Tuesday 16 December 2008

LIGI KUU ENGLAND: Kipindi kigumu kinaingia!!!

Inasemekana, hakika inaaminika hasa kwa wafuatiliaji wazuri wa historia ya LIGI KUU ENGLAND, mechi zinazochezwa mwezi Desemba hasa wakati wa kipindi cha Sikukuu ya Krismas ambako kunakuwa mechi za 'kubanana' na zinazoendelea mfululizo hadi Januari, ndizo zinazotoa mwelekeo wa nani anaweza kuwa Bingwa.
Wakati tunaelekea kipindi hicho, msimamo wa ligi mpaka sasa kwa Timu 5 za juu ni kama ifuatavyo:

-Liverpool mechi 17 pointi 38

-Chelsea mechi 17 pointi 37

-Man U mechi 16 pointi 32

-Aston Villa mechi 17 pointi 31

-Arsenal mechi 17 pointi 30

Mabingwa Watetezi Manchester United wamecheza mechi moja pungufu kwa sababu walienda kucheza mechi ya UEFA SUPER CUP na mechi yao dhidi ya Fulham ikaahirishwa.
Mechi hii sasa imepangwa kuchezwa tarehe 17 Februari 2009.

Ratiba ya mechi za 'VIGOGO' hao wa LIGI KUU katika kipindi hiki ambacho kawaida hutoa fununu wa nani anaunusa ubingwa ni kama ifuatavyo:

[Timu inayotajwa kwanza iko nyumbani]

MANCHESTER UNITED:

-Stoke v Man U [26 Desemba]
-Man U v Middlesbrough [29 Desemba]
-Man U v Chelsea [11 Januari]
-Man U v Wigan [14 Januari] [Hiki ni kiporo.
Mechi hii ilitakiwa ichezwe Desemba 21 lakini Man U watakuwa Japan kwenye Kombe la Dunia la Klabu]

CHELSEA

-Everton v Chelsea [22 Desemba]
-Chelsea v West Brom [26 Desemba]
-Fulham v Chelsea [28 Desemba]
-Man U v Chelsea [11 Januari]

ARSENAL

-Arsenal v Liverpool [21 Desemba]
-Aston Villa v Arsenal [26 Desemba]
-Arsenal v Portsmouth [28 Desemba]
-Arsenal v Bolton [10 Januari]

LIVERPOOL

-Arsenal v Liverpool [21 Desemba]
-Liverpool v Bolton [26 Desemba]
-Newcastle v Liverpool [28 Desemba]
-Stoke v Liverpool [10 Januari]

Hebu tusubiri tuone nani atavuka hivi vigingi na kuibuka kidedea.

No comments:

Powered By Blogger