Saturday 7 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

NGAO YA HISANI: Chelsea v Man United
Jumamosi Agosi 8, Wembley Stadium, Saa 11 jioni [Bongo Taimu]
Kesho pazia la Msimu mpya wa 2010/11 litafunguliwa Uwanjani Wembley Jijini London kwa Mechi kati ya Mabingwa wa LIGI KUU England, Chelsea, ambao pia ni Mabingwa wa FA Cup, dhidi ya Manchester United waliomaliza Ligi Kuu nafasi ya pili.
Kila Timu zimekuwa na maandalizi makali ambapo Chelsea walipata vipigo vitatu mfululizo walipofungwa na Ajax, Eintracht Frankfurt na Hamburg.
Man United walikuwa ziarani huko Canada, USA, Mexico na Ireland ambako walicheza Mechi 5 na kushinda 3 na kufungwa 2.
Katika Mechi ya kesho Chelsea itawakosa Kipa Petr Cech, Mabeki Alex na Jose Boswinga ambao wote ni majeruhi.
Man United itawakosa Rio Ferdinand, Michael Carrick, Mapacha wa Kibrazil Fabio na Rafael, Owen Hargreaves na Gabriel Obertan ambao ni majeruhi.
Meneja wa Chelsea, Carlo Ancelotti, amethibitisha Nyota wake Didier Drogba atanzia benchi kwa vile hajawa fiti kabisa kwa vile ametoka kwenye upasuaji wa nyonga yake.
Nae Sir Alex Ferguson amethibitisha Mastraika wake, Michael Owen na Wayne Rooney, wataonekana kwenye Mechi hiyo.
CHEKI: www.sokainbongo.com

UEFA CHAMPIONS LIGI: Tottenham kukutana na Young Boys
Tottenham, ambayo haijawahi kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI, imepangwa kucheza na Timu ya Uswisi, Young Boys, katika Raundi ya Mchujo na Washindi wa Raundi hiyo wanaingizwa kwenye droo ya kupanga Makundi.
Tottenham wataanza ugenini Agosti 17 huko Berne, Switzerland Uwanja wa Stade de Suiss na marudiano ni White Hart Lane Agosti 25.
Washindi 10 wa Raundi hii ya Mchujo watajumuika na wale Mabingwa 22 walioingizwa moja kwa moja kwenye Makundi ili kupanga Makundi manane ya Timu nne nne kila moja kwenye Droo itakayofanyika Agosti 26.
Droo kamili ya Raundi hiyo ya Mchuzjo ni:
Young Boys (Switzerland) v Tottenham Hotspur (England)
Sporting Braga (Portugal) v Sevilla (Spain)
Werder Bremen (Germany) v Sampdoria (Italy)
Zenit St Petersburg (Russia) v Auxerre (France)
Dynamo Kiev (Ukraine) v Ajax (Netherlands)
Salzburg (Austria) v Hapoel Tel-Aviv (Israel)
Rosenborg (Norway) v Copenhagen (Denmark)
Basel (Switzerland) v FC Sheriff (Moldova)
Sparta Prague (Czech Republic) v MSK Zilina (Slovakia)
Partizan Belgrade (Serbia) v Anderlecht (Belgium)
Man City bado wanataka Wachezaji wapya
Bosi wa Manchester City, Roberto Mancini, amesema wapo kwenye mazungumzo ili kuwanasa Mario Balotelli na James Milner.
Inadhaniwa mazungumzo kuhusu kumchukua Mario Balotelli kutoka Inter Milan yamekwama kwa vile Mchezaji huyo anataka Mshahara mkubwa.
Kuhusu James Milner, kuna mvutano kati ya Man City na Aston Villa kuhusu ada ya uhamisho.
Licha ya kuwataka Wachezaji hao wawili, Man City inakabiliwa na tatizo kubwa la kupunguza Kikosi chake chenye Wachezaji zaidi ya 30 ili wafikie 25 kama Sheria mpya ya usajili inavyotaka.
EUROPA LIGI: Liverpool kucheza na Trabzonspor ya Poland
Kwenye Raundi ya Mchujo ya EUROPA LIGI itakayochezwa Agosti 19 na marudio Agosti 26, Liverpool imepangiwa kucheza na Klabu ya Poland na Mechi ya kwanza itakuwa Anfield.
RATIBA KAMILI:
AIK Solna v Levski Sofia
AZ Alkmaar v FC Aktobe
Aris Salonika v Austria Vienna
BATE v Maritimo
Bayer Leverkusen v Tavriya Symferopol
Besiktas v HJK Helsinki
Borussia Dortmund v FK Qarabag
CSKA Moscow v Anorthosis Famagusta
CSKA Sofia v The New Saints
Celtic v FC Utrecht
Club Bruges v Dinamo Minsk
Debrecen v Litex Lovech
Dnipro v Lech Poznan
Dundee Utd v AEK Athens
FC Vaslui v Lille
Feyenoord v AA Gent
Galatasaray v Karpaty Lviv
Genk v FC Porto
Getafe v Apoel Nicosia
Grasshoppers v Steaua Bucharest
Gyor ETO FC v Dinamo Zagreb
Hajduk Split v Unirea Urziceni
Lausanne Sports v Lokomotiv Moscow
Liverpool v Trabzonspor
Napoli v Elfsborg
Odense BK v Motherwell
Omonia Nicosia v FC Metalist Kharkiv
PAOK Salonika v Fenerbahce
PSG v Macc Tel-Aviv
Palermo v NK Maribor
Politehnica Timisoara v Man City
Rapid Vienna v Aston Villa
SK Sturm Graz v Juventus
Ibir Novosibirsk v PSV
Slovan Bratislava v VfB Stuttgart
Sporting v Brondby
Villarreal v Dnepr Mogilev

