Sunday 14 December 2008

GAMBA OSAKA yatinga Nusu Fainali, kuikwaa MAN U Alhamisi!

Leo, Mabingwa wa Asia, Gamba Osaka ya Japan, imeipachika Adelaide United ya Australia, timu iliyoshika nafasi ya pili katika Ubingwa wa Asia. bao 1-0 na kuingia Nusu Fainali watakakopambana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United siku ya Alhamisi tarehe 18 Desemba 2008.
Katika mechi iliyochezwa Toyota Stadium mjini Tokyo, Japan, Mchezaji wa Gamba Osaka Yasuhito Endo alipachika bao la ushindi dakika ya 23.
Timu hizi, Gamba Osaka na Adelaide United, zilikutana wiki kadhaa nyuma kwenye Fainali ya Klabu Bingwa Asia na Gamba Osaka waliibuka kidedea baada ya kuichabanga Adelaide United katika mechi zote mbili jumla ya Mabao 5-0 ikiwa 3-0 mechi iliyochezwa Japan na 2-0 mechi iliyochezwa Australia.

No comments:

Powered By Blogger