwemo kubadilika kwa Wamilikaji wa Klabu na ya kifedha.
Mechi yao ya mwisho walikung’utwa bao 5-0 na Manchester United.
Lakini Sunderland nao wako kwenye kipindi kigumu cha kutoshinda mechi 11 sasa na pia watakumbuka wiki mbili zilizokwisha uwanja huo huo wa Fratton Park walifungwa na Portsmouth na kubwagwa nje ya Kombe la FA.
-Fulham v Burnley
Chini ya Meneja mpya Brian Laws ambae alikuwa hajashinda katika mechi 4, Burnley walipata ushindi wao wa kwanza Jumamosi walipoifunga West Ham nyumbani. Lakini Burnley ugenini ni wabovu na wanakutana na Fulham ambao nyumbani ni jiwe gumu.
-Wigan v Stoke City
Stoke City huwa si wazuri mechi za ugenini na wamefunga bao 4 tu katika mechi 11 za ugenini.
Timu hizi zilitoka sare 2-2 katika mechi yao ya kwanza hapo mwezi Desemba huku Mchezaji wa Wigan Maynor Figueroa akifunga bao ambalo pengine ni la msimu kwani aliupiga mpira akiwa nusu ya kwao ya uwanja.
Mancini apania kuitungua Arsenal nafasi ya 3
Meneja Roberto Mancini wa Manchester City, licha ya kupata kipigo cha 2-1 siku ya Jumamosi kutoka kwa Timu iliyo taabani karibu na mkia Hull City, bado ana imani kuwa Timu yake ina uwezo wa kumaliza ikiwa juu na wanaweza kuwang’oa Arsenal kutoka nafasi ya 3 kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Mancini, aliekiri kupandwa hasira na kuwakaripia Wachezaji baada ya kipigo cha Jumamosi, amesema anajiamini kuwa licha ya kuwa pointi 3 nyuma ya Timu ya 4 Liverpool wana uwezo wa kuwapiku Liverpool na kuwang’oa Arsenal nafasi ya 3 kwani wana mechi mbili mkononi na wakishinda hizo watakuwa pointi 2 tu nyuma ya Arsenal.
Leo Man City wanaikwaa Bolton kwenye mechi ya Ligi Kuu itakayochezwa nyumbani kwao City of Manchester Stadium.
Mancini ametamka: “Nilikasirika baada ya mechi na Hull. Hiyo ni kawaida baada ya mechi kama ile. Naamini tutamaliza Ligi tukiwa juu.”
Meneja huyo Mtaliana amesema Timu za Tottenham, Liverpool, Aston Villa, Manchester City na Arsenal ndizo zinazogombea nafasi za 3 na 4.
Kauli hiyo inamaanisha Ubingwa amewaachia Chelsea au Manchester United.
Mancini, hata hivyo, amekiri Timu yake imeathirika kwa kuwa na majeruhi kama vile Madifenda Joleon Lescott na Kolo Toure.
Pia amebainisha kuwa Timu ina upungufu wa Viungo kwani wana Wachezaji watatu tu kwenye nafasi hiyo nao ni Gareth Barry, Nigel de Jong na Stephen Ireland ambao hawatoshi kwa kucheza msimu mzima.
Wenger awakoromea Waandishi!!
Arsene Wenger amewashambulia vikali Waandishi wa Habari na kudai wanapotosha maneno yake na kuleta picha tofauti na kile anachotamka wakati akihojiwa.
Mara baada ya kipigo cha Jumapili cha Chelsea, ilidaiwa Wenger amesema Arsenal ilikuwa ndio Timu bora na hilo liliwafanya baadhi ya watu, akiwamo Mchezaji wa Chelsea Michael Ballack, kumshambulia Wenger na kudai akifungwa hutoa visingizio kibao.