Friday 6 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Leo ni Droo za UEFA CHAMPIONS LIGI & EUROPA LIGI kwa ajili ya Raundi ya Mchujo
Leo mchana, Ijumaa, Agosti 6, huko Nyon, Uswisi Makao Makuu ya UEFA, kutafanyika Droo mbili za kupanga wapinzani wa Raundi ya Mchujo ili kuingia hatua ya Makundi kwa Mashindano ya UEFA CHAMPIONS LIGI na EUROPA LIGI.
Kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI, Timu zitanazoanza hatua hiyo ya Raundi ya Mchujo ni AJ Auxerre, Werder Bremen, UC Sampdoria, Sevilla FC na Tottenham Hotspur FC na zitaunganishwa kwenye Droo hiyo na Washindi 15 wa Raundi ya 3 ya Mtoano.
Mechi hizo za Raundi ya Mchujo zitachezwa Agosti 17 na 18 na marudio ni Agosti 24 na 25.
Washindi 10 wa Raundi hii ya Mchujo watajumuika na wale Mabingwa 22 walioingizwa moja kwa moja kwenye Makundi ili kupanga Makundi manane ya Timu nne nne kila moja kwenye Droo itakayofanyika Agosti 26.
Pia Droo ya EUROPA LIGI kwa ajili ya Raundi ya Mchujo itafanyika kesho Ijumaa Agosti 6 na kwenye hatua hii zinaingizwa moja kwa moja Timu 24 kuungana na Washindi 35 wa Raundi ya 3 ya Mtoano pamoja na Timu 15 zilizotolewa Raundi ya 3 ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONS LIGI.

Thursday 5 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Vidic ashangaa uvumi yeye kuhama!
Nemanja Vidic ameshangazwa na uvumi wa muda mrefu uliomhusisha na kuhama Manchester United huku akitangazwa yu njiani kuhamia Barcelona, Real Madrid au AC Milan.
Mwenyewe Vidic, ambae Mkataba wake hivi juzi umeboreshwa na kurefushwa hapo Man United, amesema: “Siku zote nimesema nina furaha hapa! Sijawahi kusema nahama, nawashangaa hao waliokuwa wakisema hivyo! Nina furaha Man United!”
Fabregas kubaki Ze Gunners Msimu mmoja zaidi!
Baada ya mazungumzo ya faragha kati ya Meneja Arsene Wenger na Nahodha Cesc Fabregas, kumeibuka taarifa Fabregas atabaki Arsenal kwa Msimu mmoja zaidi na huenda akahamia Barcelona Mwakani.
Kumekuwa na vuta nikuvute kati ya Arsenal na Barcelona kuhusu Mchezaji huyo kwa Miezi kadhaa sasa na Arsenal iliikataa ofa ya Barca ya Pauni Milioni 29 kumnunua na baada ya hapo ikagoma kusikiliza lolote kuhusu uhamisho wa Fabregas.
Fabregas alianzia Soka lake huko Barcelona kwenye Kikosi cha Vijana na kuhamia Arsenal akiwa na Miaka 16 na sasa akiwa na Miaka 23 anaonekana lulu na Barcelona.
CHEKI: www.sokainbongo.com

