Monday 29 September 2008


RATIBA YA KOMBE la UEFA CHAMPIONS LEAGUE
Kesho na Jumatano viwanja mbalimbali Ulaya vitawaka moto kwa kuzikutanisha Klabu mahiri Ulaya katika mechi za Makundi ya kugombea Kombe la Klabu Bingwa Ulaya-UEFA CHAMPIONS LEAGUE .
Mabingwa watetezi Manchester United walioko Kundi E watakuwa ugenini nchini Denmark kupambana na Aalborg. Katika mechi ya kwanza ya Kundi hili Man U walitoka suluhu na Villarreal huko Old Trafford.
Arsenal watakuwa nyumbani Emirates Stadium kupambana na FC Porto ya Ureno huku wakiomba dua safari hii wapate ushindi baada ya kunusurika kwenye mechi ya kwanza waliposawazisha bao dakika za mwisho walipocheza ugenini na Dynamo Kiev.
Chelsea baada ya kupata ushindi mnono nyumbani Stamford Bridge walipowafunga Bordeaux bao 4-0 sasa watakuwa nchini Romania kupambana na timu mpya kwenye mashindano haya CFR Cluj-Napoca iliyofanya maajabu kwenye mechi ya kwanza ilipoifunga timu yenye uzoefu na ngumu Roma ya Italia nyumbani kwake.
Nao Liverpool baada ya kushinda ugenini kwa bao 2-1 zidi ya Marseille sasa itakuwa nyumbani Anfield kupigana kuendeleza wimbi la ushindi watakapocheza na PSV Eindhoven ya Uholanzi iliyofungwa nyumbani na Atletico Madrid.
Jumanne, 30 Septemba 2008 [saa 3 dak 45 usiku saa za bongo]


KUNDI E

Aalborg v Man U

Villarreal v Celtic

KUNDI F

Bayern Munich v Lyon

Fiorentina v Steau Bucharest

KUNDI G

Arsenal v Porto

Fenrbahce v Dynamo Kiev

KUNDI H

Bate v Juventus

Zenit St Petersburg v Real Madrid

Jumatano, 1 Oktoba 2008 [saa 3 dak 45 usiku saa za bongo]

KUNDI A

CFR Cluj-Napoca v Chelsea

Bordeaux v Roma

KUNDI B

Anorthosis Famagusta v Panathinaikos

Inter Milan v Werder Bremen

KUNDI C

Shakhtar Donetsk v Barcelona

Sporting Lisbon v Basle

KUNDI D

Atletico Madrid v Marseille

Liverpool v PSV

No comments:

Powered By Blogger