Saturday 26 July 2008

TEVEZ KUBAKI MAN U KWA MKATABA WA KUDUMU!!
DAU LA KUMBAKISHA MAN U LITAVUNJA REKODI UINGEREZA!
Muargentina Carlos Tevez ambae yuko MAN U kwa mkataba wa mkopo wa miaka miwili unaoisha mwakani atasainiwa MAN U kwa dau la Pauni milioni 32 ambalo litavunja rekodi ya kumnunua mchezaji Uingereza.

Rekodi ya sasa inashikiliwa na Chelsea pale walipomsaini Andrei Shevchenko kwa Pauni milioni 30 miaka miwili iliopita.
Carlos Tevez anamilikwa na Kampuni iitwayo MSI ingawa Man U walilazimika kuwalipa fidia Klabu ya West Ham aliyochezea Tevez kabla kuchukuliwa na Man U kwa mkopo Agosti, 2007.

Tevez ameshachezea Man U mechi 39 na kufunga mabao 19 yaliyoiwezesha Man U kutwaa Ubingwa wa LIGI KUU UINGEREZA na Ubingwa wa Klabu za ULAYA.
Kwa sasa anaonekana ni muhimu sana hasa kuhusu hatma ya hatihati ya 'kigeugeu' Ronaldo.

No comments:

Powered By Blogger