Thursday 20 August 2009

LIGI KUU ENGLAND: MAN U WABAMIZWA, LIVERPOOL, TOTTENHAM ZATOA VIPIGO & BIRMINGHAM YAJIKONGOJA!!!!
Katika mechi za Ligi Kuu zilizochezwa jana usiku, Mabingwa watetezi Manchester United, wakicheza soka bovu sana ambalo lilimkasirisha hata Meneja Sir Alex Ferguson, walichapwa na Burnley Timu iliyopanda Daraja msimu huu kwa mara ya kwanza katika muda wa miaka 33.
Burnley walipata ushindi wa bao 1-0 huku Man U wakikosa kufunga penalti aliyopiga Michael Carrick na kuokolewa na Kipa wa Burnley.
Mahasimu wa Man U, Liverpool, baada ya kupigwa 2-1 na Tottenham katika mechi ya kwanza ya Ligi, jana waliangusha mkong’oto kwa Stoke City wa mabao 4-0 wakiwa kwao Anfield.
Nao Tottenham wakicheza ugenini walipata ushindi wao wa pili mfululizo pale walipowapiga Hull City mabao 5-1. Na Birmingham waliipachika Portmouth bao 1-0.
LIGI KUU itaendelea wikiendi hii kwa Ratiba ifuatayo:
Jumamosi, Agosti 22
[Saa 11 jioni bongo taimu]
Arsenal v Portsmouth
Birmingham v Stoke City
Hull City v Bolton
Man City v Wolverhampton
Sunderland v Blackburn
Wigan v Man U
Jumapili, Agosti 23
[Saa 9 na nusu mchana]
West Ham v Tottenham
[Saa 11 jioni]
Burnley v Everton
[Saa 12 jioni]
Fulham v Chelsea

Jumatatu, Agosti 24
[Saa 4 usiku]
Liverpool v Aston Villa

No comments:

Powered By Blogger