Saturday 10 January 2009

LIVERPOOL WAANZA KUWEWESEKA: Meneja Benitez ashangaza dunia kwa kumshambulia Ferguson!

Rafa Benitez ameushangaza ulimwengu wa soka kwa kumshambulia Sir Alex Ferguson na kumtuhumu anaua Marefa.
Meneja huyo wa Liverpool inasadikiwa ameanza kuonyesha dalili za kuchanganyikiwa kwa presha kali ya LIGI KUU England kwa kuingilia kitu ambacho wadau wanahisi hakikumhusu na kutoa maneno makali huku akinukuu vitu alivyoandika kwenye karatasi zake alizoshika mkononi kitu kinachoonyesha alikusudia.
Wiki iliyokwisha Sir Alex Ferguson alikaririwa akitoa tathmini ya Manchester United kwa mwaka 2008 na alisema kuwa timu yake iliathirika kwa kucheza mechi nyingi ugenini hasa baada ya kucheza mechi za UEFA CHAMPIONS LEAGUE nje ya nchi na kujikuta mechi zinazofuata ni za ugenini hasa na timu ngumu za LIGI KUU.
Ukweli ni kwamba Manchester United washacheza na Liverpool, Arsenal, Chelsea, Aston Villa na Everton mechi zote zikiwa ugenini na zote zilifuata baada ya kuwa nje ya nchi.
Timu hizo zote sasa zinatakiwa ziende nyumbani kwa Man U uwanjani Old Trafford.
Rafa Benitez alitoa msisitizo wa kauli zake za ajabu huku akinukuu vikaratasi vyake kwa kudai: 'Ferguson ni Meneja pekee anaua Marefa na haadhibiwi!'
Pengine ni dalili ya kuchanganyikiwa kwa Rafa Benitez kwani amesahau au hataki kukumbuka kwamba Sir Alex Ferguson alipigwa faini ya Pauni Elfu 10 na kufungiwa mechi 2 mwezi Novemba, 2008 kwa kulalamika kuhusu Refa Mike Dean.
Wadau wengi wa Soka England wanamkumbuka Kevin Keagan mwaka 1996, wakati huo akiwa Meneja wa Newcastle na wakati huo ulikuwa kipindi kama cha sasa na walikuwa wakiongoza LIGI KUU kwa pointi 14, akapanda jazba na kulipuka kama Benitez.
Mwisho wa msimu huo, Sir Alex Ferguson na Manchester United ndio waliokuwa Mabingwa!

No comments:

Powered By Blogger