Saturday 7 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

UEFA CHAMPIONS LIGI: Tottenham kukutana na Young Boys
Tottenham, ambayo haijawahi kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI, imepangwa kucheza na Timu ya Uswisi, Young Boys, katika Raundi ya Mchujo na Washindi wa Raundi hiyo wanaingizwa kwenye droo ya kupanga Makundi.
Tottenham wataanza ugenini Agosti 17 huko Berne, Switzerland Uwanja wa Stade de Suiss na marudiano ni White Hart Lane Agosti 25.
Washindi 10 wa Raundi hii ya Mchujo watajumuika na wale Mabingwa 22 walioingizwa moja kwa moja kwenye Makundi ili kupanga Makundi manane ya Timu nne nne kila moja kwenye Droo itakayofanyika Agosti 26.
Droo kamili ya Raundi hiyo ya Mchuzjo ni:
Young Boys (Switzerland) v Tottenham Hotspur (England)
Sporting Braga (Portugal) v Sevilla (Spain)
Werder Bremen (Germany) v Sampdoria (Italy)
Zenit St Petersburg (Russia) v Auxerre (France)
Dynamo Kiev (Ukraine) v Ajax (Netherlands)
Salzburg (Austria) v Hapoel Tel-Aviv (Israel)
Rosenborg (Norway) v Copenhagen (Denmark)
Basel (Switzerland) v FC Sheriff (Moldova)
Sparta Prague (Czech Republic) v MSK Zilina (Slovakia)
Partizan Belgrade (Serbia) v Anderlecht (Belgium)
Man City bado wanataka Wachezaji wapya
Bosi wa Manchester City, Roberto Mancini, amesema wapo kwenye mazungumzo ili kuwanasa Mario Balotelli na James Milner.
Inadhaniwa mazungumzo kuhusu kumchukua Mario Balotelli kutoka Inter Milan yamekwama kwa vile Mchezaji huyo anataka Mshahara mkubwa.
Kuhusu James Milner, kuna mvutano kati ya Man City na Aston Villa kuhusu ada ya uhamisho.
Licha ya kuwataka Wachezaji hao wawili, Man City inakabiliwa na tatizo kubwa la kupunguza Kikosi chake chenye Wachezaji zaidi ya 30 ili wafikie 25 kama Sheria mpya ya usajili inavyotaka.
EUROPA LIGI: Liverpool kucheza na Trabzonspor ya Poland
Kwenye Raundi ya Mchujo ya EUROPA LIGI itakayochezwa Agosti 19 na marudio Agosti 26, Liverpool imepangiwa kucheza na Klabu ya Poland na Mechi ya kwanza itakuwa Anfield.
RATIBA KAMILI:
AIK Solna v Levski Sofia
AZ Alkmaar v FC Aktobe
Aris Salonika v Austria Vienna
BATE v Maritimo
Bayer Leverkusen v Tavriya Symferopol
Besiktas v HJK Helsinki
Borussia Dortmund v FK Qarabag
CSKA Moscow v Anorthosis Famagusta
CSKA Sofia v The New Saints
Celtic v FC Utrecht
Club Bruges v Dinamo Minsk
Debrecen v Litex Lovech
Dnipro v Lech Poznan
Dundee Utd v AEK Athens
FC Vaslui v Lille
Feyenoord v AA Gent
Galatasaray v Karpaty Lviv
Genk v FC Porto
Getafe v Apoel Nicosia
Grasshoppers v Steaua Bucharest
Gyor ETO FC v Dinamo Zagreb
Hajduk Split v Unirea Urziceni
Lausanne Sports v Lokomotiv Moscow
Liverpool v Trabzonspor
Napoli v Elfsborg
Odense BK v Motherwell
Omonia Nicosia v FC Metalist Kharkiv
PAOK Salonika v Fenerbahce
PSG v Macc Tel-Aviv
Palermo v NK Maribor
Politehnica Timisoara v Man City
Rapid Vienna v Aston Villa
SK Sturm Graz v Juventus
Ibir Novosibirsk v PSV
Slovan Bratislava v VfB Stuttgart
Sporting v Brondby
Villarreal v Dnepr Mogilev

No comments:

Powered By Blogger