Saturday 21 March 2009

Arsenal wainyuka Newcastle 3-1!

Magoli kupitia kwa Niklas Bendtner, Abou Diaby na Samir Nasri yamewapa Arsenal ushindi mnono ugenini wa bao 3-1 dhidi ya Newcastle ambayo ipo hatihati ya kuporomoka daraja.
Ushindi huu wa Arsenal pia unawaongezea nguvu ya kuchukua kiuhakika nafasi ya nne msimamo wa ligi kwani sasa wako pointi 3 mbele ya Aston Villa.
Villa kesho wako ugenini Anfield kumenyena na Liverpool.

Baada ya kipigo cha 2-0 cha Fulham, Ferguson asema: 'Inasikitisha lakini Refa ni Phil Dowd, ulitegemea nini?'
Nae Hodgson wa Fulham akiri bahati na kujituma kumewapa ushindi!

Ferguson amekubali Fulham walicheza vizuri sana kipindi cha kwanza lakini maamuzi ya Refa Phil Dowd yamechangia wao kufungwa.
Ferguson amedai Kadi ya Njano ya pili kwa Rooney haikustahili kabisa kwani alirusha mpira pale frikiki ilipotakiwa kupigwa.
Ferguson alidai: 'Ni Refa Phil Dowd unategemea nini? Lakini si kosa la Refa tu tujilaumu wenyewe pia!'
Meneja wa Fulham, Roy Hodgson, amesema bahati na kujituma kupita kiasi ndio kilichowapa ushindi.

No comments:

Powered By Blogger