Saturday 5 December 2009

KOMBE LA DUNIA: Wanasemaje Mameneja?
MAKUNDI:
Group A: South Africa, Mexico, Uruguay, France
Group B: Argentina, South Korea, Nigeria, Greece
Group C: England, USA, Algeria, Slovenia
Group D: Germany, Australia, Ghana, Serbia
Group E: Netherlands, Japan, Cameroon, Denmark
Group F: Italy, New Zealand, Paraguay, Slovakia
Group G: Brazil, North Korea, Ivory Cost, Portugal
Group H: Spain, Honduras, Chile, Switzerland
-Meneja wa Ufaransa, Raymond Domenech: "Tupo Kundi gumu! Inabidi tushinde mechi 2 ili kufuzu!"
-Meneja wa Italia, Marcello Lippi: "Inabidi tujitayarishe! Watu wanasema ni Kundi rahisi lakini lazima ufanye matayarisho!"
-Vicente Del Bosque, Meneja wa Spain: "Hatuna malalamiko! Hatuwezi kuficha ukweli kuwa sisi tunaonekana Timu bora!"  
-Meneja wa Ivory Coast, Vahid Halilhodzic: "Tupo Kundi gumu sana na Timu ngumu Brazil na Ureno! Inabidi tufanye maandalizi makali ili tuzipindue Timu hizo kali!"
-Meneja wa Ujerumani, Joachim Loew: "Ghana Timu ngumu, Australia tulicheza nao Kombe la Mabara na tunaiheshimu Serbia!"
-Meneja wa England, Fabio Capello: "Sio mbaya sana! Tushawahi kucheza na USA na Slovenia na kupata ushindi mzuri! Algeria pia wazuri kwani wamewafunga Egypt!! Lakini ikifika Juni mwakani Timu zote zitabadilika!"
-Meneja wa Afrika Kusini, Carlos Alberto Parreira: "Ni Kundi lenye usawa! Inabidi tufanye maandalizi ya hali ya juu na pia Watu wote waishangilie Bafana Bafana!! Hilo ni muhimu!!"

No comments:

Powered By Blogger