Man United yabonda Uwanja mpya
Katika Mechi ya ufunguzi wa Uwanja mpya wa Aviva huko Dublin, Ireland hapo jana Manchester United iliibonda Kombaini ya Ligi ya Airtricity ya huko Ireland kwa mabao 7-1.
Man United jana iliwachezesha Vigogo Wayne Rooney na Michael Owen walioanza na kubadilishwa haftaimu na pia Vidic, Park, Carrick na Valencia walianza.
Mabao ya Man United yalifungwa na Park, bao mbili, Owen, Chicharito, Valencia, Evans na Nani.
France yatangaza Kikosi
Kocha mpya wa Ufaransa, Laurent Blanc, ametangaza Kikosi chake kwa ajili ya Mechi ya kirafiki na Norway itakayochezwa Oslo Wiki ijayo ambacho hakina hata Mchezaji mmoja kati ya 23 waliocheza Kombe la Dunia huko Afrika Kusini.
Katika Kikosi kilichotangazwa wapo Wachezaji 15 ambao wameitwa kwa mara ya kwanza akiwemo Winga wa Wigan Charles N’Zogbia.
Kwa Kocha Blanc hii ni Mechi yake ya kwanza tangu achukue wadhifa toka kwa Raymond Domenech aliekumbwa na mizozo huko Afrika Kusini iliyozua ugomvi kati yake na Mchezaji Nicolas Anelka aliefukuzwa Kikosini na kisha Timu ikagoma kupinga hilo na mwisho France wakaaibishwa kwa kubwagwa nje ya Kombe la Dunia Raundi ya Kwanza huku wakishika mkia Kundi lao.
Wachezaji Samir Nasri na Karim Benzema ambao hawakuchukuliwa Kombe la Dunia wameitwa kwenye Kikosi hicho pamoja na Kiungo Lassana Diarra alieachwa dakika za mwisho baada ya kuugua.
Kikosi kamili: Nicolas Douchez (Rennes), Stephane Ruffier (Monaco), Aly Cissokho (Monaco), Mathieu Debuchy (Lille), Rod Fanni (Rennes), Philippe Mexes (Roma), Adil Rami (Lille), Mamadou Sakho (Paris St Germain), Benoit Tremoulinas (Bordeaux), Yohane Cabaye (Lille), Lassana Diarra (Real Madrid), Blaise Matuidi (Saint-Etienne), Yann Mvila (Saint-Etienne), Charles N'Zogbia (Wigan), Samir Nasri (Arsenal), Moussa Sissoko (Toulouse), Hatem Ben Arfa (Marseille), Karim Benzema (Real Madrid), Jimmy Briand (Lyon), Guillaume Hoarau (Paris St Germain), Jeremy Menez (Roma), Loic Remy (Nice).
Man United yahusishwa na Wachezaji wawili wa Ujerumani
Kumezuka habari nzito zinazowahusu Wachezaji Mesul Ozil wa Werder Bremen na Piotr Trochowski wa Hamburg kuhusishwa na kuhamia Manchester United.
Werder Bremen imeshakiri itamuuza Ozil kwa vile hataki kuongeza Mkataba utakaokwisha mwishoni mwa Msimu mpya wa 2010/11 na hivyo wasipomuuza sasa Mchezaji huyo ataondoka bure Mkataba wake ukiisha.
Kuhusu Trochowski, Wakala wake amekiri kuwepo na mipango ya uhamisho ingawa hakutoboa chochote.
Wachezaji wote hao wawili ni Viungo ambao Man United inawahitaji sana ili kuziba pengo la Paul Scholes ambae umri unampa mkono na pia kuziba nafasi ya Owen Hargreaves ambae ni majeruhi wa muda mrefu na hata nafasi ya Michael Carrick anaelegalega nafasi hiyo muhimu.
Celtic yabwagwa nje UEFA CHAMPIONS LIGI
Licha ya kushinda bao 2-1 hapo jana katika Mechi ya marudio na Braga ya Ureno huko Glasgow, Celtic imetolewa nje kwa jumla mabao 4-2 baada ya kushindiliwa 3-0 katika Mechi ya kwanza.
Sasa Celtic itatupwa kwenye kapu la kucheza Raundi ya Mchujo kuingia Makundi ambayo droo yake itafanyika kesho.

