Thursday 11 December 2008

Baada ya Miaka 40 Tuzo ya 'BALLON d'OR' yarudi OLD TRAFFORD!!!

Kabla ya kuanza mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE iliyochezwa Jumatano kati ya Manchester United na Aalborg uwanjani Old Trafford, Cristiano Ronaldo alietunukiwa 'Ballon d'Or' [KOMBE LA DHAHABU] kudhihirisha yeye ndie MCHEZAJI BORA ULAYA mwaka huu, alitambulishwa rasmi na kukabidhiwa tena Kombe hilo uwanjani hapo huku akiwa amesindikizwa na Wachezaji wa zamani wa Manchester United Dennis Law, alieshinda tuzo hiyo mwaka 1964 na Sir Bobby Charlton alieipata 1966.
Mchezaji wa mwisho wa Manchester United kushinda Tuzo hiyo ni George Best alietunukiwa mwaka 1968.
George Best ni marehemu.

No comments:

Powered By Blogger