Wenger alifoka: “Jumapili niliisifia Chelsea. Lakini Waandishi wanachukua neno moja na kuligeuza kuwa stori kubwa. Mlifanya hivyo baada ya mechi na Villa na wamefanya hivyo Jumapili. Mkitaka ntakaa kimya tu! Nimekaa muda mrefu England na najua Timu ikishinda unaweza kusema lolote lakini mimi siku zote nachambua kwa makini na kubainisha nini sawa na nini kosa!”
Wenger aliongeza na kusema bado hawajakata tamaa licha ya kufungwa mfululizo na wapinzani wao wakubwa Manchester United na Chelsea.
Wenger alitamka: “Kitu muhimu ni kushinda tu na baadae tutaona nani Bingwa. Bado kuna mechi 13 na hizo ni pointi 39.”
Wenger vile vile alipuuzia madai kuwa hakutaka kusajili mtu mwezi Januari dirisha la usajili lilipokuwa wazi na alisema walijaribu kusaini Wachezaji lakini haikuwezekana.
Hata hivyo Wenger alikiri Timu yake imeathirika sana kwa kuumia kwa Mastraika wake akiwamo Van Persie.
Alipoulizwa kuhusu kumsajili Mshambuliaji wa Bordeaux Marouane Chamakh, Wenger hakutaka kukubali kama kulikuwa na mazungumzo kati yao ingawa imeripotiwa hivi juzi Chamakh mwenyewe ana lengo la kujiunga na Arsenal.
MSIMU WA ARSENAL WAZIDI KUTOKOMEA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
HII TULIITOA: Friday, 22 January 2010
Arsenal yupo kileleni lakini kimbembe chao kinakuja!!!
• Wiki 3 zijazo, Mechi 6 zijazo kuamua MBIVU au MBICHI!!!!
Baada ya kuwatungua Bolton mabao 4-2 hapo juzi huku wakipata ‘msaada mkubwa’ wa Refa Alan Wiley na hivyo kukaa kileleni mwa Ligi Kuu, Arsenal sasa ndio wanaingia hatua ngumu mno kwao kwa kukumbana na Vigingi na Vigogo vya kila aina ambavyo wakivishinda basi wanaweza wakatwaa Mataji yao ya kwanza tangu Mwaka 2005 walipotwaa FA Cup kwa mara ya mwisho.
RATIBA YAO YA WIKI 3 ZIJAZO NI:
Jumapili, Januari 24
FA Cup: Stoke v Arsenal======KICHAPO 3-1 AUTI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Jumatano, Januari 27
LIGI KUU:
Aston Villa v Arsenal========SARE 0-0
Jumapili, Januari 31
LIGI KUU:
Arsenal v Man United========KIPONDO 1-3
Jumapili, Februari 7
LIGI KUU:
Chelsea v Arsenal=========KIPIGO 2-0
Jumatano, Februari 10
LIGI KUU
Arsenal v Liverpool============NINI??????????????
Jumatano, Februari 17
UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
FC Porto v Arsenal=========VIPI????????????????

Monday 8 February 2010

Ballack: ‘Bingwa ni sisi Chelsea au Man United, Arsenal nje!!’
• Ambatukia Wenger aache visingizio!
Kiungo wa Chelsea Michael Ballack ametamka kuwa Ubingwa wa England sasa unagombewa na Timu mbili tu, Chelsea na Manchester United, na amemtaka Arsene Wenger aache kutoa visingizio kwa Arsenal kutokuwa na uwezo wa kuwafunga wapinzani wao.
------------------------------------------------------------------------------
MSIMAMO KILELENI MWA LIGI:
 [TIMU ZIMECHEZA MECHI 25 ISIPOKUWA INAPOTAJWA]
1 Chelsea pointi 58
2 Man Utd pointi 56
3 Arsenal pointi 49
4 Liverpool pointi 44
5 Tottenham pointi 43
6 Manchester City pointi 41 [mechi 23]
7 Aston Villa pointi 41 [mechi 24]
------------------------------------------------------------------------------ 
Ballack amesema Arsenal ishajulikana na inatambulika uchezaji wake na wapinzani wake na kamwe hawawezi kuchukua Kikombe chochote kwa sasa [Kombe lao la mwisho kuchukua ni FA Cup mwaka 2005] mpaka hapo Wenger atakapoibadilisha na kuifanya iweze kutumia mbinu tofauti uwanjani.
