Sunday 2 November 2008

Vinara Liverpool wapigwa !!!, Chelsea aua !!!, Arsenal auawa !!!, Man U washinda !!!

Mechi za jana za LIGI KUU zilileta msismko ambao hakika utakuwa umeusisimua ulimwengu wa soka na kuwafurahisha baadhi ya mashabiki, kuwavunja moyo wengine na kuwafanya wengine wabaki wakiomba Mungu!
Ni matokeo ambayo polepole yanaanza kuleta picha ni nani wa kuwatolea macho kwenye msimu hu, ni nani hasa wana uchu na Ubingwa.

Tottenham 2 Liverpool 1

Roman Pavlyuchenko, Mrusi aliehamia Tottenham msimu huu, alipachika bao la ushindi kwenye dakika ya 90 na kuvunja rekodi ya Liverpool ya kutofungwa kwenye LIGI KUU msimu huu na vilevile kuwasaidia Chelsea kuwang'oa toka kileleni!
Ushindi huu vilevile umeashiria himaya nzuri kwa Meneja mpya Harry Redknapp ambae ni mechi yake ya tatu tu tangu atue hapo akitokea Portsmouth.
Mechi ya kwanza waliishinda Bolton 2-0 wikiendi iliyopita na Jumatano wakatoka suluhu 4-4 na Arsenal.
Liverpool walianza mechi hii iliyochezwa White Hart Lane, nyumbani kwa Tottenham, kwa kishindo pale walipopachika bao dakika ya 3 tu ya mchezo kupitia Dirk Kuyt na walitawala mechi yote.
Lakini kipindi cha pili mambo yalienda kombo na Liverpool wakajifunga wenyewe bao kupitia Carragher kufuatia kona na akajikuta akipiga kichwa wavuni.

Chelsea 5 Sunderland 0

Chelsea wakiwa kwao Stamford Bridge waliwashindilia Sunderland mabao 5-0 na kuchukua uongozi wa LIGI KUU baada ya Liverpool kufungwa na Tottenham.
Nicolas Anelka alipachika mabao 3 kwenye dakika za 30, 45 na 53, Alex dakika ya 27 na Lampard dakika ya 51.

Stoke City 2 Arsenal 1

Rory Delap na mipira yake ya kurusha jana iliwaua Arsenal baada ya Ricardo Fuller na Seyi Olofinjana kuunganisha mipira hiyo ya kurusha na kutikisa nyavu kwenye dakika za 11 na ya 73.
Gael Clichy aliipatia Arsenal bao lake dakika ya 90 baada ya shuti lake kuwababatiza Wachezaji watatu na kutinga wavuni.

Man U Hull City 3

Man U walitawala mechi hii na kukosa rundo la mabao lilowafanya dakika za mwisho wajikaze sana ili Hull City wasisawazishe.
Man U walijikuta wako mbele 4-1 kwa mabao kupitia Ronaldo aliefunga bao la kwanza lakini Hull wakasawazisha kupitia Daniel Cousin. Michael Carrick akaipatia Man U bao la pili, Ronaldo la tatu na Nemanja Vidic akafunga la nne na kuwafanya Man U wawe burudani mbele kwa mabao 4-1.
Ndipo wakaibuka Hull City kwa kufunga bao la pili kupitia Bernand Mendy na Rio Ferdinand akatoa penalti iliyofungwa vizuri na Geovanni na kufanya gemu kuwa 4-3.

MATOKEO MECHI NYINGINE:

Everton 1 Fulham 0

Luis Saha alifunga bao lake la kwanza tangu ahamie Everton kutokea Man U kwa kichwa kwenye dakika ya 87.

Middlesbrough 1 West Ham 1

Mullins wa West Ham aliipa bao dakika ya 11 lakini Mmisri Mido aliisawazishia Middlesbrough kwenye dakika ya 83.

Portsmouth 1 Wigan 2

Amr Zaki toka Misri aliifungia Wigan bao la kwanza kwa penalti dakika ya 45 lakini Kranjcar akaisawazishia Portsmouth dakika ya 82.
Emile Heskey akaipa ushindi Wigan kwenye dakika za majeruhi.
Hiki ni kipigo cha pili mfululizo kwa timu aliyoiacha Meneja Harry Rednapp aliehamia Tottenham na Timu kuchukuliwa na Meneja mpya Tony Adams.

West Brom 2 Blackburn 2

Andrews alifunga bao la kusawazisha dakika ya 89 na kuwaokoa Blackburn toka kipigoni baada ya West Brom kuongoza kwa mabao 2-1 yaliyofungwa na Bednar, dakika ya 55, na Miller dakika ya 62 ingawa walikuwa ni Blackburn waliopata bao la kwanza kupitia Benni McCarthy toka bondeni Afrika Kusini aliefunga kwa penalti dakika ya 13.
McCarthy alikung'utwa kadi nyekundu baadae kwenye dakika ya 36 ya mechi hiyo baada kupewa kadi mbili za njano.

No comments:

Powered By Blogger