Friday 19 December 2008

JOSE MOURINHO: 'Ni furaha kukutanishwa na Timu Bora!!'

-Aikandya ARSENAL!!!

Jose Mourinho, aliekuwa Meneja wa Chelsea na kwa sasa yuko Italia akiiongoza Inter Milan timu ambayo haijachukua Ubingwa wa Ulaya tangu 1965, ametamka ana furaha timu yake kukutana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United kwenye Raundi ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE kwa sababu ndio timu bora.
Mourinho alisema: 'Nimeridhika! Nilitaka timu bora nimeipata! Pengine baada ya siku mbili watakuwa Mabingwa wa Dunia! Wana Mchezaji Bora Ulaya, Ronaldo, Meneja Bora, Ferguson na Kiwanja Bora, Old Trafford!'
Mbali ya Liverpool, watakaopambana na Real Madrid, Timu zote 3 nyingine za England zitapambana na Klabu za Italia kuwania Ubingwa huo wa Klabu za Ulaya.
Chelsea na Juventus, Arsenal na AS Roma, Manchester United na Inter Milan.
Nae Jose Mourinho, kama alivyokuwa Chelsea, hakuacha kukandya!
Alisema: 'Mechi zote 3 kwa Timu za Italia ni fifte fifte lakini AS Roma wanaurahisi kidogo kwa sababu Arsenal sio Chelsea au Manchester United!'


RATIBA:

Jumanne, 24 Februari 2009

Arsenal v AS Roma

Atletico Madrid v FC Porto

Inter Milan v Man U

Lyon v Barcelona

Jumatano, 25 Februari 2009

Chelsea v Juventus

Real Madrid v Liverpool

Sporting v Bayern Munich

Villarreal v Panathinaikos

Jumanne, 10 Machi 2009

Bayern Munich v Sporting

Juventus v Chelsea

Liverpool v Real Madrid

Panathinaikos v Villarreal

Jumatano, 11 Machi 2009

Barcelona v Lyon

FC Porto v Atletico Madrid

Man U v Inter Milan

Roma v Arsenal

No comments:

Powered By Blogger