Wednesday 8 October 2008


UEFA CUP: Portsmouth kukutana na AC Milan

Portsmouth wamepangiwa timu ngumu ya AC Milan kwenye Kombe la UEFA wakati Aston Villa, Tottenham na Manchester City nao watakuwa na wapinzani wazito.
Aston Villa watacheza na Ajax na Hamburg wakati Tottenham watakabiliwa na Spartak Moscow na Udinese.
Lakini Manchester City, ambao watacheza na Schalke O4, Paris St Germain, Racing Santander na Timu ya Bosi wa zamani wa England Steve McClaren, FC Twente, ndio wenye mtihani mgumu zaidi.
Kila timu iko kwenye Kundi la Timu 5 na watacheza mechi 2 nyumbani na 2 ugenini na wapinzani tofauti.
Timu 3 toka kila Kundi zitasonga mbele.
Fainali ya UEFA CUP itafanyika mjini Istanbull, Uturuki tarehe 20 Mei 2009.

KUNDI A: Schalke 04 Paris St Germain MANCHESTER CITY Racing Santander FC Twente

KUNDI B: Benfica Olympiakos Galatasaray Hertha Berlin Metalist Kharkiv

KUNDI C: Sevilla Stuttgart Sampdoria Partizan Belgrade Standard Liege

KUNDI D: TOTTENHAM Spartak Moscow Udinese Dinamo Zagreb NEC Nijmegen

KUNDI E: AC Milan Heerenveen SC Braga PORTSMOUTH Vfl Wolfsburg

KUNDI F: Hamburg Ajax Slavia Prague ASTON VILLA MSK Zilina

KUNDI G: Valencia Club Brugge Rosenborg FC Copenhagen Saint-Etienne

KUNDI H: CSKA Moscow Deportiva La Coruna Feyenoord Nancy Lech Poznan

No comments:

Powered By Blogger