Sunday 7 December 2008

RONALDO AKABIDHIWA TUZO YA 'Ballon d'Or'

Leo, mjini Paris, Ufaransa, nyota wa Mabingwa wa Uingereza na Ulaya, Manchester United, Cristiano Ronaldo, amekabidhiwa Tuzo inayotukuka ya Ballon d'Or, yaani 'MPIRA WA DHAHABU' inayoashiria yeye kwa sasa ndie MCHEZAJI BORA ULAYA.
Ronaldo, ambae vilevile ndie anaetegemewa sana kushinda Tuzo ya MCHEZAJI BORA WA DUNIA inayotolewa na FIFA, ameshashinda Tuzo ya MCHEZAJI BORA WA DUNIA YA FIFPRO ambayo hutolewa na Wachezaji wa Kulipwa.
Akipokea Tuzo hiyo, huku Mama yake Mzazi aitwae Maria na Meneja wa Klabu yake Sir Alex Ferguson wakiwepo [tizama picha] kwenye ghafla iliyorushwa moja kwa moja kwenye televisheni, Ronaldo alitoa shukrani zake za dhati.
Sir Alex Ferguson alitoa nasaha zake kwenye ghafla hiyo kwa kusema: 'Cristiano, tunasikia fahari sana, wewe ni mfano bora kwa vijana wote duniani wanaokuja Manchester kutoka nje! Sasa endelea mazoezi ili ushinde, endeleza kipaji chako! Hongera! Endelea hivihivi!'
Nao Mameneja wa Chelsea, Felipe Scolari na wa Arsenal, Arsene Wenger, nao walipewa ruhusa ya kuongea kwa njia ya video.
Luis Felipe Scolari aliewahi kuwa Kocha wa Ronaldo kwenye Timu ya Taifa ya Ureno alisema: 'Hii ni tuzo yako ya kwanza kwa yote uliyofanya lakini sio ya mwisho. Hii itakuwa moja ya nyingi utakazopata kwenye historia yako.'
Arsene Wenger alisema wakati Ronaldo amesimama bega kwa bega na Ferguson kwenye ghafla hiyo: 'Una kipaji kikubwa sana! Nawapongeza nyote wawili kwani hii ni kazi ya pamoja.'

No comments:

Powered By Blogger