Thursday 24 July 2008

Sunderland wametangaza kumsaini kiungo wa Tottenham Teemu Tainio, umri miaka 28 ambae ni raia wa Finland, kwa mkataba wa miaka mitatu.
Wachezaji wengine wa Tottenham wanaohusishwa kujiunga na Sunderland ni Steed Malbranque, Younes Kaboul na Pascal Chimbonda.

Nao West Ham wamemsajili mchezaji wa Kimataifa wa Uswisi Valon Behrami kutoka Lazio ya Italia.
Behrami, miaka 23, hucheza kama beki wa kulia au kiungo, amesaini mkataba wa miaka mitano na aliichezea Uswisi mechi zake zote za EURO 2008.

No comments:

Powered By Blogger