Arsenal wamevikwaa vipigo viwili mfululizo na wapinzani wao wakubwa cha kwanza kikiwa Jumapili iliyopitwa walipochapwa 3-1 na Manchester United na jana kufungwa 2-0 na Chelsea na sasa wako nafasi ya 3 wakiwa pointi 9 nyuma ya Chelsea na pointi 7 nyuma ya Manchester United.
Akimjibu Wenger aliedai Timu nzuri ndio iliyofungwa, Ballack alisema: “Nadhani siku zote anasema hivyo wakifungwa. Wakifungwa siku zote hutoa visingizio. Soka si kumiliki mpira tu. Soka ni kushinda na siku zote tukicheza nao sisi tunacheza kushinda si kumiliki mpira.”
Wadau wengi ambao ni wataalam wa kandanda wanadai Arsenal haina uwezo wa kubadili mbinu ikiwa uwanjani kuibadili soka yao ya kutandaza pasi na kushambulia kwa nguvu ili kufunga mabao na pia haina ubavu wa kuhimili mikikimikiki ya Timu zinazotumia ubavu.
WAFUNGAJI BORA LIGI KUU:
-Rooney [Man United] mabao 21
-Drogba [Chelsea] mabao 17
-Defoe [Tottenaham] 15
-Bent [Sunderland] 14
-Tevez [Man City] 12
-Torres [Liverpool] 12
-Fabregas [Arsenal] 11
-Saha [Everton] 11
-Agbonlahor [Aston Villa] 10
-Lampard [Chelsea] 10
-Kuyt [Liverpool] 9
-Adebayor [Man City] 8
-Anelka [Chelsea] 8
-Berbatov [Man United] 8
-Arshavin [Arsenal] 7
LIGI KUU: Kuendelea Jumanne na Jumatano, Wikiendi inayokuja ni FA Cup!
Mechi za Ligi Kuu zitachezwa tena kesho Jumanne na siku inayofuatia Jumatano na Wikiendi inayokuja, yaani Jumamosi na Jumapili, ni wikiendi ya mechi za Raundi ya 5 ya Kombe la FA.
Kwa Wadau wengi mechi za mvuto ni pale Jumatano na hasa ile ya kukata na shoka ya Arsenal aliejeruhiwa vibaya atakapocheza na Liverpool iliyofufuka Uwanjani Emirates.
Mechi nyingine tamu za siku hiyo ni zile za Aston Villa v Manchester United na ya Everton v Chelsea.
RATIBA KAMILI:
[saa za bongo]
LIGI KUU
Jumanne, Februari 9
[saa 4 dak 45 usiku]
Fulham v Burnley
Man City v Bolton
Portsmouth v Sunderland
Wigan v Stoke
Jumatano, Februari 10
[saa 4 dak 45 usiku]
Arsenal v Liverpool
Aston Villa v Man Utd
Blackburn v Hull
West Ham v Birmingham
Wolverhampton v Tottenham
[saa 5 usiku]
Everton v Chelsea
FA CUP
Jumamosi, Februari 13
[saa 9 mchana]
Chelsea v Cardiff
[saa 9 na nusu mchana]
Southampton vPortsmouth
[saa 12 jioni]
Derby County v Birmingham
Reading v West Bromwich
[saa 2 na robo usiku]
Manchester City v Stoke City
Jumapili, Februari 14
[saa 10 na nusu jioni]
Bolton v Tottenham
[saa 12 jioni]
Fulham v Notts County
[saa 12 dakika 45]
Crystal Palace v Aston Villa
Chelsea kicheko tu!!!
