Monday 2 March 2009

Wenger bado ana imani licha ya Timu kuzomewa na Washabiki wao Emirates!!!

Bosi wa Arsenal, Arsene Wenger, ameonyesha kustaajabu kwa nini Mashabiki wa Arsenal wamepoteza imani wakati yeye na Timu yote bado wana imani kubwa na uwezo wao.
Mara baada ya filimbi ya mwisho baada ya pambano la LIGI KUU dhidi ya Fulham lililochezwa Emirates Stadium nyumbani kwa Arsenal kuisha 0-0 ikiwa ni suluhu ya nne mfululizo ya bila magoli kwa Arsenal kwenye ligi, Mashabiki wao waliwazomea Wachezaji wao.
Arsene Wenger amesema: 'Sijui kwa nini Mashabiki hawana imani! Hilo halinisumbui! Kitu muhimu ni kuwa ninaamini tunachofanya ni sawa. Kuzomewa si tatizo, tatizo ni kuwa tunashindwa kushinda mechi tunazotakiwa kushinda!'

Ferguson aitaka Timu kuwa makini!

Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, baada ya kutwaa taji jingine tena safari hii ikiwa Kombe la Carling, ametaka kikosi chake kuwa makini na kutuliza akili huku wakipigania kutetea Ubingwa wao kwenye LIGI KUU England na UEFA CHAMPIONS LEAGUE pia na wakiwania kulitwaa Kombe la FA.
Ferguson amenena: 'Nina uzoefu mkubwa sana wa kujua Soka ni mchezo katili! Tunaweza kutwaa Vikombe vyote msimu huu lakini pia inawezekana wikiendi ijayo tukaenda kucheza na Fulham na mpira ukambabatiza mtu matakoni na kuingia goli, tumefungwa, tumetolewa nje ya FA Cup! Nani anajua hilo?'
Hata hivyo Sir Alex Ferguson amekiri wikiendi hii imekuwa njema sana kwao baada ya kuwaona wapinzani wao wakubwa Liverpool wakifungwa na hivyo kupoteza pointi muhimu kwenye LIGI KUU na pia Man U kutwaa Carling Cup.
Ferguson alimalizia: 'Kitu muhimu sasa ni kutilia mkazo mechi ya Jumatano tunayocheza ugenini na Newcastle LIGI KUU na kuhakikisha tunashinda'

Kipa Ben Foster wa Man U atoboa siri ya umahiri wa kuokoa penalti Fainali Carling Cup

Golikipa wa Manchester United, Ben Foster ]25], kawaida ni Kipa wa Akiba lakini alicheza Fainali ya Carling Cup dhidi ya Tottenham jana kufuatia msimamo wa Bosi wao Sir Alex Ferguson kuchezesha chipukizi na wale wasiokuwa na namba kwenye Kikosi cha Kwanza kwenye mashindano hayo ya Kombe la Carling.
Ben Foster aliibuka shujaa wa mechi hiyo na kuondoka na Tuzo Maalum ya Mchezaji Bora wa fainali hiyo na pia kuibua tena zile imani kuwa yeye ndie Kipa Bora wa England, msimamo ambao wengi walikuwa nao lakini ukafifia kwani Foster alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu baada ya kuumia goti.
Foster ametoboa kuwa kilichomsaidia kuukoa penalti ya kwanza ya Tottenham iliyopigwa na Jamie O'Hara ni kwa sababu yeye na Kocha wa Makipa wa Man U Eric Steele, kabla ya penalti kupigwa, walikuwa wanacheki iPod [kifaa sawa na simu ya mkononi kinachorekodi na kuchezesha video] iliyokuwa na Wachezaji mbalimbali wa Tottenham wakiwa wanapiga penalti.
Hivyo, Foster alidai, walijua O'Hara akipiga basi atapiga juu kidogo na kushoto kwake na hilo kweli lilitokea.

No comments:

Powered By Blogger