Wednesday 4 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Chelsea waendelea kupigwa huko Ujerumani
Kwa mara ya pili mfululizo huko Ujerumani, Chelsea leo imefungwa tena 2-1 na Hamburg ya Ujerumani katika Mechi ya kirafiki iliyofanyika Uwanja wa HSH Nordbank Arena.
Jumapili iliyopita Chelsea ilipigwa 2-1 na Eintrant Frankfurt.
Leo Chelsea ilitangulia kufunga kwa bao la Frank Lampard dakika ya 24.
Hamburg walipata bao zao mbili Kipindi cha pili zilizofungwa na Mladen Petric, dakika ya 71 na Son dakika ya 86.
Huang bado hajatoa ofa
Mfanya biashara wa Kichina, Kenny Huang, ambae anadaiwa yuko mbioni kuinunua Liverpool kutoka kwa Wamiliki wake Wamarekani wawili, Tom Hicks na George Gillet, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakihaha kutafuta mnunuzi wa Klabu hiyo yenye deni kubwa la zaidi ya Pauni Milioni 237, amekiri kuwa na nia ya kuinunua Liverpool lakini amethibitisha bado hajatoa ofa rasmi.
CHEKI: www.sokainbongo.com

Ancelotti azungumzia kuondoka Cole
Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti amesema ujio wa Yossi Benayoun utawanufaisha baada ya kuondoka Joe Cole ambae walishindwa kumpa Mkataba mpya baada ya ule wa mwanzo kumalizika.
Joe Cole tayari ameshaini Liverpool.
Ancelotti amedai Benayoun ni Mchezaji bora kupita Cole ambae Msimu uliokwisha hakucheza sana kufuatia operesheni ya goti lake.
Wakati huo huo, Ancelotti amedai Sheria mpya ya usajili wa Wachezaji 25 tu na ndani yake 8 wawe ‘wamelelewa’ England au Wales kwa Miaka mitatu kabla hawajatimiza umri wa Miaka 21 haiwapi shida kwa vile Kikosi chao kinakidhi Sheria hiyo.
Sunderland yamwania Kipa Hart kwa Mkopo
Sunderland wamefungua mazungumzo na Manchester City ili wamchukue Kipa Joe Hart, Miaka 23, kwa mkopo.
Msimu uliokwisha, Joe Hart alichezea Birmingha kwa mkopo na Kocha wa Sunderland Steve Bruce amesema tayari washawajulisha Man City kuhusu nia yao na sasa wanangoja jibu tu.
Man City wanakabiliwa na tatizo la kupunguza Wachezaji ili kukidhi Sheria mpya ya usajili wa Wachezaji 25 tu na ndani yake 8 wawe ‘wamelelewa’ England au Wales kwa Miaka mitatu kabla hawajatimiza umri wa Miaka 21.