• Wamsapoti Nahodha John Terry
Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti na Shujaa wao Mfungaji wa bao zao za jana Ddier Drogba wamejipongeza kwa ushindi wao wa 2-0 dhidi ya Arsenal uliowafanya watwae tena uongozi wa Ligi Kuu kwa kummwagia sifa Nahodha wao John Terry aliendamwa na kashfa ya kutembea na gelfrendi wa Mchezaji mwenzake Wayne Bridge na kumfanya atimuliwe Unahodha wa England.
Mara baada ya mechi ya jana, Drogba alisema: “Ni wiki ngumu kwetu! Tulimsapoti sana Nahodha Terry!! Ni vyema alicheza na tumeshinda kwani hilo linamtuliza.”
Nae Ancelotti alisema: “Ni Kepteni bora kwetu. Uamuzi wa England si wangu! Kwetu ni mtu safi! Alicheza mechi hii vizuri sana!”
Ancelotti alikataa kuifuta Arsenal kwenye mbio za Ubingwa na amesema Arsenal ni Timu nzuri ila itategemea Chelsea na Manchester United wana mafanikio gani katika mechi zao.
Wenger akiri Ubingwa kwao ni nje ya uwezo!!!
Kufuatia kipigo cha Stamford Bridge hapo jana mikononi mwa Chelsea cha bao 2-0 za Didier Drogba, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amekiri Ubingwa wa Ligi Kuu uko nje ya uwezo wao ingawa amesema hawajakata tamaa.
Wenger ametamka: “Sasa tupo nje ya kinyang’anyiro lakini hatujakata tamaa! Tutapigana mpaka siku ya mwisho! Naamini kila mtu atapoteza pointi. Lazima tushinde Jumatano na Liverpool halafu tutajua tumesimama wapi!”
Kipigo cha jana cha Chelsea kimeifanya Timu ya Wenger iwe kwenye wakati mbaya kwa wiki moja iliyopita kwani Jumapili iliyopita walibamizwa 3-1 na Manchester United nyumbani kwao Emirates.
Wenger amechambua mechi ya jana kwa kusema: “Tulimiliki mpira zaidi ya asilimia 70. Tulikuwa tunashambulia lakini kwenye mechi kubwa ukiwa 2-0 nyuma ni mambo magumu sana! Chelsea walijihami vizuri”
Hata hivyo aliiponda Chelsea kwa kudai kuwa hawakuwa wabunifu na waliharibu soka.
Wenger alisema amefurahishwa na uchezaji wa Timu yake ukilinganisha na mechi ya Manchester United waliyozidiwa kila kitu.
Mchezaji alia na Refa!!!
Straika wa Bolton Kevin Davies amemponda Refa Mark Clattenburg baada ya kulikataa goli lake safi ambalo lingeipata ushindi Timu yake ilipocheza na Fulham katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa Reebok Stadium na kwisha 0-0 hapo Jumamosi.
Davies amedai: “Kila mara akituchezesha, Clattenburg anatuonea! Nilipojua Refa ni nani nilijua hatupati kitu! Siku zote naamini Refa huyo ana chuki binafsi na sisi au mimi!!”
KWINGINEKO ULAYA: MATOKEO 
SERIE A:
Jumapili, Februari 7
Atalanta 1 v Bari 0
Inter Milan 3 v Cagliari 0
Lazio 0 v Catania 1
Bologna 0 v AC Milan 0
Udinese 3 v Napoli 1
Siena 1 v Sampdoria 2
Genoa 1 v Chievo Verona 2
LA LIGA:
Jumapili, Februari 7
Osasuna 1 v Tenerife 0
Racing Santander 1 v Atletico Madrid 1
Athletic Bilbao 3 v Xerez 2
BUNDESLIGA:
Jumapili, Februari 7
Mainz 05 1 v Borussia Moenchengladbach 1
Borussia Dortmund 2 v Eintracht Frankfurt 3

Sunday 7 February 2010

Kipigo kingine kwa Arsenal!!
