Monday 15 December 2008

Mabingwa Man U watua Tokyo, Japan kucheza KOMBE LA KLABU BINGWA DUNIANI

Kikosi cha Wachezaji 23 wa Mabingwa wa Ulaya Manchester United kikiongozwa na Meneja wao Sir Alex Ferguson leo asubuhi kimetua Uwanja wa Ndege wa Narita mjini Tokyo [pichani] ili kupambana kwenye Nusu Fainali ya FIFA CLUB WORLD CUP na Gamba Osaka ya Japan ambao ndio Mabingwa wa Asia.
Jana Gamba Osaka iliifunga Adelaide United ya Australia bao 1-0 na kuingia Nusu Fainali.
Mechi hii itachezwa siku ya Alhamisi tarehe 18 Desemba 2008 saa 7 na nusu mchana kwa saa za bongo.
Kikosi cha Man U kilichopo Japan ni:
MAKIPA: Van der Sar, Kuszczak, Amos; WALINZI: Neville, Evra, Ferdinand, Vidic, O'Shea, Evans, Rafael; VIUNGO: Ronaldo, Anderson, Giggs, Park, Carrick, Nani, Scholes, Fletcher, Gibson; WASHAMBULIAJI: Berbatov, Rooney, Tevez, Welbeck.
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Harry Redknapp: 'Bingwa ni Man U au Chelsea!'
Meneja wa Tottenham Harry Redknapp amesema Bingwa wa England msimu huu atakuwa Chelsea au Watetezi Man U na hadhani kama Liverpool ana ubavu wa kuhimili mikikimikiki ya muda mrefu.
Redknapp, ambae Timu yake Tottenham ililazimisha sare ya 0-0 ilipocheza na Mabingwa Man U juzi, alisema: 'Mmoja kati ya Chelsea au Man U atashinda. Arsenal wamepoteza pointi nyingi na siwaoni kama wanaweza kurudi kwenye kinyang'anyiro! Nao Liverpool wanawategemea sana Steve Gerrard na Fernando Torres! Sijui kiktokea kitu kwa hao wawili watafanya nini na hivyo wana mapungufu ukilinganisha na vikosi vya Chelsea na Man U!'
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
LIGI KUU ENGLAND: MECHI ZA WIKIENDI [saa ni za bongo]
JUMAMOSI, 20 Desemba 2008
[saa 12 jioni]

Blackburn v Stoke

Bolton v Portsmouth

Fulham v Middlesbrough

Hull v Sunderland

[saa 2 na nusu usiku]

West Ham v Aston Villa

JUMAPILI, 21 Desemba 2008

[saa 10 na nusu jioni]

West Brom v Man City

[saa 12 jioni]

Newcastle v Tottenham

[saa 1 usiku]

Arsenal v Liverpool

JUMATATU, 22 Desemba 2008
[saa 5 usiku]

Everton v Chelsea

No comments:

Powered By Blogger