Tuesday 3 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Chelsea kumnunua Ramires
Chelsea wako mbioni kumsaini Kiungo toka Brazil, Ramires, anaecheza Klabu ya Ureno Benfica kwa Pauni Milioni 17.
Ramires anategemewa kupimwa afya yake na Chelsea Siku ya Jumatano na akifuzu huenda akasaini Mkataba wa Miaka minne.
Hata hivyo, Ramires, Miaka 23, hamilikiwa na Benfica moja kwa moja na hilo limeleta utata katika uhamisho wake.
Mchezaji huyo, aliechezea Brazil mara 16, anamilikiwa na Benfica kwa Asilimia 50 na Asilimia 50 nyingine ni ya Mfanya Biashara wa Uingereza.
Ili kukamilisha uhamisho ni lazima Chelsea wafikie makubaliano na Benfica tu na si huyo Mfanya Biashara kwani Sheria za Ligi Kuu England haziruhusi Mchezaji kumilikiwa na Watu baki.
Chelsea ipo mbioni kuziba mapengo yaliyoachwa na Joe Cole, Michael Ballack na Deco ambao wote wameondoka Klabuni hapo.
Ben Haim atua West Ham kwa Mkopo
West Ham imekamilisha usajili wa Beki Tal Ben Haim, Raia wa Israel, anaechezea Portsmouth iliyoshushwa Daraja toka Ligi Kuu Msimu uliopita.
Ben Hain atakuwepo West Ham hadi Januari Mwakani.
Mchezaji huyo amewahi pia kucheza Klabu za Bolton, Chelsea na Manchester City.
Ben Haim ataungana na Meneja Avram Grant ambae wote wanatoka Israel na wote walikuwa pamoja Portsmouth Msimu uliopita.
FIFA yazipiga Faini Spain na Holland
Holland na Spain ambao walikutana Fainali ya Kombe la Dunia hapo Julai 11 huko Afrika Kusini na Spain kuibuka Bingwa mpya wa Dunia huku Mechi hiyo ikivunja rekodi ya kutolewa Kadi nyingi na Refa wameadhibiwa na FIFA.
Holland imepigwa Faini ya Pauni 9000 kwa Wachezaji wake 8 kupata Kadi za Njano na Beki John Hetinga kupewa Nyekundu baada ya kuchukua Kadi za Njano mbili.
Spain imedungwa Faini ya Pauni 6000 kwa Wachezaji wake watano kupata Kadi za Njano.
Refa katika Mechi hiyo alikuwa Howard Webb wa England.
FIFA ina Sheria inayotaka Nchi ipigwe Faini ikiwa itapata Kadi 5 katika Mechi moja.
Katika Fainali hiyo Spain iliifunga Holland 1-0 na kutwaa Kombe la Dunia.

Monday 2 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Man United kufungua Uwanja mpya Ireland
Baada ya kufungua Uwanja mpya huko Guadalajara, Mexico Siku ya Ijumaa, Manchester United Jumatano watafungua tena Uwanja mpya huko Dublin, Ireland Uwanja ambao unaitwa Aviva kwa kucheza na Kombaini ya Ligi ya huko.
Mastaa ambao hawakuwepo kwenye ziara ya Man United huko Canada, Marekani na Mexico kwa vile walikuwepo Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na hivyo kupewa muda zaidi kupumzika, Wayne Rooney, Michael Carrick, Ji-sung Park na Nemanja Vidic pamoja na Valencia aliekuwa majeruhi, watashuka huko Aviva, Dublin.
Sir Alex Ferguson amethibitisha Wachezaji wake wenye asili ya Ireland, John O’Shea na Darron Gibson, watacheza na Nahodha wa Kikosi hicho atakuwa O’Shea.
Pia alisema Chicharito atashiriki kwenye Mechi hiyo.
CHEKI: www.sokainbongo.com

