Sunday 28 September 2008

Tottenham wazidi kushindiliwa misumari: wapigwa 2-0 na Portsmouth!

Sasa kibarua kinazidi kuwa kigumu kwa Meneja wa Tottenham kutoka Spain Juande Ramos baada ya Tottenham kupata kipigo kingine kwenye LIGI KUU leo walipofungwa 2-0 na Portsmouth kwenye Uwanja wa Portsmouth Fratton Park.

Tottenham ndio wameshika mkia kwenye msimamo wa LIGI KUU wakiwa na pointi mbili tu katika mechi 6 walizocheza.

Mabao yaliyowaua Tottenham yalifungwa na Jermaine Defoe na Peter Crouch. Ingawa Portsmouth walimaliza mechi wakiwa 10 baada ya Kiungo wao Lassana Diara kupata kadi mbili za njano na hivyo kutolewa kwa kadi nyekundu Tottenham walionyesha dhahiri hawana ubavu wowote.

Portsmouth: James, Johnson, Campbell, Distin, Belhadj, Little, Diarra, Hughes, Armand Traore, Crouch, Defoe. AKIBA: Ashdown, Kaboul, Hreidarsson, Pamarot, Utaka, Mvuemba, Kanu.

Tottenham: Gomes, Corluka, Dawson, Woodgate, Assou-Ekotto, Bentley, Jenas, Zokora, O'Hara, Gilberto, Pavlyuchenko. AKIBA: Cesar, Huddlestone, Lennon, Bent, Modric, Gunter, Giovani.

REFA: Mike Dean (Wirral).

No comments:

Powered By Blogger