• Drogba awapiga viwili!!!
Goli mbili za Didier Drogba, dakika ya 7 na 23, zimewaua tena Arsenal kwenye Ligi Kuu na kuwapaisha tena Chelsea kuipiku Manchester United na kuchukua uongozi wa Ligi sasa wakiwa na pointi 58 na Man United wakiwa nafasi ya pili na wana pointi 56.
Arsenal wamebaki nafasi ya 3 wakiwa na pointi 49.
Katika mechi hii Chelsea walitumia mbinu ya kudifendi na kuwaacha Arsenal washambulie na kisha wao kutegemea kuunasa mpira na kufanya shambulizi la nguvu na haraka.
Mbinu hiyo ilifanikiwa mno na ndio iliozaa bao la pili baada ya kaunta ataki ya Chelsea kufanikiwa na Drogba kufunga bao hilo la pili.
Bao la kwanza la Chelsea lilitokana na kona ambayo Arsenal walishindwa kujipanga vizuri na kichwa cha Nahodha wao Terry kumkuta Drogba akiwa pembeni na kupachika kilaini.
Juu ya Chelsea kudifendi vizuri Arsenal nao inabidi wajilaumu wenyewe kwani walimiliki mpira kwa kiwango kikubwa lakini zile mbwembwe za ‘soka tamu’ ndio tatizo lao kubwa huku wakitaka ‘watembee na mpira’ mpaka wavuni.
Sasa, pengine, karata ya mwisho ya Arsenal ipo Jumatano watakapocheza na Liverpool na wakifungwa tu hata hiyo nafasi yao ya 3 iko hatarini kwani Liverpool akishinda mechi hiyo atakuwa na pointi 47 zikiwa pointi 2 tu nyuma ya Arsenal.
Vikosi vilivyyoanza:
Chelsea: Cech, Ivanovic, Carvalho, Terry, Cole, Mikel, Lmpard, Malouda, Ballack, Drogba, Anelka
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Clichy, Walcott, Fabregas, Song, Diaby, Arshavin, Nasri
Refa: Mike Dean
Birmingham 2 Wolves 1
Katika mechi ya Ligi kuu iliyoitangulia ile Bigi Mechi ya Chelsea v Arsenal Wolves walitangulia kufunga bao na kuongoza hadi mapumziko lakini Mkongwe Kevin Phillips, miaka 36, akitokea benchi aliifungia Birmingham bao mbili dakika za mwishoni na kuwapa ushindi wa 2-1.
DROO YA EURO 2012: Tayari, Makundi yapangwa!!!
England imepangwa Kundi moja na Wapwa zao Wales katika Kundi G kuwania kuingia Fainali za EURO 2012 zitakazofanyika katika Nchi mbili, Poland na Ukraine, kwa pamoja.
Nchi nyingine kwenye Kundi la England ni Switzerland, Bulgaria na Montenegro.
Makundi yapo 9 na Makundi 6 yana Nchi 6 na matatu yana Nchi 5.
Fainali hizo za EURO 2012 zitachezwa kuanzia Juni 8, 2012 hadi Julai 1, 2012 na kuna nafasi 14 zinazogombewa na hayo Makundi 9 kujumuika na Wenyeji Poland na Ukraine kufanya jumla ya Timu 16 katika hizo Fainali.
Mechi za Makundi zitachezwa kuanzia Septemba 2010 na kumalizika Oktoba 2011.
Washindi 9 wa Makundi pamoja na Timu moja iliyo nafasi ya pili bora kuliko zote zilizoshika nafasi hiyo ndizo zitaingia Fainali moja kwa moja.
Timu nyingine 8 zilizoshika nafasi ya pili zitapangiwa mechi maalum za mtoano ili kupata Timu 4 zitakazoenda Fainali.