Anderson anusurika ajali ya Gari!
Kiungo wa Manchester United Anderson Jumamosi alfajiri alinusurika kwenye ajali ya Gari lililopinduka na kuwaka moto huko Braga, Ureno lakini bahati Wasamaria wema wakamnyotoa kabla Gari hilo halijalipuka.
Inadaiwa Anderson alikuwa amekesha kwenye Naitiklabu huko Braga.
Ndani ya Gari hilo pia kulikuwa na Watu wengine wawili lakini haijulikani nani alikuwa akiliendesha.
Anderson, Miaka 22, ambae bado anauguza Goti lake, aliwekwa Hospitali hadi Jumamosi mchana na kisha kuruhusiwa kutoka na inasemekana yuko njiani kurudi Manchester.
Cole si Biashara, adai Ancelotti
Meneja wa Chelsea, Carlo Ancelotti, amesisitiza Beki Ashley Cole hauzwi huku kukiwa na habari nzito kuwa yuko njiani kwenda Real Madrid kuungana na Jose Mourinho ambae ndie aliemtoa Arsenal na kumuingiza Chelsea wakati Mourinho alipokuwa Kocha Chelsea Mwaka 2006.
Ancelotti ametamka: “Cole ni Mchezaji wa Chelsea na kila Mtu asahau kama atauzwa! Hauzwi kwa bei yeyote!”
Mchina aiwania Liverpool!!
Mfanya biashara wa Kichina, Kenny Huang, yuko mbioni kutoa ofa ya kuinunua Liverpool kutoka kwa Wamiliki wake Wamarekani wawili, Tom Hicks na George Gillet, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakihaha kutafuta mnunuzi wa Klabu hiyo yenye deni kubwa la zaidi ya Pauni Milioni 237.
Ingawa Huang ni miongoni mwa Wanunuzi 6, Mchina huyo ndie anaedaiwa kuwa na ofa bora zaidi ambayo ni kumaliza Deni lote na pia kumpa Meneja Roy Hodgson fungu nono la kununua Wachezaji wapya kuimarisha Timu.
Huang anasifika sana kwa kuwekeza kwenye Michezo huko China na pia Marekani ambako Kampuni yake ina hisa kwenye Klabu ya Mpira wa Vikapu ya Cleveland Cavaliers na pia Timu ya Beziboli ya New York Yankees.
Song ang’atuka Cameroun!
Beki Mkongwe wa Cameroun Rigobert Song, Miaka 34, ametangaza kustaafu kuichezea Timu ya Taifa ya Cameroun baada ya kuichezea Mechi 137 tangu Mwaka 1993.
Song ndie anaeshika Rekodi ya kuwa Mchezaji wa kwanza wa Afrika kucheza Fainali za Kombe la Dunia mara 4 na ameshacheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mara 8 na kutwaa Kombe hilo Mwaka 2000 na 2002 alipokuwa Nahodha wa Cameroun.
Song amezichezea Klabu za England Liverpool na West Ham pia Metz ya Ufaransa na Italia Klabu ya Salernitana.
Pia alishacheza Ujerumani kwenye Klabu ya Cologne na baadae kwenda Ufaransa kujiunga na Lens.
Kwa sasa yuko Uturuki na Klabu ya Trabzonspor na kabla ya hapo alikuwa na Galatassaray
Song amenena: “Ni lazima ujue wakati gani ustaafu. Naondoka kwa fahari.”

Sunday 1 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Liverpool yatunguliwa na Monchengladbach
Joe Cole leo alicheza Mechi yake ya kwanza kwa Klabu yake mpya Liverpool lakini ikachapwa 1-0 huko Ujerumani na Borussia Monchengladbach iliyokuwa ikisherehekea Miaka 110 kwenye Uwanja wao Borrusia Park.
Leo, Meneja wa Liverpool, Roy Hodgson, alishusha Kikosi chake imara pale Nahodha Steven Gerrard, Jamie Carragher na Glen Johnson walipochezeshwa kwa mara ya kwanza kabisa katika matayarisho yao ya Msimu mpya.
Bao la ushindi kwa Borussia Monchengladbach lilifungwa dakika ya 8 na Karim Matmour, Mchezaji kutoka Algeria, aliemzidi maarifa Beki wa Liverpool, David Ayala aliechezea shilingi chooni.
Chelsea nayo yatunguliwa!
Chelsea, ikiwa na Vigogo wao John Terry na Frank Lampard waliokuwa wakicheza Mechi zao za kwanza, walichapwa 2-1 na Eintracht Frankfurt Uwanja wa Commerzbank-Arena.
Ochs ndie aliefunga bao la kwanza kwa Frankfurt lakini Lampard akasawazisha.
Bao la ushindi kwa Frankfurt lilikuwa la penalti iliyofungwa na Mchezaji wa Kimataifa wa Uturuki Halil Altintop.
Arsenal yatwaa EMIRATES CUP
Leo Arsenal imefanikiwa kuifunga Celtic ya Scotland bao 3-2 na kutwaa Kombe lao wenyewe la Emirates.
Kikombe hiki pia kilishirikisha AC Milan na Lyon ambazo zilitoka sare 1-1 katika Mechi ya awali leo.
Arsenal walijikuta wako mbele kwa bao 3-0 lakini Celtic wakaja juu na kufunga bao mbili na nusura wasawazishe.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Calos Vela, dakika ya 3, Sagna, dakika ya 45 na Samir Nasri, dakika ya 51.
Celtic walifunga kupitia Murphy dakika ya 73 na Sung Yong dakika ya 83.
CHEKI: www.sokainbongo.com

