Tuesday 16 December 2008

Rooney, Ronaldo wanusurika adhabu

Nyota wa Manchester United, Wayne Rooney na Cristiano Ronaldo, wamenusurika kubandikwa adhabu na UEFA na FA baada ya kutuhumiwa kutenda makosa katika mechi na makosa hayo kutoonwa na Marefa wa mechi hizo.
Rooney alituhumiwa kumkanyaga Mlinzi wa Aalborg ya Denmark Kasper Risgard kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE kati ya Man U na Aaalborg iliyochezwa Old Trafford Jumatano iliyopita.
Baada ya UEFA kupitia mkanda wa video wameamua hakuna hatua zozote zinastahili kuchukuliwa.
Baada ya mechi hiyo, Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, aliwapandishia Waandishi wa Habari kwa kulivalia njuga tukio ambalo halikustahili chochote.
Nae Ronaldo alituhumiwa kumpiga teke Mlinzi wa Tottenham Michael Dawson kwenye mechi ya Tottenham na Manchester United siku ya Jumamosi.
FA ilimtaka Refa wa pambano hilo Mike Dean kulitazama tena tukio hilo kwenye video na kuamua kama angeliliona angechukua hatua gani lakini Dean alithibitisha hata kama angeliona asingempa Ronaldo Kadi Nyekundu.

No comments:

Powered By Blogger