Thursday 11 December 2008

FIFA CLUB WORLD CUP JAPAN 2008 yaanza!!!

Mabingwa wa Afrika Al Ahly kucheza Jumamosi, Man United dimbani wiki ijayo!!!!!

Leo mashindano ya kugombea 'KOMBE LA KLABU BINGWA YA DUNIA' yajulikanayo kama 'FIFA CLUB WORLD CUP JAPAN 2008' yameanza rasmi huko Tokyo, Japan kwa mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa kati ya Adelaide United, Washindi wa Pili wa Klabu Bingwa Asia wanaotoka Australia, na Waitakere United ya New Zealand, ambayo inawakilisha Timu kutoka Nchi za Oceania.
Katika mechi hiyo ya ufunguzi, Adelaide United ilibwaga Waitakere United kwa mabao 2-1 wafungaji wakiwa ni Daniel Mullen na Travis Dodd kwa Adelaide kwenye dakika ya 38 na 83.
Paul Seaman aliifungia Waitakere dakika ya 34.
Sasa Adelaide United wanasonga mbele na watakutana na Gamba Osaka ya Japan ambao ndio Mabingwa wa Bara la Asia mchezo ambao utachezwa Toyota Stadium, mjini Tokyo, Japan siku ya Jumapili tarehe 14 Desemba 2008.
Kesho ni mapumziko na siku ya Jumamosi tarehe 13 Desemba 2008, Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri, inashuka dimbani National Stadium, Tokyo, Japan kucheza na Pachuca ya Mexico ambao ni Mabingwa wa CONCACAF [Nchi za Marekani ya Kati, Kaskazini na Carribean].
Mshindi wa mechi hii atapambana na Liga de Quito ya Ecuador, Mabingwa wa Nchi za Marekani ya Kusini kwenye Nusu Fainali ya kwanza.
Mabingwa wa Ulaya, Manchester United, wao wameingizwa moja kwa moja Nusu Fainali ya pili na watapambana na mshindi wa mechi kati Adelaide United na Gamba Osaka hapo Alhamisi tarehe 18 Desemba 2008 mjini Yokohama, Japan.

No comments:

Powered By Blogger