MAKUNDI NI:
KUNDI A: Azerbaijan, Kazakhstan, Belgium, Austria, Turkey, Germany
KUNDI B: Andorra, Armenia, Macedonia, Republic of Ireland, Slovakia, Russia
KUNDI C: Faroe Islands, Estonia, Slovenia, NORTHERN IRELAND , Serbia, Italy
KUNDI D: Luxembourg, Albania, Belarus, Bosnia, Romania, France
KUNDI E: San Marino, Moldova, Hungary, Finland, Sweden, Netherlands
KUNDI F: Malta, Georgia, Latvia, Israel, Greece, Croatia
KUNDI G: Montenegro, WALES , Bulgaria, Switzerland, ENGLAND
KUNDI H: Iceland, Cyprus, Norway, Denmark, Portugal
KUNDI I: Liechtenstein, Lithuania, SCOTLAND , Czech Republic, Spain
BIGI MECHI Jumapili Stamford Bridge: Chelsea v Arsenal
Walipofumuliwa na Didier Drogba na Chelsea yake Uwanja wa Emirates mwezi November mwaka jana mabao 3-0, kila mtu aliwafuta Arsenal toka kwenye kinyang’anyiro cha Ubingwa wa Ligi Kuu lakini wenyewe hawakukata tamaa bali walijikongoja na kurudi tena vitani na kufika kileleni huku wakipigana vikumbo na viongozi wenzao Chelsea na Manchester United.
Lakini kipigo cha 3-1 walichokipata Jumapili iliyopita nyumbani kwao Emirates mikononi mwa Manchester United na sasa kuwafanya wawe pointi 7 nyuma ya Man United walio kileleni na pointi 6 nyuma ya Chelsea walio nafasi ya pili, kumeifanya mechi ya Arsenal na Chelsea huko Stamford Bridge leo iwe ya kufa na kupona kwa Arsenal kwani kipigo kingine ni kusema bai bai Ubingwa kwa Arsenal msimu huu.
Hata hivyo, mechi hii na Chelsea ni ngumu mno kwa Arsenal hasa ukichukulia fomu yao ya hivi karibuni na jinsi wanavyopigwa mabao yanayofanana kwa jinsi yanavyofungwa yote yakiwa yanatoka kwenye ‘kaunta ataki’, yaani mashambulizi ya kushtukiza ya wapinzani wa Arsenal.
Juzi, Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, alipasua kuwa kwa vile Arsenal wanamiliki sana mipira ni lazima watakuja mara kwa mara kwenye boksi lako na ukimudu kuwapokonya mpira wakati huo na kufanya shambulizi la kushtukiza na haraka ni lazima utapata bao kwa vile Wachezaji wao karibu wote wanakuwa wamesonga mbele golini kwako.
Na hivyo ndivyo magoli ya Manchester United yalivyopatikana na hata katika mechi ya nyuma yake Arsenal walipocheza na Everton, bao la Everton lilipatikana mara tu kufuatia kona waliyopiga Arsenal golini kwa Everton na Everton kuunasa mpira na kuelekea mkuku golini mwa Arsenal na kufunga bao sekunde kadhaa baada ya kona ya Arsenal.
Kitu cha kutia hofu kwa Arsenal ni kuwa, licha ya Masentahafu wao William Gallas na Thomas Vermaelen kucheza vizuri sana kibinafsi, Timu haichezi kitimu na kwa sasa hawana Mchezaji ambae ni kiongozi wa majeshi uwanjani kama vile alivyokuwepo Tony Adams au Patrick Viera enzi hizo ambae anaweza kuwabatukia wenzake wakikosea au kuwahamasisha
Ndio, Cesc Fabregas ni Mchezaji mzuri sana lakini si kiongozi na hana sifa za uongozi kwani haamrishi wenzake uwanjani.