Adebayor kuhama Man City?
Kuna taarifa kuwa Emmanuel Adebayor ameambiwa anaweza kuhama Manchester City ikiwa ni Miezi 12 tu tangu atue hapo kwa vishindo akitokea Arsenal.
Inaaminika kuwa Klabu za Italia Juventus na AC Milan ndizo zinazomuwinda lakini huenda tatizo likawa Mshahara wake mkubwa kwa vile analipwa Pauni 130,000 kwa Wiki na Man City na hivyo njia ya mkato ni kwenda huko kwa mkopo tu.
Kuhama kwa Adebayor kunahusishwa na kazi kubwa aliyo nayo Meneja Roberto Mancini kukipunguza Kikosi chake hadi Wachezaji 25 na kukidhi Sheria mpya inayotaka kati ya hao 25 wanane wawe ‘wamelelewa’ kwa Miaka mitatu katika Klabu za England au Wales kabla hawajatimiza Miaka 21.
Inter Milan 3 Man City 0
• Viera awashwa Nyekundu kwa kumpiga kipepsi Materazzi!!!
Katika Mechi ya kirafiki iliyochezwa jana huko Marekani, Mabingwa wa Ulaya Inter Milan wamewachapa Manchester City mabao 3-0 huku Kiungo wa Man City, Patrick Viera, akiwashwa Kadi Nyekundu baada ya kuvaana na Beki mwenye migogoro mingi, Marco Materazzi.
Ilidaiwi Viera, ambae alitokea Inter Milan kabla kujiunga Man City, alimpiga kipepsi Materazzi kwenye dakika ya 21 lakini marudio ya tukio hilo yalionyesha Viera hakuwa na nia hiyo na Materazzi alimdanganya Refa kwa kujifanya kaumizwa.
Mabao ya Inter Milan yalifungwa na Victor Obina, Joleon Lescott wa Man City alijifunga mwenyewe na Christian Biraghi alipachika bao la 3.
Kufuatia mabadiliko ya Kanuni toka kwa FA zilizoanza 2009, Viera hatacheza Mechi 3 za Kirafiki kwa Kadi Hiyo Nyekundu.
Awali, Kanuni zilikuwa hazibagui Mechi za kirafiki na Viera angeweza kuzikosa Mechi za Ligi Kuu.
CHEKI: www.sokainbongo.com

Ozil aiota LIGI KUU
Mchezaji wa Ujerumani alieng’ara huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia, Mesut Ozil, amedokeza kuwa atafurahia akijiunga na Manchester United au Chelsea.
Klabu ya Ozil, Werder Bremen, imeshakata tamaa kumbakiza Klabuni hapo na ishaona ni afadhali imuuze sasa kuliko kusubiri Mkataba wake uishe Mwakani na kukosa hata Senti moja.
Inaaminika Werder Bremen wakipewa dau la Pauni Milioni 13 watamuuza Ozil.
Aurelio arudi tena Anfield
Beki kutoka Brazil, Fábio Aurélio, Miaka 30, ambae aliruhusiwa kuondoka Liverpool Mwezi Mei Mwaka huu baada ya Mkataba wake kumalizika amepewa tena Mkataba mpya wa Miaka miwili.
Meneja wa Liverpool, Roy Hodgson, alimruhusu Aurelio kufanya mazoezi na Liverpool na akaridhika na kiwango chake na kuamua kumpa Mkataba.
Hodgson ametamka: “Niliuliza Klabuni kama Aurelio amepata Klabu mpya na nlipoambiwa bado nikawaambia mwiteni!”
Beki huyo Mbrazil aliichezea Liverpool mara 71 tangu 2006 na kufunga bao 3.
Aurelio anakuwa Mchezaji wa nne kwa Liverpool kumchukua kwa ajili ya Msimu mpya wengine wakiwa Milan Jovanovic, Joe Cole na Danny Wilson.
Powered By Blogger