Friday 4 December 2009

RATIBA LIGI KUU WIKIENDI HII:
JUMAMOSI, DESEMBA 5:
[SAA 9 DAK 45]
Portsmouth v Burnley
[SAA 12 JIONI]
Arsenal v Stoke
Aston Villa v Hull
Blackburn v Liverpool
West Ham v Man U
Wigan v Birmingham
Wolves v Bolton
[SAA 2 NA NUSU USIKU]
Man City v Chelsea
JUMAPILI, DESEMBA 6
[SAA 12 JIONI]
Fulham v Sunderland
[SAA 1 USIKU]
Everton v Tottenham
Portsmouth yashindwa kulipa Wachezaji Mishahara!!!
Kwa mara ya pili sasa katika msimu huu, Klabu ya Ligi Kuu England, Portsmouth, imeshindwa kuwalipa Wachezaji wake Mishahara baada ya baadhi yao kukosa Mishahara ya Novemba.
Portsmouth yenyewe imethibitisha tukio hilo lakini imesema Wachezaji watalipwa leo. Mwezi Septemba Klabu hiyo ilishindwa kulipa Mishahara ingawa baadae walilipwa na Mnunuzi mpya wa Klabu hiyo Sulaiman Al Fahim alieinunua Klabu kutoka kwa Alexandre Gaydamak. Sulaiman kwa sasa ameuza asilimia 90 ya Klabu hiyo kwa Tajiri wa Saudi Arabia Ali Al Faraj lakini Al Faraj alikiri ameinunua Klabu kwa ajili ya faida tu na si Soka.
Kwa sasa Portsmouth imezuiwa na FA kutosajili Mchezaji yeyote hadi watakapozilipa Klabu nyingine Madeni yanayohusiana na ununuzi wa Wachezaji ambayo hawajayalipa.

No comments:

Powered By Blogger