Saturday 21 March 2009

Wakati Mabingwa Man U wapata kipigo cha pili mfululizo LIGI KUU England, Chelsea nao watunguliwa!!

Fulham, wakiwa nyumbani kwao Craven Cottage huku wakipata msaada mkubwa wa Refa Phil Dowd aliewatwanga Wachezaji wa Man U Paul Scholes na Wayne Rooney Kadi Nyekundu, wameifunga Man U bao 2-0 hiki kikiwa kipigo cha pili mfululizo kwa Mabingwa hao.
Wiki iliyokwisha walifungwa 4-1 na Liverpool.

Chelsea, wakiwa nyuma ya Man U kwa pointi 4 ingawa Man U ana mechi moja mkononi, wameshindwa kupunguza tofauti ya pointi baada ya kupigwa na wenzao wa London, Tottenham, bao 1-0.

Matokeo mechi nyingine za LIGI KUU leo:

Blackburn 1 West Ham 1

Stoke 1 Middlesbrough 0

West Brom 1 Bolton 1

Portsmouth 2 Everton 1

Sasa hivi mechi kati ya Newcastle na Arsenal ndio inaanza.

Vikosi ni kama ifuatavyo:

Newcastle: Harper, Steven Taylor, Coloccini, Bassong, Jose Enrique, Ryan Taylor, Butt, Nolan, Duff, Lovenkrands, Martins.

Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Toure, Clichy, Arshavin, Denilson, Diaby, Nasri, Van Persie, Bendtner.

No comments:

Powered By Blogger