Monday 3 November 2008

RATIBA LIGI KUU LEO Jumanne, 3 Novemba 2008:

Newcastle v Aston Villa

St James Park, nyumbani kwa Newcastle, leo kutakuwa na mpambano wa LIGI KUU kati ya wenyeji Newcastle na Aston Villa, mechi ambayo itaanza saa 5 usiku saa za Afrika Mashariki.
Newcastle mpaka sasa wana pointi 9 tu kwa mechi 10 walizocheza na wako nafasi ya 20 kwenye msimamo wa ligi, nafasi ambayo ni ya mwisho.
Aston Villa wako nafasi ya 5 wakiwa na pointi 20 kwa mechi 10 walizocheza.
Leo Newcastle wanategemewa kuwachezesha mastaa wao Michael Owens na Nicky Butt ambao wote walikuwa majeruhi.
Refa kwenye mechi atakuwa Steve Bennet.

No comments:

Powered By Blogger