Monday 3 November 2008


Bolton 2 Man City 0

Mabao mawili yaliyofungwa mwishoni kipindi cha pili yameiwezesha Bolton kuwafunga Manchester City na hivyo kujikwamua kutoka kwenye nafasi tatu za mwisho za msimamo wa LIGI KUU.
Robinho aliupoteza mpira katikati ya uwanja na Bolton wakapanda kufanya shambulizi la haraka lililomkuta Mjamaica Gardner aliepachika bao kwenye dakika hiyo ya 77. Gardner alikuwa resevu kwenye mechi hii na aliingizwa dakika ya 43 kuchukuwa nafasi ya Riga.
Zikiwa zimebaki dakika 2 mechi kuisha, Gardner alipenyeza krosi murua ambayo katika harakati za kuokoa Richard Dunne wa Manchester City akajifunga mwenyewe.

No comments:

Powered By Blogger