Thursday 20 August 2009

Mwana wa Sir Alex Ferguson matatani!!!!
Mtoto wa Sir Alex Ferguson, Darren Ferguson ambae ni Meneja wa Klabu ya soka ya Peterborough United, timu iliyo Daraja chini tu ya Ligi Kuu England liitwalo Coca Cola Championship, ameshitakiwa na FA, Chama cha Soka England, kwa kosa la kumtukana Refa mara tu baada ya mechi ya Ligi ambapo Timu yake ilifungwa bao 3-2 na West Bromwich Albion.
Darren Ferguson [pichani], aliepewa mpaka Jumanne ijayo kuwasilisha utetezi wake, alikasirishwa na kitendo cha Refa kuwanyima Peterborough bao la kusawazisha.

No comments:

Powered By Blogger