Sunday 14 December 2008

LIGI KUU ENGLAND: Liverpool, Arsenal na Man U wabanwa mbavu! Chelsea leo!

Vigogo Man U, Liverpool na Arsenal jana walitoka suluhu katika mechi zao za LIGI KUU na sasa nafasi iko wazi kwa Chelsea kuchukua uongozi wa ligi hiyo toka mikononi mwa Liverpool endapo watawafunga West Ham kwenye mechi yao ya leo itakayochezwa Stamford Bridge saa 1 usiku saa za bongo.
Liverpool, akiwa kwake Anfield, alijikuta yuko nyuma kwa bao 2-0 walipocheza na Hull ndani ya dakika 22 za kwanza kwa mabao yaliyofungwa na McShane dakika ya 12 na Beki wa Liverpool Carragher akajifunga mwenyewe dakika ya 22.
Nahodha wa Liverpool Steve Gerrard akaokoa jahazi kwa kurudisha mabao yote kwenye dakika za 24 na 32.
Arsenal waliocheza ugenini uwanjani Riverside dhidi ya Middlesbrough, walipata bao dakika ya 17 kupitia Adebayor lakini Boro wakasawazisha kupitia Mchezaji wao ambae zamani alikuwa Arsenal Aliadiere dakika ya 29.
Nao Mabingwa Man U wakicheza ugenini White Hart Lane nyumbani kwa Tottenham, walilazimishwa sare ya 0-0 huku Kipa wa Spurs Gomez akiibuka nyota kwa kuokoa mipira mingi ya hatari ya Wachezaji wa Man U.
Ronaldo alifanikiwa kupachika bao lakini Mwamuzi Mike Dean alilikataa kwa kudai aliunawa kabla ya kufunga.

MATOKEO MECHI NYINGINE:

Aston Villa 4 Bolton 2

Man City 0 Everton 1

Stoke o Fulham 0

Sunderland 4 West Brom 0

Wigan 3 Blackburn 0

MECHI ZA LEO:

Portsmouth v Newcastle [saa 10 na nusu mchana]

Chelsea v West Ham [saa 1 usiku]

LA LIGA: Barcelona 2 Real Madrid 0

Magoli yaliyofungwa na Samuel Etoo dakika ya 80 na Lionel Messi kwenye dakika za majeruhi yamewaua Mahasimu Real Madrid na kuwafanya Barcelona waendelee kuongoza Ligi ya Spain na kuwa pointi 12 mbele ya Real Madrid.

FIFA CLUB WORLD CUP:

Leo ni mechi kati ya Mabingwa wa Asia, Gamba Osaka ya Japan na Adelaide United ya Australia ambao ni Washindi wa pili wa Klabu Bingwa Asia.
Katika mechi ya awali, Adelaide United waliifunga Waitakere United ya New Zealand 2-0.
Mshindi wa mechi hii atapambana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United siku ya Alhamisi Desemba 18 katika Nusu ya pili.

No comments:

Powered By Blogger