Tuesday 16 December 2008

PAUL INCE ATIMULIWA BLACKBURN!!

Klabu ya Blackburn Rovers imemfukuza kazi Meneja wake Paul Ince kufuatia matokeo mabaya kwenye LIGI KUU.
Ince alijiunga Blackburn mwezi Juni akitoka MK Dons na kuiongoza timu hiyo kwenye mechi 17 za LIGI KUU lakini wameshinda mechi 3 tu kati ya hizo na ushindi wao wa mwisho ulitokea Septemba 27 walipoifunga Newcastle.
Kwa sasa Blackburn ipo nafasi ya 19 kwenye msimamo wa ligi yaani timu ya pili toka mwisho.
Mwenyekiti wa Blacburn John Williams akitangaza uamuzi huo wa kumtimua alisema: 'Ushindi wa mechi 3 katika 17 kwa timu iliyomaliza ligi nafasi ya 7 msimu uliopita na kutufanya sasa tuwe wa 19 kati ya timu 20 haukubaliki!'
Paul Ince ameweka historia ya kuwa Meneja wa kwanza mweusi kuongoza klabu iliyo LIGI KUU.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Benitez alazwa hospitali jana, augua ugonjwa uleule uliomlaza Scolari juzi!!!
Klabu ya Liverpool imethibisha Meneja wao Rafa Benitez alikimbizwa hospitali Jumatatu usiku na inabidi afanyiwe operesheni ndogo baadae wiki hii kwa kuwa anasumbuliwa na vijiwe kwenye figo.
Taarifa hizi zimekuja masaa 24 tu tangu Meneja wa Chelsea Luis Felipe Scolari alazwe hospitali kwa usiku mmoja kwa tatizo la aina hiyohiyo.
Katika msimamo wa LIGI KUU, Liverpool ndio inaongoza ikifuatiwa na Chelsea walio pointi moja nyuma.

No comments:

Powered By Blogger