Thursday 8 January 2009

FERRARI YA RONALDO ILIVYOBAMIZWA!!
Cristaiano Ronaldo leo asubuhi akiwa njiani kwenda mazoezini alipata ajali wakati akiendesha gari lake la thamani aina ya Ferrari [pichani].
Ingawa yeye mwenyewe hakuumia gari lake hilo la kifahari limeharibiwa vibaya.
Ajali hiyo ilitokea kwenye barabara ya chini ya ardhi inayopita chini ya Uwanja wa Ndege wa Manchester.
Wakati ajali hiyo ikitokea Mchezaji mwenzake wa Man U Kipa Edwin van der Sar alikuwa akija na gari lake nyuma yake nae pia alikuwa akienda mazoezini.
Polisi waliofika mara baada ya ajali walimpima Ronaldo kama alikuwa amelewa au la na walithibitisha vipimo havikuonyesha kama alikuwa na ulevi wa aina yeyote mwilini mwake.
Baadae, Ronaldo aliweza kushiriki mazoezi kama kawaida pamoja na wenzake.

No comments:

Powered By Blogger