Sunday 14 December 2008

LIGI KUU ENGLAND: Nao Chelsea wakwama!!!

Chelsea leo wameshindwa kuchukua mwanya wa Liverpool kutoka suluhu ya bao 2-2 na Hull City hapo jana na wao kushinda leo ili wachukue uongozi wa ligi baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na West Ham wakiwa nyumbani kwao Stamford Bridge.
West Ham, wakiongozwa na Meneja wao Gianfranco Zola ambae alikuwa Mchezaji nyota hapo Chelsea, walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Craig Bellamy aliefunga dakika ya 33.
Nicholas Anelka aliisawazishia Chelsea dakika ya 51.
Matokeo hayo yanawafanya Liverpool waendelea kuongoza ligi wakiwa na pointi 38 kwa mechi 17, Chelsea wanafuata pointi 37 kwa mechi 17, kisha Mabingwa Man U pointi 32 mechi 16, Aston Villa pointi 31 mechi 17 na Arsenal ni wa 5 wakiwa na pointi 30 kwa mechi 17.

Portsmouth 0 Newcastle 3

Katika mechi ya awali ya LIGI KUU leo, Newcastle, ikiwa ugenini, iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Portsmouth huo ukiwa wa ushindi wao wa kwanza wa mechi za ugenini msimu huu ambao umewafanya kuchupa hadi nafasi ya 14 kutoka nafasi ya 18.
Hadi mapumziko mechi ilikuwa 0-0 na kipindi cha pili mabao ya Nahodha wao Michael Owens dakika ya 52, Obafemi Martins dakika ya 77 na la Guthrie dakika ya 89 yaliwapa ushindi.

No comments:

Powered By Blogger