Saturday 13 December 2008

Mabingwa wa Afrika Al Ahly yatolewa nje KLABU BINGWA DUNIANI!
Wabandikwa 4-2 na Pachuca!!!

Leo Jumamosi tarehe 13 Desemba 2008, Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri, waliingia dimbani National Stadium, Tokyo, Japan kucheza na Pachuca ya Mexico ambao ni Mabingwa wa CONCACAF [Nchi za Marekani ya Kati, Kaskazini na Carribean].
Al Ahly walikuwa wakiongoza mabao 2-0 huku la kwanza Pachuca wakijifunga wenyewe kupitia Fausto Pinto na la pili akafunga Mshambuliaji wa Al Ahly kutoka Angola Amado Flavio.
Pachuca wakasawazisha kupitia Luis Montez na Christian Gimenez dakika ya 47 na 73.
Mpaka dakika 90 kumalizika mabao yalibaki 2-2 na dakika 30 za nyongeza zikachezwa.
Pachuca wakatoka kifua mbele kwa mabao ya Damian Alavarez dakika ya 98 na Gimenez akaongeza la 4 dakika ya 110.
Pachuca sasa watapambana na Liga de Quito ya Ecuador, Mabingwa wa Nchi za Marekani ya Kusini kwenye Nusu Fainali ya kwanza itakayochezwa Jumatano tarehe 17 Desemba 2008 .
Kesho ni mechi kati ya Mabingwa wa Asia, Gamba Osaka ya Japan na Adelaide United ya Australia ambao ni Washindi wa pili wa Klabu Bingwa Asia.
Mshindi wa mechi hii atapambana na Mabingwa wa Ulaya Manchester United siku ya Alhamisi Desemba 18 katika Nusu ya pili.

No comments:

Powered By Blogger