Ni kitu cha msingi ukipiga kona ni lazima uhakikishe nyuma kwako kuna Wachezaji wa kutosha kuleta ulinzi.
Hili kwa Arsenal halipo.
Ukitaka kubeba mataji lazima uweke uwiano mzuri wa ‘soka tamu’ na misingi ya ulinzi bora.
DONDOO ZA MECHI YA Leo:
Ukweli ni kwamba Arsenal bado hawajaenguliwa kutoka kinyang’anyiro cha Ubingwa wa Ligi Kuu na kwa mechi ya leo kitu kikubwa kwao ni kurudisha heshima yao baada ya kubamizwa mabao 3-1 na Manchester United wiki iliyopita tena wakiwa Uwanja wa nyumbani Emirates.
Vilevile watakuwa na usongo na mechi ya leo wakikumbuka kipigo toka kwa Chelsea cha bao 3-0 katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu msimu huu.
Lakini msimu uliokwisha, Arsenal waliifunga Chelsea 2-1 hapo hapo Stamford Bridge na hiyo ndiyo mechi ya mwisho kwa Chelsea kufungwa nyumbani sasa zikiwa ni jumla ya mechi 35 bila kufungwa.
Tottenham 0 Aston Villa 0
Tottenham na Aston Villa jana walivimbiana Uwanja wa White Hart Lane na hakuna mbabe aliepatikana na ngoma kuisha 0-0 katika mechi ya Ligi Kuu.
Makipa wa pande zote, Brad Friedel wa Aston Villa na Heurelho Gomes, walistahili pongezi kwa kuziokoa Timu zao.
Kwa Timu hizi mbili ushindi ulikuwa muhimu ili kuipiku Liverpool toka nafasi ya 4 waliyoichukua katika mechi iliyochezwa kabla ya hii walipowafunga Everton 1-0 na kufikisha pointi 44 kwa mechi 25.
Kwa sare hiyo Tottenham wamebaki nyuma ya Liverpool na wana pointi 43 kwa mechi 25 wakifuata Man City wenye pointi 41 kwa mechi 23 na Aston Villa pointi 41 kwa mechi 24.
Baada ya Mechi, Meneja wa Tottenham Harry Redknapp alisema: “Kila tukitaka kufunga mpira unambabatiza mtu au unazuiawa! Itakuwa kazi kubwa kuipata nafasi ya 4 au hata ya tatu! Liverpool wanaenda vizuri, Man City na Villa wapo pia!”
Na Meneja wa Aston Villa Martin O’Neill akasema: “Mabeki wetu walikuwa makini. Tottenham ni timu ngumu!”
KWINGINEKO ULAYA: MATOKEO YA WIKIENDI NA RATIBA YA LEO
SERIE A:
Jumamosi, Februari 6
Livorno 0 v Juventus 0
Palermo 2 v Parma 1
Jumapili, Februari 7
Atalanta v Bari
Inter Milan v Cagliari
Lazio v Catania
Bologna v AC Milan
LA LIGA:
Jumamosi, Februari 6
Valencia 2 v Valladoid 0
Barcelona 2 v Getafe 1
Real Madrid 3 v Espanyol 0
Jumapili, Februari 7
Osasuna v Tenerife
Racing Santander v Atletico Madrid
Athletic Bilbao v Xerez
BUNDESLIGA
Ijumaa, Februari 5
Werder Bremen 2 v Hertha Berlin 1
Jumamosi, Februari 6
Freiburg 0 v Schalke 0
Wolfsburg 1 v Bayern Munich 3
1899 Hoffenheim 2 v Hannover 1
Bochum 1 v Bayer Leverkusen 1
Cologne 3 v Hamburg 3
Nurnberg 1 v Stuttgart 2
Jumapili, Februari 7
Mainz 05 v Borussia Moenchengladbach
Borussia Dortmund v Eintracht Frankfurt
Powered By Blogger